• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WALIMU WASISITIZWA KUTOA TAKWIMU ZILIZO SAHIHI KATIKA SEKTA YA ELIMU-GEITA DC

Posted on: March 22nd, 2024

Na: Hendrick Msangi            

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) inajukumu la kukusanya takwimu za Elimu ya Awali, Msingi, Sekondari, Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi.

Takwimu hizo hukusanywa kila Mwaka kama zinavyokuwa tarehe 31Mwezi Machi kwa kutumia Madodoso ya Takwimu za shule/madarasa ya Elimu ya Awali (TSA), Takwimu za Shule za Msingi (TSM), Takwimu za Elimu ya Sekondari (TSS) naTakwimuza Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi (TWM).

Lengo la kukusanya takwimu hizi ni kutoa taarifa na picha ya hali halisi iliyofikiwa kutokana na viashiria mbalimbali vya kielimu katika Sekta ya Elimu msingi, Elimu ya Sekondari Kidato cha Tano na Sita na Elimu ya Watu Wazima. Viashiria hivyo huonesha ni kwa kiasi gani utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo umefanikiwa.

Ili kufikia lengo la kukusanya taarifa hizo muhimu kwa usahihi, Mwongozo huo umeandaliwa kuwezesha wanaohusika na ukusanyaji wa taarifa hizo kuelewa kwa ufasaha maswali na takwimu zinazohitajika katika kufanikisha zoezi lengwa.

Wakuu wa shule za Msingi na Maafisa Elimu kata wakiwa kwenye semina elekezi ya ukusanyaji wa Takwimu sahihi Halmashauri ya wilaya ya Geita. Zoezi hilo linatarajiwa kuhitimishwa na Afisa Elimu wa Halmashauri kwa kufanya Uhakiki na kuthibitisha (Approve) Usahihi wa takwimu katika mfumo kwa kila Shule kabla ya tarehe 8 Mei, 2024.

Katika  kutekeleza hilo, Halmashauri ya Wilaya ya Geita imefanya kikao kazi na walimu wakuu wa shule zote za msingi, maafisa elimu kata na walimu wenye dhamana ya kutunza takwimu kwenye shule za msingi ili kuendelea kuwajengea uwezo wa kutekeleza jukumu hilo muhimu kwa Taifa.

Akifungua semina hiyo elekezi, Kaimu Mkuu wa Idara ya elimu ya awali na msingi Mwl Richard Paul Magubiki alisema zoezi la takwimu linafanyika kila mwaka na lina maana kubwa sana katika shughuli zote za kiserikali kama ilivyo Sheria ya Takwimu Na.9 ya Mwaka 2015 inavyosisitiza utoaiji wa takwimu zilizo sahihi “Takwimu ndio kiini cha kila kitu hivyo kila mtu ahakikishe anatoa takwimu zilizo sahihi kwani kutokutoa takwimu zisizo sahihi kunaiingizia serikali hasara kubwa” alisema Mwl Magubiki.

Kaimu Mkuu wa Idara ya Elimu ya awali na Msingi Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mwl Magubiki akiwa na maafisa Elimu wa Halmashauri katika semina elekezi kwa wakuu wa shule ,walimu wa takwimu na maafisa elimu kata ya ujazaji wa takwimu sahihi

Akiendelea kuwapa semina elekezi walimu hao, Mwl Magubiki alisema Takwimu husaidia kubaini mahitaji muhimu katika sekta ya elimu, kujua kuna nini katika elimu ya msingi ikiwa ni pamoja na miundombinu ya thamani zilizopo,idadi ya  wananafunzi, walimu na kufahamu mapungufu katika sekta ya elimu.

Aidha Mwl Magubiki alisema zoezi hilo likifanywa kwa ukamilifu litasaidia serikali kupanga bajeti kwa kutumia takwimu zilizo sahihi na kuwataka walimu hao na watakwimu kutojifungia mashuleni bali kushirikiana kupata taarifa sahihi kwa kujipanga mapema ili zoezi hilo likamilike kwa wakati na kuleta matokeo chanya yenye uhalisia.

Wakuu wa Shule, Walimu wa Takwimu na Maafisa Elimu Kata kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Geita walipokutana katika kikao elekezi kutekeleza Sheria ya Takwimu Na.9 ya Mwaka 2015 ambayo ni miongoni mwa Sheria zilizofanyiwa urekebu (revision) Mwaka 2019 na kutangazwa na Serikali tarehe 28 Februari, 2020 (GN 140/2020). Urekebu huo katika Sheria ya Takwimu unajumuisha marekesho ya Mwaka 2018 na 2019.Kwa mantiki hiyo, kuanzia tarehe 28 Februari, 2020, Sheria ya Takwimu itanukuliwa kama “Sheria ya Takwimu, SURA 351

Halmashauri ya Wilaya ya Geita ina jumla ya shule za msingi 246 za serikali zikiwa 235 na shule binafsi 11 na walimu 3258. Zoezi la Uhakiki na kuthibitisha (Approve) Usahihi wa takwimu katika mfumo kwa kila Shule linatarajiwa kukamilika kabla ya tarehe 8 Mei, 2024.

Maafisa Elimu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Geita wakiwa kwenye kikao na  wakuu wa shule, maafisa elimu kata na walimu wa takwimu katika semina elekezi iliyofanyika shule ya msingi Nzera.


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa