• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WAZIRI NAPE ASISITIZA MATUMIZI MAZURI YA TEKNOLOJIA KATIKA FURSA ZA KIUCHUMI

Posted on: July 18th, 2024

WAZIRI wa Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mh. Nape Nnauye (MB) Julai 17 amefanya ziara Mkoani  Geita  katika Kata ya Nyamigota kijiji cha Luhuha Jimbo la Busanda Halmashauri ya Wilaya ya Geita ambapo amekagua Mnara wa simu uliojengwa na kampuni ya Airtel kwa kushirikiana na Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) ulionzishwa na serikali ili kuwezesha huduma za mawasiliano vijijini.

Mhe Waziri wa Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe Nape Nnauye(MB)  akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Geita na Wananchi Kata ya Nyamigota kijiji cha Luhuha Jimbo la Busanda Halmashauri ya Wilaya ya Geita

Mhe Nape amesema  misingi ya Wizara  ni kuwezesha upatikanaji wa huduma ili kila Mtanzania apate huduma popote, huduma zipatikane kwa ubora na ziweze kupatikana kwa urahisi kwa watumiaji huku zikiwa salama na kuweza kuleta matokeo mazuri.

Waziri wa Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe Nape Nnauye(MB)  ameeleza kuwa Mradi wa ujenzi wa Minara 758 ya simu kwa Teknolojia ya 2G, 3G na 4G utawanufaisha Watanzania Milioni 8.5 waishio katika maeneo ya vijijini

Aidha Mhe Waziri Nape (MB) amewataka wananchi wa Kata hiyo kuhakikisha wanatumia Teknolojia ya Mawasiliano kama fursa katika kufanya biashara kupitia huduma zinazotokana na mawasiliano na si kutumia Teknolojia vibaya kwani Teknolojia huacha alama.

Pamoja na hayo Mhe Waziri Nape (MB) amesema Serikali imeleta kiasi cha Fedha shilingi Bilioni 2.2 kwa ajili ya kutatua changamoto ya Mawasiliano ndani ya mkoa wa Geita katika ujenzi wa miundombinu ya huduma za mawasiliano vijijini.

Bi Justina Mashiba Mkurugenzi wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) amesema zaidi ya wananchi laki 2 wa  wa Mkoa wa Geita watanufaika na Minara 17 ya Mawasiliano ya simu inayojengwa katika Mkoa wa Geita katika kata 16 na vijiji 27 ambapo Serikali imetoa ruzuku ya Shilingi Bilioni 2.2

Mh.Nauye amesema matarajio ya Serikali ni kujenga jumla ya minara 758 kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) Kwa mradi wa Miundombinu ambayo inajengwa Tanzania bara katika mikoa 26 huku akisema Serikali inatoa ruzuku zaidi ya Bilioni 266 ya ujenzi wa Minara hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigela amemshukuru  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuupatia Mkoa wa Geita Shilingi  Bilioni 2.2 kwa ajili ya ujenzi wa Minara ya Mawasiliano  maeneo ya vijijini.

Geita ni mkoa wa 10 kwa kuwa na idadi kubwa ya laini za simu ambapo hadi mwezi Machi 2024 jumla ya laini 2,417,513 zilikuwa zimesajiliwa kutoka laini 2,050,124 mwezi Juni 2022.

Jumla ya Minara 55 imejengwa mkoani Geita kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) katika wilaya 5 za Mkoa wa Geita ambazo ni Bukombe (10) Chato (9) Geita Dc (10) Mbogwe (18) na Wilaya ya Nyang’wale (8) ambapo wananchi 643,354 wananufaika kupitia minara hiyo na katika Minara 758 Tanzania Bara jumla ya minara 17 inatarajiwa kujengwa Mkoani Geita katika kata 16 za Wilaya za Bukombe, Chato, Geita na Mbogwe na kunufaisha wakazi 241,240.


Mhe Nape Nnauye(MB) akisalimiana na Mbunge wa jimbo la Geita Mji Mhe Kanyasu na Wakurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya na Mji Mkoani Geita alipofanya Ziara ya Kukagua hali ya usikivu wa simu na redio mkoani geita 

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa