• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MWENYEKITI WA BARAZA LA MADIWANI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA ASISITIZA UWAJIBIKAJI KATIKA UKUSANYAJI WA MAPATO

Posted on: May 10th, 2024

Na: Hendrick Msangi

MKUTANO wa kawaida wa baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Geita, May 9, 2024 umeendelea kwa uwasilishaji wa taarifa za utekelezaji wa Shughuli za Serikali ngazi ya Halmashauri kwa kipindi cha Januari hadi Machi.

Katika Kikao hicho kamati za kudumu za Halmashauri zimewasilisha taarifa zake kwa kipindi cha Januari hadi Machi ikiwa ni pamoja na kujibu maswali kutoka kwa wajumbe wa baraza hilo kwa mujibu wa kanuni ya 22 ya kanuni za kudumu za Halmashauri.


Kamati zilizo wasilisha taarifa za utekelezaji wa Shughuli za Serikali ni pamoja na Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango, Kamati ya Uchumi, Ujenzi na mazingira, Kamati ya Elimu, Afya na Maji, na Kamati ya Maadili.

Madiwani hao wameonyesha kukereka na swala la CSR kwa namna utekelezaji wake unavyoendelea .Wakizungumzia miradi inayotekelezwa na Mgodi wa dhahabu wa Geita (GGML) madiwani hao wamesema swala la CSR limekuwa ugonjwa unaowatafuna katika kata zao na kuazimia kuwa na baraza maalumu kwa ajili ya kujadili miradi ya CSR ambayo imekuwa viporo kwa muda mrefu.

Aidha madiwani hao  wametaka miradi inayotekelezwa na nguvu za wananchi kupewa kipaumbele ili kukamilika kwa wakati na kwa ubora huku wakitoa agizo uwepo wa wahusika wa miradi kutoka mgodi wa dhahabu wa GGML kushiriki vikao vyote ikiwepo baraza ili kutoa majibu kwa waheshimiwa madiwani juu ya miradi wanayoitekeleza.

Kwa upande wake Katibu Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Geita,Gabriel Nyasilu amelipongeza baraza la madiwani kwa namna walivyo endesha kikao cha baraza hilo na ushirikiano walio nao katika kufanya kazi kuleta matokeo mazuri katika kufikia malengo ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi.

Aidha Cde Gabriel amepongeza maamuzi yaliyofanywa na baraza hilo kwa kutokuuza mitambo ambayo haijafanya kazi muda mrefu kutokana na ubovu. “Tumeridhishwa na maamuzi yenu ya kutokutaka kuuza mitambo, fanyeni jitihada ili itengenezwe iweze kusaidia changamoto za barabara katika kata.” Amesema Cde Gabriel.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Dkt Alphonce Bagambabyaki amesema Halmashauri itatekeleza yale yote yaliyoazimiwa na baraza hilo ikiwa ni pamoja na kusimamia ukusanyaji wa mapato ikiwa ni pamoja na kuendelea kuweka vizuizi  katika maeneo mbalimbali ili  kudhibiti utorashaji wa mazao hasa nyakati za usiku.

"Tutakuwa na Baraza Maalumu kwa ajili ya kujadili Miradi ya CSR ambayo imekuwa viporo Kwa muda mrefu, kwani suala la CSR limekuwa ugonjwa unaotutafuna" Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Akifunga Kikao cha Baraza hilo la robo ya tatu, Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe Charles Kazungu ametoa rai kwa watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita kuendelea kufanya kazi kwa kujituma huku wakiyatimiza yale yote ambayo baraza limeazimia katika kutimiza wajibu wao.

"Watumishi Ongezeni bidii katika ukusanyaji wa mapato ili Halmashauri iweze kufanya shughulizi zake" Mhe Charles Kazungu 

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Aidha Mhe Kazungu, amewasisitiza watumishi kuendelea kuweka bidii katika ukusanyaji wa mapato kwa kuongeza kasi katika ukusanyaji wa mapato na kutoa agizo kwa watendaji wote ambao hawafanyi vizuri katika ukusanyaji wa mapato kunyang’anywa mashine za kukusanyia ushuru(Pos) na kuwapa watu wengeine ambao watakusanya kwa bidii kwani wapo watendaji ambao wanachelewesha kwa makusudi kubenki fedha za mapato.

 “ Mimi ni Muumini wa mapato hivyo mapato yakusanywe ili Halmashauri iweze kujiendesha na tukasimamie shughuli za maendeleo katika kata zetu ili fedha zinatolewa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zilete matokeo na pia mkumbuke kusoma mapato na matumizi katika maeneo  yenu ” alisema Mhe Kazungu

Mhe Kazungu amewashukuru waheshimiwa madiwani kwa michango yao katika baraza hilo na kuendesha baraza kwa muda mfupi huku akiwapongeza wakuu wa idara na vitengo wa Halmashauri  kwa namna walivyotoa ushirikiano katika  kufanikisha baraza hilo.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa