• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WAZABUNI WABABAISHAJI KUNYIMWA KAZI-GEITA DC

Posted on: January 21st, 2025

Makamu Mwenyekiti Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe Hadija Said, Januari 20 ameongoza wajumbe wa Kamati ya Fedha na Uongozi Halmashauri ya Wilaya ya Geita kukagua miradi ya Maendeleo jimbo la Geita. 

Mhe Hadija  ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Nyamigota ametoa  pongezi kwa Watumishi wa Halmashauri kwa namna ambavyo  wanasimamia miradi  inayotekelezwa na Serikali.

Pamoja na pongezi hizo Makamu Mwenyekiti huyo amewataka  mafundi wanaotekeleza miradi hiyo kuweka bidii ili miradi ikamilike kwa wakati na kuanza kutoa huduma.

" Jitihada ziongezeke na iwapo kuna mkwamo  wowote basi mtoe taarifa kwa Mkurugenzi Mtendaji ili hatua za haraka zichukuliwe" amesisitiza Mhe Hadija katika ziara hiyo.

Kwa upande  wake Diwani wa Kata ya Lwezera Mhe Chinchina amewataka  wahandisi kuzingatia  kuweka mifumo ya kuvuna maji  kwenye shule  ili  yaweze kusaidia katika matumizi mbalimbali. 

" Tunapokuwa na Mifumo ya kuvuna maji  itasaidia  uwepo  wa maji ya kutosha na kusaidia kuzuia magonjwa ya milipuko" Amesema Mhe Chinchina. 

Aidha wajumbe wa Kamati ya Fedha na Uongozi wamempongeza Diwani wa Kata ya Kakubilo Mhe Kessy kwa kutoa  eneo lake kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Msingi  Ikigijo. 

Vilevile Kamati hiyo imewaagiza mafundi kuongeza nguvu kazi ya kutosha ili kuweza Kukamilisha miradi ndani ya muda kwa ubora  unaotakiwa.

Pamoja na kuwasisitiza mafundi ujenzi kuongeza nguvu kazi,  Kamati hiyo imetoa  wito  kwa Watumishi wanaosimamia wazabuni  wanaomba kazi za miradi  kupitia mfumo wa Nest kuepuka kuwapa kazi wazabuni wanaochukua kazi nyingi ilihali hawana uwezo wa kuzitekeleza kwa wakati na kusababisha kuchelewa kukamilika kwa miradi



Kamati ya Fedha na Uongozi ikiwa katika Ujenzi wa Nyumba ya Mtumishi  Shule ya Sekondari Nyakaduha. Mradi huu una Thamani ya Shilingi Milioni 100,000,000 kutoka Serikali Kuu.




Kamati ya Fedha na Uongozi ikiwa katika Mradi wa Ujenzi wa Shule ya Amali Nzera wenye thamani ya Shilingi Milioni 584,280,029


Kamati ya Fedha na Uongozi ikiwa katika Mradi wa Ukamilishaji wa Bweni Shule ya Sekondari Kakubilo  wenye thamani ya Shilingi Milioni 60,000,000 kutoka Serikali Kuu. Kamati hiyo imewataka wanafunzi wanaotumia Bweni hilo kulitunza

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa