• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

Naibu waziri wa Elimu Sayansi na Technolojia aahidi kuharakisha ujenzi wa VETA

Posted on: August 2nd, 2019


Naibu waziri wa elimu Sayansi na Tecnolojia William Olenasha ameahidi kupitia Wizara yake kuhakikisha wanatilia mkazo utekelezaji wa haraka wa ujenzi wa chuo cha ufundi VETA, ambao unatakiwa kuendelea katika kata ya Bombambili mkoani Geita.

Olenasha amesema ujenzi wa chuo hicho ulipata changamoto ya mkandarasi ambaye aligundulika amedanganya vielelezo na kujitengenezea uwezo ambao hakua nao, hivyo wakaamua kusitisha mkataba wake.

Aidha Naibu Waziri ameahidi kwenda kuyajadili maombi makuu mawili yaliyowasilishwa na kaimu mkuu wa wilaya ya Geita Thomas Dimme,ambayo ni gari la uthibiti ubora wa shule ili kurahisisha shughuli za ukaguzi pamoja na kuajili baadhi ya watumishi wa idara hiyo, pia ombi la kuajili walimu wa sayansi kwa shule za sekondari na walimu wengine katika idara ya elimu msingi.

Katika hatua nyingine Naibu waziri amepongeza idara ya uthibiti ubora wa shule Halmashauri ya Wilaya ya Geita pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Ali Kidwaka kwa juhudi walizozifanya katika ukamilishaji wa haraka wa jengo la uthibiti ubora ambalo limeshaezekwa,kwasasa lipo katika hatua ya upigaji ripu na uwekaji wa mfumo wa umeme.

Mthibiti mkuu ubora wa shule Wilaya ya Geita Dismas Manyonyi amesema ujenzi wa jengo hilo ulianza tarehe 03/06/2019 na hadi kufikia tarehe 31/07/2019 fundi alikuwa amekamilisha hatua ya kupaua jengo, kazi ya upigaji lipu na dari vilikuwa vinaendelea.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ali Kidwaka amesema ushirikiano baina yake, wathibiti ubora wa shule pamoja na wataalam mbalimbali wa Halmashauri ndio uliosababisha jengo hilo kukamilika kwa haraka.

Mradi huo wa ujenzi wa ofisi za mthibiti ubora kwa kanda ya ziwa unajumuisha ofisi 15 ambapo mkoa wa Geita umepata ofisi 5, ambazo zinajengwa katika Halmashauri ya Mji na Wilaya Geita, Nyang’wale, Mbogwe pamoja na Chato.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa