• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MADIWANI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WALA KIAPO RASMI KUANZA KUWATUMIKIA WANANCHI

Posted on: December 4th, 2025

Nzera-Geita

Mkutano wa kwanza wa Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Geita umefanyika leo Desemba 04,2025 katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Akifungua  Mkutano huo Katibu Tawala Wilaya ya Geita Bi Lucy Beda amewasihi Madiwani hao kwenda kuwatumikia wananchi ili matarajio yao yaweze kutimia.

Katibu Tawala Wilaya ya Geita Bi Lucy Beda akizungumza katika Mkutano wa Kwanza wa Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Geita ambapo amewataka Waheshimiwa Madiwani kuwatumikia Wananchi walio wachagua ili kutimiza matarajio yao

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita Dkt Alphonce Bagambabyaki akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Serikali kwa kipindi ambacho Baraza lilivunjwa,  amewapongeza Waheshimiwa Madiwani kwa Kuchaguliwa na kuaminiwa na wananchi kutekeleza shughuli za maendeleo ndani ya Halmashauri ,

" Ni imani yetu mtashirikiana kwa umoja, hekima na uwazi katika kupanga, Kushauri na kutekeleza mipango ya maendeleo itakayoboresha maisha ya wananchi katika nyanja zote ikiwepo elimu, afya, miundombinu, uchumi na huduma za kijamii" Amesema Dkt Bagambabyaki.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Halmashaur ya Wilaya ya Geita Dkt Alphonce Bagambabyaki akizungumza Katika Kikao cha Kwanza cha Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Geita na kuwataka Waheshimiwa Madiwani kwenda kutekeleza mipango ya maendeleo itakayoboresha maisha ya wananchi katika Halmashauri

Pamoja  na shughuli nyingine katika Mkutano huo Waheshimiwa Madiwani wamekula kiapo mbele ya Hakimu Mkazi Mahakama ya Geita Mhe Faraja Thomas pamoja na ahadi ya uadilifu kwa Viongozi wa Umma mbele ya Kamishina wa Maadili Bw Kweka.

Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe Jumanne Sengo Misungwi ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Ludete akizungumza na Waheshimiwa Madiwani katika Kikao cha Kwanza cha Baraza la Madiwani.Mhe Misungwi amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri kwa kupata Kura 50 kati ya 51 za Wajumnbe wote waliompigia kura ya ndio

Aidha katika Mkutano huo Mhe Jumanne Sengo Misungwi Diwani wa Kata ya Ludete  amechaguliwa kwa Kura za Ndio  5o kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ambapo kura 1 ilisema Hapana huku  Diwani wa Kata ya Nkome Mhe Sylvester Christopher Kahesi akichaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri kwa kura 51 akishindana na Diwani wa Kata ya Butundwe Mhe Charles Luzukana wa chama cha ACT Wazalendo aliyejitoa katika kura za ndio na hapana akimuunga mkono Mgombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi.

Mhe Sylvester Christopher Kahesi Diwani wa Kata ya Nkome akiwashukuru Waheshimiwa Madiwani mara baada ya kuchaguliwa kwa kura zote za ndio Katika Mkutano wa Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Geita

Mkutano huo ni wa kwanza tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu Oktoba 29,2025 ambapo Halmashauri Halmashauri ya Wilaya ya Geita ilishiriki Uchaguzi huo kwa majimbo matatu ya Uchaguzi ambayo ni Geita, Busanda na jimbo jipya la Katoro.

Tangazo

  • HIZI HAPA AJIRA ZA KUMWAGA GEITA DC July 15, 2025
  • TANGAZO LA KUKODI MAGARI August 31, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 02, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MADIWANI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WALA KIAPO RASMI KUANZA KUWATUMIKIA WANANCHI

    December 04, 2025
  • GEITA DC YAPOKEA ZANA ZA KILIMO KUTOKA WIZARA YA KILIMO

    December 01, 2025
  • KATIBU TAWALA MOROGORO DKT MUSSA AZITAKA HALMASHAURI KUUNGA JUHUDI ZA VIKUNDI VINAVYOWEZESHWA NA SERIKALI KULETA MATOKEO CHANYA.

    November 14, 2025
  • WATAALAM KUTOKA MKOA WA GEITA WAPATIWA MAFUNZO UTEKELEZAJI WA MRADI WA KUKUZA USAWA WA KIJINSIA TANZANIA(PAMOJA)

    November 13, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa