• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

UZINDUZI WA KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA GEITA WANANCHI WAASWA KUJITOKEZA KWA WINGI

Posted on: January 26th, 2025

Uzinduzi wa  Kampeni  ya Kitaifa ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia umefanyika leo Januari 26,2025 Mkoani Geita.

Akimuwakilisha Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe Dotto Mashaka Biteko( MB), Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe Martine Shigela amezindua Kampeni hiyo  ambayo Wizara ya Katiba na Sheria  imekasimiwa kuratibu Kampeni hiyo.

Uzinduzi huo umefanyika katika viwanja vya Kalangalala ambapo   Taasisi mbalimbali zimehudhuria ambazo ni wakala  wa usajili ufilisi na udhamini(RITA), Tanganyika Law Society (TLS) na  Shirika la NELICO.

Mhe Shigela amesema Serikali ya awamu ya sita inayo ongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan inatambua wananchi wengi wanakosa msaada wa kisheria kwa kuwa gharama za kulipa Mawakili ni kubwa.

"Mhe  Dkt Samia Suluhu Hassan ameona  wapo watanzania ambao hawana uwezo wa kulipa Mawakili ili kupata huduma za kisheria  hivyo  Serikali inayofedha ya kuwalipa Mawakili ili wananchi wanufaike na huduma ya msaada wa kisheria" Amesema Mhe Shigela.

Aidha Mhe Shigela amesema Kampeni hiyo inaongeza wigo wa kupata elimu  na kupata huduma za kisheria ikiwa ni pamoja na kupanua utawala bora  na demokrasi na kupunguza matatizo ambayo yanahitaji msaada wa kisheria Bila kujali umri na uwezo wa wananchi.

"Tuendelee kujipanga na kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi ili  mambo yanayowakabili wananchi hasa kwenye madini, ardhi, Mirathi , ndoa,  ukatili wa kijinsia na watoto yaweze kupatiwa ufumbuzi na yale mambo yatakayobainika na kupelekwa mahakamani basi wananchi wajitokeze kwenda kutoa ushahidi. " Ameongeza Mhe Shigela.

"Mjitokeze kutoa ushahidi kwani Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan anazo fedha za kuwalipa mawakili  wote wanaosimamia hizo kesi. Tujipange kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma" Amesisitiza Mhe Shigela.

Pamoja na hayo Mhe Martine Shigela ametoa  wito kwa wananchi waliohudhuria uzinduzi huo kuwa Mabalozi kwa wengine ili waweze kujitokeza kupata huduma hiyo. Vilevile Mhe Shigela amezitaka Taasisi mbalimbali,  vyama vya siasa, Taasisi za Kidini Pamoja na vyombo vya habari kuendelea kutoa taarifa na kuhamasisha wananchi ili kujitokeza  katika kampeni hiyo.

"Niwasihi kujipanga kuhamasisha wananchi,  Viongozi wa Dini hii iwe sehemu ya Ibada kwani  wananchi wanapopata huduma mnapata thawabu" Ameongeza Mhe Shigela.

Akihitimisha hotuba yake Mkuu wa Mkoa wa Geita amesema dhamira ya Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan ni kuwahudumia Watanzania na ameendelea kuwa na ubunifu kila wakati  kuigusa mioyo  ya watu waliopoteza haki zao na kutoa wito kwa Mawakili wanaosimamia mashauri ya wananchi kuyapeleka mahakamani yale yanayotakiwa huku akiwasihi wananchi kujitokeza kutoa ushahidi wanapohitajika.

Mkoa wa Geita una jumla ya Halmashauri Sita ambazo kila Halmashauri inatarajiwa kufikiwa kwa idadi ya kata 10.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa