• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

UNESCO-NATCOM YATOA MAFUNZO KUBORESHA MIMEA-DAWA SEKTA YA TIBA ASILI.

Posted on: July 2nd, 2025

Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania (UNESCO-NATCOM) imeendesha mafunzo ya programu maalumu ya kuboresha uhifadhi kilimo na uchakataji wa Mimea-Dawa pamoja na tiba lishe kwa Wataalamu wa Tiba Asili Halmashauri ya Wilaya ya Geita, huku lengo likiwa ni kupanua wigo wa huduma ya afya kwa wananchi.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo ya Awamu ya kwanza tarehe 1, Julai na Wataalamu wa Tiba Asili kutoka Vijiji vya Nungwe na Mharamba, Mshauri wa ndani wa masuala ya Afya kutoka Hospitali ya Muhimbili, Dkt. Rogers Mwakalukwa amesema kuwa, dawa za asili zina mchango mkubwa kwenye sekta ya afya ambapo takwimu zinaonyesha kuwa zaidi ya 60% ya wananchi wanatumia dawa za asili huku zaidi ya 50% ya dawa zote zinatokana na mimea.

Aidha, Dkt. Rogers pia amesema Sera ya Taifa ya Afya, Sheria Na. 23 ya mwaka 2002 inatambua huduma za tiba asili kama mojawapo ya huduma rasmi za afya nchini, na kwamba kanuni, miongozo na taratibu pia zipo, na hivyo kuwataka wataalamu hao wahakikishe wanajisajili kupitia Mfumo wa Rufaa (Enhanced Referral System) ili waweze kutambulika rasmi pamoja na kushirikiana na Hospitali na Vituo vya Afya wilayani humo.

Kwa upande mwingine, Mtaalamu wa Mimea, Bw. Frank Mbago amesema kuwa, mchango mkubwa wa afya ya binadamu unatokana na mimea, hivyo Wataalamu wa Tiba Asili wanapaswa kuchukua hatua kuhakikisha wanaitunza na kuiendeleza mimea hiyo ili iweze kuleta manufaa kwenye jamii.

Bw. Mbago pia amewasisitiza wataalamu hao kurithisha utaalamu unaotokana na Tiba Asili kwa vizazi vijavyo ili huduma hiyo iwe endelevu na kuangalia namna bora ya kuitunza na kuitumia mimea asili kama dawa.

Naye Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya, Geita, Bi. Beatrice Munisi amesema kuwa Serikali imeanzisha utaratibu wa kuhakikisha uratibu wa huduma za Tiba Asili na Tiba Mbadala zinapatikana katika ngazi zote za Mkoa na Halmashauri ili kuwapa unafuu Wataalamu wa Tiba Asili kufanya shughuli zao.

Bi. Beatrice pia ametoa wito kwa wataalamu hao kushirikiana na watoa huduma za Tiba za Kisasa kwa lengo la kuboresha huduma za tiba asili na tiba mbadala ili kudumisha huduma zinazozingatia usalama na ufanisi wa huduma za afya wilayani humo.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI. June 05, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WATENDAJI WASIMAMIWE KUHAKIKISHA AFUA ZA LISHE ZINATEKELEZWA - MHE. KOMBA

    July 12, 2025
  • HALMASHAURI ZATAKIWA KUONGEZA UBUNIFU KWENYE UKUSANYAJI WA MAPATO.

    July 12, 2025
  • VIKUNDI 111 VYANUFAIKA NA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI HALMASHAURI YA WILAYA, GEITA

    July 11, 2025
  • MHE. KOMBA ARIDHISHWA NA MAENDELEO YA UJENZI WA OFISI YA KATA, BUGULULA.

    July 05, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa