• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

VIJANA WAASWA KUWA NA MCHANGO CHANYA KWENYE TAIFA

Posted on: October 8th, 2024

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa 2024, Ndg. Godfrey Eliakimu Mnzava amewataka vijana kuishi yale waliyoelezwa kwenye kongamano ili kuwa na mchango chanya kwenye jamii zao pamoja na kuepukana na tabia hatarishi ili waweze kuyafikia malengo yao.

Akizungumza na Vijana wa kata ya Nkome Wilayani Geita, Ndg. Godfrey Mnzava amesema kuwa vijana wanapaswa kuzinoa fikra zao ili ziwe na tija kwenye taifa pamoja na kuwa wazalendo.

"Vijana wanatakiwa watekeleze yale yaliyosemwa kwenye kongamano hili la vijana ili kuendelea kuzinoa fikra zao ziwe zenye kuleta matokeo makubwa na hivyo kuleta faida kwa jamii na taifa kwa ujumla." Amesema Ndg. Mnzava.

Vijana Wilayani Geita wametakiwa kuyafanyia kazi yale waliyoelezwa kwenye kongamano ili kuwa na mchango kwenye jamii.

Aidha, kiongozi huyo pia amewataka waratibu wa kongamano hizo kuhakikisha wanakuwa na vikao vya mara kwa mara na vijana ili kuwa na mchango kwenye jamii.

"Tuendelee kuzungumza na vijana mara kwa mara, ikiwezekana mara nne kwa mwaka tukiendelea kuwatengeneza kwa kuwa ni nguvu kazi ya taifa. Hii itasaidia hata wao kuziangalia fursa kwa mtazamo wa kipekee, lakini pia itawapa nafasi vijana kutoa maoni yao."

Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Halmashauri ya Wilaya, Geita, Bi. Mathalena Mgina, amewataka vijana kuchangamkia fursa za mikopo inyotolewa na Halmashauri ili kuweza kujikwamua kiuchumi.

"Jukumu letu sisi kama Halmashauri ni kuhakikisha tunawasaidia kujikwamua kiuchumi ili kuondokana na suala la utegemezi kwenye jamii yetu. Ili kuweza kupata mikopo ambayo inatolewa na Halmashauri, mnapaswa kuanzisha au kujiunga kwenye vikundi ili muweze kufaidika na mikopo hii." Amesema Bi. Mathalena.

Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Halmashauri ya Wilaya, Geita, Bi. Mathalena Mgina, amewataka vijana kuchangamkia fursa za mikopo inayotolewa na Halmashauri.

Mada zilizofundishwa kwa vijana ni pamoja na fursa mbalimbali za kiuchumi zinazopatikana katika Halmashauri ya Wilaya, VETA, SIDO Pamoja na Benki ya NBC huku vijana wakiitaka serikali kuendelea kupewa mikopo isiyo na riba kwa wakati, kujengewa uwezo kwenye masuala mtambuka, pamoja na kushirikishwa kwenye vyombo vya maamuzi.

Meneja Benki Ndugu Amiri Mhina kutoka Benki ya NBC Geita amewasisistiza vijana kuwa na tabia ya kujiwekea akiba kwaajili ya badae.

Elimu ya Uzalendo na Uadilifu iliwasilishwa na Ndugu Ally Ally Abdul Mkurugenzi Chuo Kikuu Huria Tanzania Geita aliyewaasa vijana kuwa wazalendo, wajiamini, Pamoja na kuwa waadilifu.

Bakari Moshi Kitoboli (Afisa Uendelezaji Biashara) kutoka SIDO Geita amewataka vijana kuwa na dhana ya kujitegemea kwa kuanzisha biashara ndogo ndogo zinazoweza kuwaingizia kipato.

Mganga Mfawidhi kutoka Zahanati ya Nkome, Dkt. Charles Kafulela amewataka vijana kutambua changamoto zinazowakabili kwenye mazingira yao na kuzigeuza kuwa fursa.


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa