• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

RC SENYAMULE AWATAKA WATUMISHI KUFUATA MAADILI YA KAZI ZAO ILI KUEPUKA MISUGUANO NA WAAJIRI WAO SEHEMU ZA KAZI

Posted on: May 1st, 2022

RC Senyamule ametoa wito huo wakati akihutubia wafanyakazi na wananchi waliojitokeza katika maadhimisho ya sikukuu ya wafanyakazi Duniani Meimosi, 2022  yaliyofanyika Kimkoa katika viwanja vya Kalangalala mjini Geita Mhe. Senyamule akiwa mgeni rasmi.

Akijibu risala ya Wafanyakazi iliyogusia changamoto mbalimbali zinazowakabili Mhe. Senyamule amesema kuwa changamoto zinaihusu Serikali zimesikilizwa na zitafanyiwa kazi kwa kuwa Serikali ni  sikivu na inaheshimu Misingi ya Utawala bora.

Aidha ametoa wito kwa waajiri wote katika Mkoa wa Geita kuzingatia Sheria, miongozo, na taratibu za utumishi wa Umma pale wanaposhughulikia masuala ya kinidhamu kwa watumishi ili kuepuka udhalilishaji kwa watumishi sanjari na kuwakumbusha watumishi kuzingatia maadili ya kazi zao.

RC Senyamule ametumia pia fursa hiyo kukemea tabia ya baadhi ya watu kuwatumikisha watoto kwa kuwafanyisha kazi za nguvu zenye ujira mdogo na usiokidhi haja zao huku akisema vitendo hivyo ni kinyume cha sheria na kutoa wito kwa makundi mbalimbali vikiwemo vyombo vya dola kupinga suala hilo kwa kuwa haki ya mtoto ni kupewa Elimu pekee.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Wilson Shimo amewataka watumishi kuunga mkono juhudi za Mtumishi namba moja nchini Rais Samia Suluhu Hassan kwa kufanya kazi kwa bidii na kutimiza wajibu wao wa kuwatumikia wananchi.

Aidha Mhe. Shimo amesisitiza kuwa mafao na maslahi ya watumishi yanajengwa na wajibu wao ambao wanautimiza kila siku, huku akiwakumbusha kuzingatia uchapakazi, uadilifu, na weledi ili malengo yao ya kupata maslahi zaidi yawezekane kwa urahisi.

Naye Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg. John Wanga amesema kuwa Kauli mbiu ya ''Mishahara na maslahi bora kwa wafanyakazi ndiyo kilio chetu kazi iendelee'' kwa Watumishi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa haiwafanyi wakapoteza lengo lao kuu la kuwatumikia watanzania katika sehemu zao za kazi huku akiwapongeza kwa kuupiga mwingi katika kutekeleza majukumu yao.

Mkurugenzi Wanga ameendelea kusema kuwa Sikukuu ya Meimosi inawakumbusha watumishi duniani kote kutafakari majukumu yao katika nafasi zao mbalimbali, huku akitoa wito wa kumuunga mkono Mhe. Rais katika kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya 2020/2025 iliyolenga kuwaletea huduma bora Wananchi.

Awali akisoma risala kwa mgeni rasmi Katibu wa TALGWU Ndg. David Mhagama amesema kuwa watumishi wanakabiliwa na changamoto mbalimbali kama maslahi duni, kuchelewa kwa mafao ya watumishi, na kutokukaa kwa mabaraza ya wafanyakazi huku Serikali ikishauriwa kudhibiti mfumuko wa bei ili kupunguza gharama za maisha kwa watumishi na wananchi kwa ujumla.

Maadhimisho ya siku ya Wafanyakazi duniani katika Mkoa wa Geita yamepambwa na burudani na michezo kutoka vikundi mbalimbali  ndani ya mkoa wa Geita huku Mgeni rasmi akikabidhi zawadi kwa wafanyakazi bora wa Umma, taasisi na mashirika mbalimbali.






Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa