• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MSIMAMIZI WA UCHAGUZI AKAGUA VITUO VYA KUANDIKISHA WAPIGA KURA

Posted on: October 11th, 2024

Msimamizi wa uchaguzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Ndg. Karia Magaro, ametembelea vituo vya kuandikisha wapiga kura katika kata za Nkome, Lwenzera, na Nzera, ndani ya halmashauri hiyo. Ziara hiyo ilikuwa na lengo la kukagua maendeleo ya zoezi hilo muhimu.

Akiwa katika kata ya Nzera, Magaro alijisajili katika daftari la wapiga kura kama sehemu ya kutekeleza haki yake ya kikatiba. Katika ziara hiyo, alisisitiza umuhimu wa wananchi kuhamasishana na kujitokeza kwa wingi ili waweze kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Oktoba 27, 2024.

Msimamizi wa Uchaguzi ngazi ya Halmashauri Ndg. Karia Magaro (kushoto) akionesha alama ya kidole baada ya kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura katika Kata ya Nzera.

Magaro aliwakumbusha wananchi kutofautisha kati ya kujiandikisha kuwa mpiga kura kwa ajili ya serikali za mitaa na kuhuisha taarifa katika daftari la kudumu la wapiga kura, ambalo litatumika katika uchaguzi wa serikali kuu wa mwaka 2025.

Wananchi wasichanganye kujiandikisha katika daftari la wapiga kura na zoezi lililotangulia la kuboresha taarifa za mpiga kura katika daftari la kudumu la mpiga kura, zoezi hili la sasa ni maalumu kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za mitaa hivyo kila mwananchi bila kujali alijiandikisha katika daftari la kudumu la mpiga kura au hakujiandikisha anahaki na wajibu wa kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura katika kitongoji chake ili aweze kuchagua viongozi wa ngazi ya kijiji ifikapo Novemba 27,2024, Alisema Magaro.

Msimamizi wa uchaguzi ngazi ya Halmashauri Ndg. Karia Magaro (katikati) akiwaelezea jambo waandikishaji pamoja na mawakala wa vyama vya siasa alipotembelea kituo cha uandikishaji wapiga kura katika kata ya Nzera


Kwa siku ya kwanza ya zoezi hilo, zaidi ya watu 500 walijiandikisha katika kata za Nkome, Nzera, na Lwenzera. Idadi ya waliojiandikisha inatarajiwa kufika zaidi ya elfu tano kabla ya kukamilika kwa zoezi hilo.

Msimamizi wa Uchaguzi Ndg Karia Magaro (wa kwanza kulia) akichukua taarifa za wananchi waliojitokeza kujiandikisha katika orodha ya mpiga kura katika kata ya Katoro, wengine pichani ni mwandikishaji wapiga kura pamoja na mawakala wa vyama vya siasa

Uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika Oktoba 27, 2024, unafanyika chini ya kauli mbiu inayosema, "Serikali za Mitaa ni Sauti ya Watu; Jitokeze Kushiriki Uchaguzi."

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa