• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA YATOA MIKOPO ISIYO NA RIBA YA SHILINGI MILIONI 500 KWA VIKUNDI 58

Posted on: January 5th, 2026

Halmashauri ya Wilaya ya Geita kupitia Divisheni ya Maendeleo ya Jamii imetoa mikopo isiyo na riba yenye thamani ya shilingi milioni 500 kwa vikundi 58 vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

Hafla ya utoaji wa mikopo hiyo imefanyika katika viwanja vya Halmashauri ya Wilaya ya Geita tarehe Januari 5, 2026, ambapo Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Geita, Bi Janeth Mobe, alikuwa mgeni rasmi akimuwakilisha Mhe Hashim Komba Mkuu wa Wilaya ya Geita.

Kaimu Mkuu wa Wilaya Bi Janeth Mobe akizungumza na wanavikundi waliojitokeza katika zoezi la ugawaji wa mikopo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Bw Jonas Kilave, amesema jumla ya vikundi 58 vimefanikiwa kupata mikopo hiyo baada ya kukidhi vigezo, kati ya vikundi vilivyokuwa vimewasilisha maombi ambavyo ni vikundi 94 vya wanawake, 92 vya vijana na 16 vya watu wenye ulemavu.

Ameongeza kuwa pamoja na utoaji wa mikopo, Halmashauri imeendelea kutoa mafunzo kwa wanufaika wa mikopo hiyo yakiwemo mafunzo ya utunzaji wa kumbukumbu za vikundi, usimamizi wa fedha, umuhimu wa kuweka akiba, ujasiriamali pamoja na utatuzi wa migogoro ndani ya vikundi.

Mkuu wa Divisheni ya maendeleo ya jamii Jonas Kilave akizungumza na wananchi waliojitokeza katika zoezi la ugawaji mikopo 

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi na Mazingira Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Mhe Paschal Mapung’o, amevitaka vikundi vilivyopata mikopo hiyo kuitumia fedha hizo kwa malengo yaliyokusudiwa ili kuleta tija kwa jamii na kuhakikisha marejesho yanafanyika kwa wakati.

Naye Mwakilishi wa TAKUKURU, Bw Said Lipunjaje, amesisitiza umuhimu wa kudumisha umoja ndani ya vikundi, akisema umoja huo uendelee hata baada ya kupokea mikopo ili malengo ya vikundi yafikiwe na marejesho yafanyike kwa wakati, hali itakayowawezesha wanufaika wengine kunufaika na mikopo hiyo.

Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Geita, Bi Leminatha Mbegete, amewataka wanufaika kuwa na nidhamu ya mikopo kwa kuhakikisha wanarejesha mikopo hiyo kwa wakati, akisisitiza kuwa mikopo hiyo iwe chachu ya maendeleo yao binafsi na maendeleo ya jamii kwa ujumla.

Akihitimisha hafla hiyo, Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Geita, Bi Janeth Mobe, ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa kuandaa fedha kwa ajili ya vikundi, akisisitiza kuwa mikopo hiyo si hisani bali ni mikopo inayopaswa kurejeshwa kwa wakati. Ameongeza kuwa mikopo hiyo itumike vizuri ili iweze kusaidia vikundi vingine vingi zaidi siku zijazo. Aidha amewaasa wanufaika kuwa mabalozi wazuri wa serikali kwa kuitangaza na kuonesha jitihada zake za kuwajali wananchi. Kwa upande wa waendesha bodaboda, amesisitiza umuhimu wa kuwa na leseni halali.

Kaimu Mkuu wa Wilaya Bi Janeth Mobe akikata utepe kurasmisha zoezi la utoaji mikopo kwa vikundi

Kwa upande mwingine, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Mhe Jumanne Misungwi, amesema serikali ipo pamoja na wananchi na inaendelea kuwatambua, huku akisisitiza suala la uzalendo kwa vijana. Amewataka wazazi na walezi kuwa mabalozi wazuri kwa kuwalea na kuwaelimisha vijana katika misingi ya uzalendo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Mhe Jumanne Misungwi akizungumza na wananchi waliojitokeza katika zoezi la ugawaji wa mikopo kwa  vikundi

Kwa upande wa wanufaika, Bi Furaha Yusufu mkazi wa Katoro na mwakilishi wa vikundi vya vijana, amesema mikopo hiyo itamsaidia kuendeleza biashara ya utengenezaji wa bidhaa za ngozi kama viatu na hivyo kuboresha maisha yake na kuwa mlipa kodi mzuri.

Naye Mwakilishi wa wanawake, Mama Sabina Kaitila kutoka Tarafa ya Bugando na Mwenyekiti wa Kikundi cha Kazabuti, ameishukuru serikali kwa kutoa mikopo hiyo akisema itawasaidia wanawake wengi kujiimarisha kiuchumi na kuepuka changamoto zilizokuwa zikisababishwa na mikopo isiyo rafiki.

Kwa upande wake, Bw Hamisi Masegenya, Mwenyekiti wa Kikundi cha Abhabhelu, ameishukuru serikali na kuomba siku zijazo wapewe vyombo vya moto ili waweze kuongeza kipato chao.

Mikopo hiyo ni sehemu ya asilimia kumi ya mapato ya ndani ya Halmashauri inayotengwa kwa ajili ya kukopesha vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.


Vikundi vya Wanawake, Vijana na watu wenye ulemavu wakiwa wameshika mfano wa hundi ya Sh Milioni 500 wakati wa upokeaji wa mikopo inayotolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Tangazo

  • HIZI HAPA AJIRA ZA KUMWAGA GEITA DC July 15, 2025
  • TANGAZO LA KUKODI MAGARI August 31, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 02, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA YATOA MIKOPO ISIYO NA RIBA YA SHILINGI MILIONI 500 KWA VIKUNDI 58

    January 05, 2026
  • MUUNGANO WA VIKUNDI VYA ASILIMIA KUMI VYARUDISHA KWA JAMII

    December 31, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA YAKABIDHI MADAWATI KWA SHULE ZA MSINGI.

    December 30, 2025
  • SERIKALI KUSHUGHULIKIA AFYA, ELIMU, BARABARA LWAMGASA.

    December 21, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa