• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

"SERIKALI YA AWAMU YA 6 INA NIA YA DHATI YA KUWAONDOLEA KERO WANANCHI KWA KUWABORESHEA HUDUMA MBALIMBALI ZA KIJAMII" RC SHIGELA

Posted on: April 30th, 2023

Na Michael Kashinde

Katika kilele cha maadhimisho miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar Mkuu wa mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigela amewataka wananchi kuendelea kuuenzi muungano uliojengwa kwa misingi  ya undugu na kutobaguana ambao umekuwa  chachu ya maendeleo ya Taifa.

RC Shigela ameyasema hayo 28 April, 2023 akiwa katika Kijiji cha Nyakagwe kata ya Butobela Halmashauri ya Wilaya ya Geita ambapo alizindua mradi wa bweni la wanafunzi 80 wa kike katika shule ya sekondari ya Nyakagwe, mradi uliogharimu jumla kiasi cha Tshs. 157,084,142.85/=.

Katika mradi huo wa bweni la wasichana RC Shigela ameielekeza Halmashauri ya Wilaya ya Geita kupitia CSR na vyanzo vingine vya mapato kuhakikisha wanapeleka magodoro, pamoja na huduma ya umeme na maji katika shule hiyo ili wananchi wasichangishwe, huku akipongeza kazi ya ujenzi huo kusimamiwa vizuri na kwa ubora unaokubalika.

Aidha Mhe. Shigela aliendelea kwa kusema kuwa Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan ina nia ya dhati ya kuwaletea maendeleo watanzania ambapo kwa kipindi cha miaka miwili maendeleo makubwa yameonekana katika sekta zote  ambapo kwa mwaka huu pekee tayari kuna bilioni 12 zimeletwa kwa ajili ya ujenzi wa madarasa.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Cornel Magembe akiwahutubia wananchi hao wa kijiji cha Nyakagwe ametoa wito kwa wasimamizi wa miradi mbalimbali ya Serikali kuwa waadilifu na kutimiza wajibu wao ili kumuunga mkono Mhe. Dkt. Samia ambaye anahangaika kuzitafuta fedha hizo kwa lengo la kuwaletea maendeleo watanzania.

Wakati huo huo ametumia nafasi hiyo kutoa wito kwa jamii kuwalinda watoto wa kike ili kuwaepusha na vitendo vinavyoweza kuathiri maisha na elimu yao huku akisistiza kuwa Serikali haitawafumbia macho wale wenye tabia ya kuwalaghai kimapenzi wanafunzi wa kike.

Naye mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Geita Ndg. Barnabas Mapande alisema kuwa fedha ni nyingi zinazotolewa na Rais Samia na zinajenga miradi bora kabisa inayopunguza kero kwa wananchi ikiwemo kwenda shuleni na madawati huku akisistiza kuwa Chama  kitaendelea kumuunga mkono kwa kusimamia miradi hiyo kama kama inavyoleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi.

Awali akitoa taarifa ya Mradi wa Bweni la wasichana 80 katika shule ya sekondari Nyakagwe Afisa Mtendaji wa kata ya Butobela Ndg. Reuben Malume Makala alisema kuwa mradi huo uliojengwa kwa jumla ya Tshs. 157,084,142.85/=, 10% ya fedha za mradi huo ambayo ni Tshs.17,550,000.00/= imechangiwa na wananchi huku kiasi cha Tshs. 139,534,142.85 ikitolewa na mfuko wa maendeleo (TASAF).

Mradi huu unatajwa kuondoa au kupunguza utoro wa wanafunzi wa kike shuleni kutokana na changamoto za mimba za utotoni na kutembea umbali mrefu kuhudhuria masomo ambapo kukamilika kwake kunatazamiwa kuongeza hali ya ufaulu kwa watoto wa kike shuleni.

Mradi huo licha ya kuwajengea uwezo kamati ya usimamizi ya jamii hususani katika masuala ya usimamizi na manunuzi ya mradi kwa ujumla lakini pia mradi huo umetoa ajira mbalimbali za ufundi ujenzi, huduma za vifaa na chakula kutoka kwa wafanyabiashara mbalimbali hali iliyoongeza mzunguko wa fedha kwenye jamii.

Kupitia mradi huo Serikali ya kijiji cha Nyakagwe imetoa shukrani za dhati kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa awamu ya Sita pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa kuboresha miundombinu ya kutolea elimu katika shule ya sekondari Nyakagwe hali itakayoongeza ufaulu wa wanafunzi na kuondoa utoro shuleni hususan kwa watoto wa kike.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa