• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WAFANYABIASHARA GEITA DC WAPEWA ELIMU YA URASIMISHAJI WA BIASHARA KATIKA KUCHANGIA MAPATO YA SERIKALI

Posted on: November 11th, 2024

Wananchi Wilayani Geita wanaojihusisha na biashara ndogo ndogo pamoja na wajasijiriamali wametakiwa kuhakikisha wanazikatia biashara zao leseni pamoja na kuwa na vibali halali kutoka serikalini ili kuweza kufanya biashara zao kwa uhakika na kuepukana na adha wanayoweza kukumbana nayo ya kufungiwa biashara hizo.

Akizungumza na wafanyabiashara hao wa Kata za Nkome, Nyamboge, Lwezera na Nzera  katika zoezi la uelimishaji na ukaguzi wa vibali na leseni halali za biashara, Afisa Biashara kutoka Halmashauri ya Wilaya, Geita, Bw. Dennis John Lihepa amewataka wafanyabiashara hao kuondokana na tabia ya kufanya biashara kiholela bila ya kuwa na leseni na vibali stahiki, kwani kufanya hivyo ni kuikosesha serikali mapato ambayo ni msingi wa maendeleo kwa kuchangia miradi mbalimbali katika jamii.

Afisa Biashara kutoka Halmashauri ya Wilaya, Geita, Bw. Dennis John Lihepa akiwa katika zoezi la uelimishaji na utoaji wa leseni za biashara kwa baadhi ya wafanyabiashara wenye maduka ya jumla na wasimamizi wa nyumba za kulala wageni kwenye Kata ya Nkome.

“Kama mfanyabiashara, unapaswa kuhakikisha unaikatia biashara yako leseni, pamoja na kuwa na vibali stahiki vitakavyowezesha kufanya biashara yako kwa amani na utulivu. Lakini pia unapaswa kutambua kuwa, kwa kuikatia leseni bishara yako, unakuwa umechangia katika kuleta maendeleo kwenye jamii kwani fedha inayopatikana ndiyo inayowezesha utekelezaji wa miradi mbali mbali kwenye Halmashauri.” Amesema Bw. Lihepa.

Kwa upande mwingine, baadhi ya wafanyabiashara waliotembelewa na timu hiyo, wameipongeza Serikali kwa hatua hiyo, huku wakiitaka elimu hiyo kwa mfanyabiashara kutolewa mara kwa mara ili kuwawezesha wafanyabiashara kuwa na uelewa zaidi wa masuala ya kodi.

Baadhi ya maduka katika Kata ya Nkome yaliyofikiwa na huduma ya urasimishwaji wa biashara kwa kukatiwa leseni na Maafisa Biashara kutoka Halmashauri.

“Kwa hakika hatua hii ni ya kupongezwa kwa serikali kwasababu inatuwezesha sisi kama wafanyabiashara kutambua nini tunapaswa kufanya ili kuzirasimisha biashara zetu. Tunapenda kutoa wito kwa Serikiali kuhakikisha inatoa elimu hii kwa wafanyabiashara mara kwa mara ili kuwapa uelewa wa faida za kulipa kodi na namna tunavyoweza kuchangia katika kuleta maendeleo kwenye jamii yetu.” Amesema Bi. Sophia Ngoni anaejishughulisha na biashara ya saluni.

Zoezi la utoaji elimu kwa wafanyabiashara juu ya umuhimu wa kulipia leseni za biashara ni endelevu katika kuhakikisha Halmashauri inafikia malengo yake katika ukusanyaji wa Mapato ambapo kwa mwaka wa fedha 2024/25 Halmashauri kupitia vyanzo mbalimbali vya mapato inatarajia kukusanya zaidi ya Bilioni 8.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa