• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

"Wanaume wasindikizeni Wenza wenu Kliniki" Asema Munisi

Posted on: August 30th, 2018

Muuguzi Mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Geita bibi Beatrice Munisi amewaasa wanaume nchini kuwasindikiza wenza wao kuhudhuria kliniki katika vituo mbalimbali vya kutolea huduma kwa lengo la kujua maendeleo ya wenza wao na mtoto katika kipindi cha ujauzito.

Ameyasema hayo leo alipokua Akiongea na washiriki wa semina iliyoandaliwa na mradi wa USAID Boresha Afya unaofadhiliwa na shirika la misaada la watu wa  Marekani (USAID) wakati wa majadiliano ya kutengeneza mkataba wa utoaji wa huduma za afya  kati ya Halmashauri na mteja iliyofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita.

Afisa wa Masuala ya Jinsia na vijana kutoka mradi wa boresha afya ndugu Revocatus Kadoshi akitoa ufafanuzi wa namna wauguzi na wakunga wanapaswa kutoa huduma bora kwa jamii

“Kumekuwa na tabia isiyopendeza kwa baadhi ya wanaume kutowasindikiza wenza wao kliniki na hii imepelekea migogoro mikubwa kwenye familia na wengi kutokufuatilia kabisa maendeleo ya mama na mtoto katika kipindi cha ujauzito na kujifungua. Ni wakati sasa wa wanaume kubadilika na kujua mtoto na mama wanahitaji uangalizi mkubwa katika kipindi hicho”. Amesema Munisi

Aidha kwa upande wa afisa wa masuala ya jinsia na vijana kutoka mradi wa USAID Boresha Afya bwana Revocatus Kadoshi amewaomba wauguzi na wakunga kutoa huduma za afya zenye utu, staha na kuzingatia heshima na haki za kijinsia kwa afya ya uzazi, mama wajawazito, watoto wachanga na watoto wenye umri chini ya miaka mitano na huduma rafiki kwa vijana ili kuepuka migogoro na wateja wao.

Semina hiyo imeshirikisha wadau mbalimbali wa afya kutoka Halmashauri za Wilaya na Mji Geita kama vile  waheshimiwa wenyeviti wa Halmashauri,wenyeviti wa kamati za kudumu za huduma za jamii, Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya, viongozi wa dini na wataalam mbalimbali kutoka halmashauri hizo.


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa