• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WADAU WA ELIMU WAOMBWA KUSAIDIA HALI ZA WANAFUNZI MASHULENI ILI KUONGEZA UFAULU NA HAMASA YA UJIFUNZAJI

Posted on: June 6th, 2022

Baada ya kukutana na Wadau mbalimbali wa Elimu kuanzia ngazi za Vijiji, na Kata, Shirika la Plan International June 02, 2022 lilikutana na Wadau wa Elimu ngazi ya Halmashauri katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Nzera, kwa lengo la kujadili changamoto, maendeleo na kuweka mikakati ya kuendelea kumlinda Mtoto.

Kwa mujibu wa Ndg. Abeid Mkwawa Mratibu wa Mradi wa kutokomeza ajira kwa watoto mkoa wa Geita, Halmashauri ya Wilaya  Geita imefanikiwa katika mambo mbalimbali yanayomhusu mtoto ikiwemo huduma ya Chakula mashuleni, upatikanaji wa huduma ya maji na vyumba maalumu vya hedhi salama mashuleni, usalama wa watoto na kukomesha ajira za watoto hasa katika maeneo ya shughuli za uvuvi na uchimbaji wa madini.

Miongoni mwa mbinu zinazotajwa na Ndg. Mkwawa kutumika katika kufanikisha hali hizo ni pamoja na kuwashirikisha wadau mbalimbali kwa kuwapatia Elimu ya Haki za watoto zinazopaswa kulindwa sambamba na kuunda kamati mbalimbali kuanzia ngazi za Shule, Vijiji na Kata ambazo zimekuwa zikifuatilia na kuchukua hatua kwa kuwasaidia watoto hao ikiwemo kuwarudisha mashuleni watoto wanaojiingiza katika shughuli za uzalishaji mali.

Wadau wanaziona changamoto mbalimbali kama vile lishe duni kwa watoto, mazingira yasiyo vutivu ya kujifunzia, huduma za maji na vyumba vya hedhi salama mashuleni kuchangia kudhorotesha maendeleo ya kitaaluma na ufaulu wa watoto huku wakiweka mikakati mbalimbali ya kuendelea kuboresha hali za wanafunzi mashuleni.

Wadau wameazimia kutoa Elimu na hamasa kwa wananchi na viongozi wa ngazi mbalimbali ili wafahamu umuhimu wa chakula mashuleni na miundombinu rafiki ya Hedhi salama, suala litakalowafanya kuhamasika kuchangia maendeleo ya hali hizo ili kumsaidia mtoto kusoma katika mazingira salama na kuongeza ufaulu kwa ujumla.

Aidha wadau wameshauri pia kutumia mashamba ya shule na vipindi vya Elimu ya Kujitegemea (EK) kwa ajili ya kuzalisha chakula cha wanafunzi shuleni huku wakiwashirikisha wataalamu wa kilimo ambao watashauri kitaalamu kuhusu mazao yanayotakiwa kuzalishwa katika maeneo husika kulingana na hali za mashamba hayo.

Shirika la Kivulini linaloshirikana na PLAN limefanikiwa kuwatumia wataalamu wa huduma za Afya kufundisha jinsi ya kutengeneza Sodo kwa ajili ya wanafunzi wa kike mashuleni huku ujuzi huo ukiendelea kutolewa kwa jamii ili kuwasaidia kupunguza gharama za kununua taulo za kike ambazo wanafunzi wengine wanashindwa kugharamia.

Katika kuona unyeti wa changamoto hiyo Halmashauri ya Wilaya ya Geita ina mkakati wa kutenga chumba maalumu cha hedhi salama katika majengo ya vyoo yanayojengwa kwa sasa ili kupunguza changamoto hiyo ambapo pia wadau wanaomba kuwepo kwa madawati ya jinsia angalau katika kila kata ili kuongeza ufuatiliaji wa kesi za ukatili dhidi ya watoto.

Ufinyu wa bajeti unatajwa kutotosheleza mahitaji ya walengwa suala ambalo wadau mbalimbali kwa kushirikiana na Serikali wana wajibu wa kusaidia katika kutatua changamoto hizo ili kuepuka kumnyanyasa mtoto kwa kujua au kutokujua ingawa uwepo wa fedha za kutosha ungeweza kusaidia hata kununua vifaa ambavyo vingeweza kutumiwa na wanafunzi wenyewe kutengeneza Sodo ambazo wangezitumia wakiwa shuleni kuliko kuacha kuhudhuria masomo.

Aidha jamii pia inawajibika kuwahudumia watoto kwa kuwapatia mahitaji mbalimbali ya msingi ikiwemo huduma za Afya, Chakula na malazi na kutotimiza wajibu huo ni kumnyanyasa mtoto.  




Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa