• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

Historia


Wilaya ya Geita ni moja ya wilaya 5 zinazounda mkoa wa Geita. Ilipata hadhi ya kuwa wilaya mwaka 1962.Kipindi hicho iliitwa Geita province.Wilaya ya Geita ipo kati ya mita 1,100 hadi 1,300 kutoka usawa wa bahari.Pia ipo katika latitudi 208 hadi 3028 kusini mwa mstari wa ikweta na longitudi 32045 na 370 mashariki mwa mstari wa Greenwich.

 Kabla ya Uhuru wa Tanzania bara (Tanganyika),wilaya ya Geita ilikuwa na ukubwa wa kilomita za mraba 16,638 ambapo nchi kavu ilikuwa ni kilomita za mraba 10,123.94 na maji ilikuwa ni kilomita za mraba 6,514.06. Katika kipindi hicho Geita ilikuwa na idadi ya watu wapatao 371,407. Mnamo mwaka 1975 wilaya ya Geita iligawanywa na kupata wilaya ya Sengerema.Baada ya kugawanywa kwa wilaya hizi mbili, Wilaya ya Geita ilibaki na kilometa za mraba 7,825 ambapo nchi kavu ni kilometa za mraba 6,775 na maji ni kilometa za mraba 1,050.

Mnamo mwaka 2013 wilaya ya Geita iligawanywa tena na kupata wilaya ya Nyang'hwale.Wilaya ya Geita ina Halmashauri mbili ambazo ni "Halmashauri ya wilaya ya Geita na Halmashauri ya Mji".Halmashuri ya Geita ina ukubwa wa kilomita za mraba 5,366.7(4,316 nchi kavu na 1,050 maji).

Asili ya jina Geita: Neno Geita limetokana na maneno matatu ya kabila la Wayango (Warongo) ambayo ni Akabanga keita abhantu likiwa na maana kupotea kwa mazingara ambayo yalikuwa kwenye mlima huo wa Akabanga keita abhantu uliokuwa ukitumiwa na warongo kama eneo la mitambiko ya jadi.Jina hili la Geita lilikuwa maarufu kutokana na wazungu kushindwa kutamka maneno Akabanga keita abhantu na hivyo kukatisha kuwa Geita hadi leo.Makabila yaliyokuwepo ya Wazinza, Wasukuma,Wasumbwa na Wasubi wakaigiza matamushi ya wazungu Geita na hivyo neno la Akabanga keita abhantu likaanza kupotea polepole hadi leo.

Wilaya ya Geita hupata mvua yenye wastani wa 900mm-1000mm katika tarafa za Busanda na Kasamwa,pia hupata mvua za wastani wa 1000mm-1300mm katika tarafa za Butundwe na Bugando.

shughuli za uchumi kaika wilaya ya Geita ni;kilimo,ufugaji,uvuvi na uchimbaji wa madini ya dhahabu.

UTAWALA KABLA YA WAKOLONI

Kabla ya kuingia kwa wakoloni (Wajerumani na Waingereza) Geita ilikuwa na tawala za asili saba (7) ambazo ni:

UTAWALA
CHIFU/MTEMI 
 MAKAO MAKUU
Busambilo
Ludomya Ng’hwele
Nyarubele
Msalala
Musa Chasama Mbiti
Kitongo
Buyombe
Mgunga Kadama
Busanda
Buchosa
Paulo Lukakaza
Nyakalilo
Kharumo
Alexander Gerevas
Kharumo
Bukoli
Mganila Nonga
Bukoli
Mwingiro
Nyorobi Mapumba
Idetemya Mwingiro


Wakoloni wa kwanza kuingia Geita walikuwa ni wajerumani ambao utawala wao ulikuwa ni wa moja kwa moja(Direct rule) na hivyo kushindwa kabisa kwani wawakilishi wao waliokuwa wakiletwa toka makao makuu Bagamoyo(Pwani) walikuwa wakiuwawa na wenyeji.

Utawala wa pili ulikuwa wa waingereza baada ya vita kuu ya pili ya dunia,ambao wao walitumia utawala usikuwa wa moja kwa moja(Indirect rule) yaani kwa kuwatumia machifu/watemi wa maeneo husika ili kutekeleza azma/malengo yao.

Eneo la mji wa Geita aliwekwa Liwali Petro Nyango ambaye alifanya kazi chini ya utawala wa kwa eneo la mjini.

 BARAZA LA JADI (NATIVE AUTHORITY)

Baraza hili lilikuwa chini ya uangalizi wa Mkuu wa Wilaya(DC) wa kikoloni,liliundwa na watemi 7 na liwali 1.Mwenyekiti wa baraza hilo alitokana na watemi hao.Aidha katibu wa baraza hilo alitokana na watemi au karani kutoka ofisi ya DC.

Makao makuu ya baraza hilo yalikuwa mjini Geita eneo jirani na Benki ya CRDB, kila mtemi alijengewa nyumba ya kupumnzikia na kulala.

MAJUKUMU YA BARAZA HILO

  • Kusimamia ulinzi na usalama
  • Kusimamia shughuli za maendeleo hasusani katika elimu ya msingi,kilimo mkazo ikiwa zao la pamba na mazao ya chakula(Mahindi,Mtama na Uwele) pamoja na barabara.

Historia ya Wahe. Wenyeviti wa Halmashauri ya wilaya ya Geita

Na
Jina kamili
Mwaka alioanza
Mwaka alioonddoka
1.
Samwel S. Mabeyo
1984
1988
2.
Edward K. Sumuni
1988
1997
3.
Said S. Mahuma
1997
2000
4.
Jeremia M. Ikangala
2000
2010
5.
Musukuma J. Kasheku
2010
2011
6.
Elisha H. Lupuga
2011
-

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa