• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WANAFUNZI 16 WA SHULE YA SEKONDARI LWEZERA WAJERUHIWA KWA RADI, DC NA AFISA ELIMU WAWAFARIJI

Posted on: August 11th, 2021

Mkuu wa wilaya ya Geita Mh Wilson Samwel Shimo amewatoa hofu wanafunzi wa shule ya Sekondari Lwezera, kufuatia ajali ya radi iliyotokea leo Agosti11, 2021 na kuwajeruhi wanafunzi 16 wa shule hiyo.

Ajali hiyo ya radi imetokea leo majira ya saa tano asubuhi wakati wanafunzi wakiwa wanaendelea na ratiba zao za masomo ambapo wanafunzi wanane ni wasichana na wanane wengine ni wavulana huku kati ya hao wasichana watatu na wavulana wawili wamelazwa katika Hospitali ya wilaya Nzera.

Tukio la ajali hiyo ya radi limetokea wakati ambapo Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Geita Wilson shimo akiwa kwenye kikao cha Baraza la madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Geita na kulazimika kuacha kikao hicho na kuelekea eneo la tukio.

Akiwa katika shule ya Lwezera ilipotokea ajali hiyo Mh Wilson Shimo amezungumza na uongozi wa shule na wanafunzi ambapo amewataka wanafunzi  kuwa watulivu na kuendelea na masomo kama kawaidia na kuagiza ukaguzi ufanyike kubaini vitu vinavyoweza kuvuta radi katika shule hiyo ili kujihadhari.

Aidha Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Dr. Modest Rwekaemula, amesema walipopata taarifa hizo hatua ya kwanza walipofika shuleni hapo waliwachukua wanafunzi wote waliopata madhara na kuwakimbiza katika zahanati ya Lwezera ambapo baadhi wamepewa huduma ya kwanza na wengine kulazimika kuwapeleka Hospitali ya wilaya nzera kwa ajili ya matibabu zaidi. 

Amesema kwamba wamepatiwa matibabu na hali zao zinaendelea vizuri na kuongeza kuwa wameshatoa elimu kila shule namna ya kuchukua tahadhari na kukabiliana na majanga kama hayo ikiwemo kutoa taarifa katika zahanati iliyo karibu na kutoa taarifa katika uongozi wa wilaya ili kuongeza nguvu.


Kwa upande wake Diwani wa kata ya Lwezera Mh. Misango Jeremiah Misango amewasihi wanafunzi wasiwe na hofu bali waendelee na masomo wakiamini kuwa Serikali inawatambua na kuwajali.

Hata hivyo baadhi ya majeruhi wa ajali hiyo akiwemo Anastazia Richard na Veneranda Myengi wamesema wakiwa darasani gafla ilipiga radi iliyowafanya wapoteze fahamu kwa mshtuko na baadae kujikuta wakiwa Hospitalini wakiwa na maumivu makali mwilini.


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa