• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

UJENZI SHULE ZA SEKONDARI HALMASHAURI WILAYA

Posted on: April 17th, 2021

Kiitikio cha salamu mpya hapa nchini Tanzania kijulikanacho kama “kazi iendelee” kimeendelea kudhihirika mkoani Geita Aprili 17, 2021 baada ya mkuu wa mkoa wa Geita mhandisi Robert Gabriel kuweka mawe ya msingi katika shule za sekondari mpya tatu za Izumacheli, Mnyala pamoja na Katoma kati ya zinazoendelea kujengwa ndani ya halmashauri ya wilaya ya Geita, jimbo la Geita ikiwa ni jimbo la sita kutembelewa katika ziara yake kuyatembelea majimbo saba ya mkoa mzima.


Katika ziara yake, mhandisi Gabriel ameeleza kufurahishwa kwake kwa hatua ya ujenzi iliyofikiwa kwenye shule hizo na kuahidi kuwa, kwaiba ya serikali atahakikisha anaendelea kuunga mkono jitihada zilizooneshwa na wananchi, wadau pamoja na halmashauri katika kuongeza miundombinu ili kuwasaidia wanafunzi ndani ya kata zao, huku akiwakumbusha wadau mbalimbali wa maendeleo ndani ya Geita kuikumbuka kata ya Izumacheli ambayo ipo ndani ya kisiwa lakini pia kuutaka uongozi kuweka jitihada kumalizia madarasa yaliyobaki na kuanza ujenzi wa mabweni pamoja na maabara.

“hii ni ziara yangu kwa mkoa mzima, nimefarijika sana kwa jinsi mnavyojituma kufanya kazi. Pongezi kwenu kampuni za African Underground Mining Services ltd, AKO Group Ltd, Eagle Brand Mining ltd, na Capital Drilling bila kumsahau mbunge Joseph Musukuma kwa kuunga mkono juhudi za serikali na wananchi katika kujiletea maendeleo, hivyo na makampuni mengine Geita muikumbuke Izumacheli na shule nyingine pia” alisema mhandisi Gabriel.


 

Akihitimisha ziara yake, mhandisi Gabriel amewataka wazazi wawahimize watoto wao kusoma ili siku moja kata zao zitoe viongozi bora wa kuliongoza taifa lakini pia kama mkakati wa kuondoa umasikini kwenye jamii huku akiwaasa viongozi kuacha alama na siyo lawama, wakileta matokeo na siyo matukio.

 

Wananchi wa kata ya Izumacheli ambacho ni kisiwa nao wakaiomba serikali kuona namna bora ya kuwasaidia upatikanaji wa maji safi na salama ukizingatia uwepo wa wanyama hatari “Mamba” kwenye mwambao wa ziwa wanalolitumia kupata maji, kuwawezesha vyombo vya usafiri majini ili iwasaidie kupunguza gharama ya vifaa vya ujenzi lakini pia ujenzi wa bweni kuepuka wanafunzi kuvuka maji kila watakapoenda shule.

 

Kwa upande wa kata ya Nkome na Katoma zilipo shule za Mnyala na Katoma sambamba, wameiomba serikali kuzisaidia umeme pamoja na maji safi na salama, suala lilitolewa ufafanuzi na wataalamu wa maji na umeme kwa kuhakikisha kuwa, umeme utayafikia maeneo hayo kuanzia mwezi Julai, 2021 na maji kupatikana kupitia mradi mkubwa wa maji utakaotekelezwa hivi karibuni.

 

Katika ziara hiyo iliyohudhuliwa na viongozi wa tarafa na kata, wa chama tawala CCM na serikali, mhandisi Gabriel aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Geita Fadhili Juma, mkurugenzi wa halmashauri, wataalam wa sekta ya elimu, afya, maji, umeme na mipango ngazi ya mkoa na wilaya ambao waliweza kutolea ufafanuzi masuala mbalimbali yaliyojitokeza kwenye ziara hiyo.




  



Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa