• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI MKOANI GEITA KUNUFAIKA NA MSAADA WA KISHERIA KUPITIA MAMA SAMIA LEGAL AID COMPAIGN

Posted on: January 25th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe Martine Shigela ameongoza wananchi wa Mkoa wa Geita katika Uzinduzi wa Maonesho ya Wiki ya Sheria ambayo yameanza tarehe 24-31,Januari 2025 katika viwanja vya EPZA vilivyo Geita.

Akiwa katika viwanja vya EPZA, Mhe Shigela ametembelea banda la Mahakama Kuu Kanda ya Geita,Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa( TAKUKURU), Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya jamii ( NSSF), Tume ya Usulihishi na Uamuzi(CMA), Ofisi  ya Taifa ya Mashtaka Mkoa wa Geita, Chama  cha Mawakili wa kujitegemea, Madalali na Wasambazaji Nyaraka wa Mahakama.

Mabanda Mengine yaliyotembelewa ni banda la Uhamiaji , Magereza, Zimamoto na banda la wajasiriamali.

Akizungumza katika uzinduzi huo Mhe Martine Shigela amewapongeza watendaji wa Mahakama kwa namna ambavyo wamejipanga kuifanikisha wiki ya sheria Mkoani Geita.

" Nimefarijika kuona washiriki  wote wa Maonesho wamefika ili kuwahudumia wananchi na kuhakikisha Maonesho yanafana" Amesema Mhe Shigela.

Aidha Mkuu wa Mkoa ametoa wito kwa wananchi kujitokeza katika viwanja vya EPZA ili kujifunza mambo mbalimbali ya kisheria.

" Tujitokeze kupata elimu, kupata ushauri wa kisheria  ili kupata muongozo wa mambo mbalimbali ya kisheria kwani Mahakama ni chombo cha kutoa haki" Ameongez Mhe.Shigela.

Shigela Ameongeza kuwa malalamiko yanapopungua yanajenga heshima kubwa kwa Mahakama Kuu Kanda ya Geita.

Vilevile Mhe Shigela amepongeza matumizi ya Teknolojia kwa kurahisisha mahakama kufanya kazi kisasa

" Unaweza fungua  mashauri kwenye mtandao popote pale ulipo ndani na nje ya nchi, pia nafarijika kuona utendaji na utoaji wa haki unaenda kwa wakati ndani ya mkoa  wa Geita kwani kesi zimekuwa zikimalizika kwa wakati" Amesema Mhe Shigela.

Pamoja na hayo Mhe Shigela ameishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayo ongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kutoa fedha nyingi kwa ajili ya uboreshaji wa huduma za mahakama  na kuwataka  wananchi  kuendelea kuiunga mkono mahakama kuu Kanda ya Geita.

"Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan ametia nguvu  kuunga mkono kazi za Mahakama kwa kuleta kampeni ya Msaada wa Kisheria ijulikanayo kama Mama Samia Legal Aid Compaign (MSLAC)  ambayo inaenda kusambaa katika vijiji  Mkoani Geita" Amesema Mhe Shigela.

Maonesho hayo yamebebwa na Kauli mbiu isemayo: " Tanzania ya 2025, Nafasi ya Taasisi zinazosimamia Haki Madai Katika Kufikia Malengo Makuu ya Dira ya Taifa ya Maendeleo"


Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe Martine Shigela akizungumza katika uzinduzi wa wiki ya Sheria katika viwanja vya EPZA vilivyo Bombambili Manispaa ya Geita. 


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa