• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

RC SHIGELA ATOA RAI KWA JAMII KUITUMIA SIKU YA UKIMWI DUNIANI KUTAFAKARI NAMNA YA KUPAMBANA NAO

Posted on: December 1st, 2022

Na. Michael Kashinde

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigela akiwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani Disemba 1, 2022 amewataka wananchi kuitumia siku hiyo kutafakari namna ya kupambana na Ugonjwa wa UKIMWI kwa kuwa ni moja ya ugonjwa hatari duniani ambao hauna chanjo wala dawa ya kuutibu.

Akiwa katika viwanja vya Kakubilo katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita  yalipofanyikia maadhimisho hayo Kimkoa, RC Shigela amesisitiza kuwa ni lazima kila mmoja aweze kujikinga na ugonjwa wa UKIMWI ambapo pia ametumia nafasi hiyo kueleza madhumuni ya siku ya UKIMWI duniani kuwa ni kukumbushana UKIMWI bado upo, na ni fursa pia ya kuwakutanisha wadau na Serikali kueleza mipango iliyopo ya kuhakikisha ugonjwa wa UKIMWI unatokomezwa.

Aidha RC Shigela ametumia nafasi hiyo kuwahamasisha wananchi kujitokeza kupata Elimu ya ugonjwa wa UKIMWI na kipima ili kujua Afya zao, sambamba na kuanza kutumia dawa mara tu mtu anapogundulika kuwa na maambukizi  huku akiongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imeboresha huduma hizo kwa kutoa vipimo na dawa bure kwa kuwa ni Serikali inayojali Afya za watanzania.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Wilson Shimo akizungumza katika maadhimisho hayo ameendelea kuwakumbusha wananchi kuchukua tahadhari zote za kujinga na virusi vya UKIMWI kwa kuwa taarifa zinaonyesha UKIMWI bado upo, huku akiwataka wananchi hao pia kujitokeza kwa wingi katika zoezi la Chanjo ya Polio linaloendelea kuanzia leo hadi Disemba 4 likiwalenga Zaidi watoto wa umri wa chini ya miaka mitano.

Awali Akizungumzia hali ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI katika Mkoa wa Geita Dkt. Yohane Kihaga Kaimu Mratibu wa kupambana na Virusi vya UKIMWI mkoa wa Geita amesema kuwa matokeo ya tafiti ya mwaka 2016 na 2017 yanaonyesha kuwa wastani wa maabukizi katika Mkoa wa Geita ni 5% ambapo hali ya sasa ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI nchini inaonyesha kuwa 40% ya maambukizi yote ni vijana ambapo 80% ya vijana hao ni wa kike.

Kwa upande wa hali ya jumla ya kijinsia na kiumri inaonyesha kuwa kuna maambukizi makubwa kwa wanawake kuliko wanaume ambapo pia afua mbalimbali zimeendelea kuchukuliwa ili kudhibiti maambukizi ikiwa ni pamoja na kutoa Elimu kwa jamii ya kujinga na virusi vya UKIMWI, kuepuka mila potofu dhidi ya ugonjwa huo na kuhamasisha jamii kutumia dawa za kufubaza makali ya virusi vya UKIMWI ingawa wanaume wanatajwa kuwa na mwitikio mdogo zaidi wa kupima ili kujua Afya zao ikilinganisha na wanawake.

Naye Bi. Patricia Nsinde Mratibu wa UKIMWI katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita amesema kuwa katika Afua ya Huduma na matunzo kwa mwaka huu Halmashauri ya Wilaya ya Geita imetumia kiasi cha milioni 22 na laki 2 kutoka mapato ya ndani kwa ajili ya kulipia BIMA ya Afya iliyoboreshwa kwa Kaya 740.

Aidha katika kutekeleza Afua hiyo ya huduma na matunzo Halmashauri ya Wilaya ya Geita Disemba Mosi, 2022 imetoa msaada wenye thamani ya shilingi Milioni 4 Laki 4 na elfu 20 kwa ajili ya kuhudumia watoto 66 waliobainishwa kuwa wanalelewa katika mazingira magumu ambapo kila mmoja amepatiwa mashuka manne, kilo sita za chakula, miche 6 ya sabuni, na ndoo kwa ajili ya kutumia kutunzia maji ya kunywa kwenye kaya ambapo Mgeni Rasmi RC Shigela amekabidhi misaada hiyo.

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI duniani mwaka huu yameambatana na kauli mbiu isemayo “Imarisha Usawa” ambapo huduma mbalimbali na elimu imekuwa ikitolewa katika mabanda maalumu yaliyoanza kuhudumia wananchi tangu Novemba 28, 2022 ambapo hii leo Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigela alipata nafasi ya kutembelea mabanda hayo na kusikia kutoka kwa wataalamu huduma zinazotolewa.


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa