• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MKUU WA MKOA WA GEITA MARTINE SHIGELA AKABIDHI ZAWADI KWA KAYA MASIKINI KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU UKIMWI DUNIANI.

Posted on: December 2nd, 2023

Na Hendrick Msangi.

MKUU wa Mkoa wa Geita, Mhe Martine Shigela, Desemba mosi amekabidhi zawadi kwa watoto wanaoishi kaya masikini na zile ambazo zimeathiriwa na maambukizi ya virusi vya UKIMWI.

Zawadi hizo zilizotolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Geita ni pamoja na Sukari kilo 150, Mashuka pisi 150, sabuni za miche 300, daftari boksi 10 na kalamu boksi 4 ambazo zitagawanywa kwa uwiano sawa kwa kila tarafa katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita ikiwa ni sehemu ya kuonyesha kuwajali na kuwathamini watoto wanaoshi katika kaya hizo.

Baadhi ya zawadi zilizokabidhiwaa na Mhe Mkuu wa Mkoa wa Geita Martine Shigela kwa ajili ya kupelekwa kwa Kaya Masikini ambazo zimekumbwa na janga la Ukimwi Katika Halmashauri ya wilaya ya Geita.

Katika Maadhimisho hayo yaliyokuwa na kauli mbiu “Jamii iongoze kutokomeza Ukimwi” ambayo Mkuu huyo wa mkoa alikuwa mgeni rasmi, alisema Mkoa wa Geita ni Mkoa wenye muingiliano mkubwa wa watu kutoka sehemu mbalimbali kutokana na fursa zinazopatikana mkoani humo ikiwemo ya upatikanaji wa madini ya dhahabu, ziwa viktoria, kuingiliana na nchi jirani hivyo aliwaasa wananchi kutumia maadhimisho hayo kukumbushana walipo toka, walipo na wanapoelekea katika kujikinga na janga la Ukimwi.

Aidha alizishukuru  taasisi na wadau mbalimbali yakiwepo mashirika kama MDH, Icap, hospitali  Pamoja na viongozi wa dini  kwa kuendelea kukumbusha jamii dhidi ya janga la ukimwi na kuitaka jamii kuendelea kuchukua tahadhari ikiwa ni pamoja na  kupima na kujitambua ili kuweza kuweka mikakati ya namna ambavyo jamii itakabiliana na ugonjwa huo wa upungufu wa kinga mwilini.

“Tuyatumie maadhimisho ya siku ya ukimwi kupeana elimu kuwa ugonjwa upo, bado una ambukiza na bado unaua na hivyo ni vema wananchi tukatumia nafasi hii kujifunza na kuweka tafakuri itakayotusaidia dhidi ya kujikinga”, alisema Mkuu wa Mkoa.

Hata hivyo aliwaasa wananchi kutokuupa nafasi Unyanyapaa kwa wagonjwa wenye upungufu wa kinga mwilini kwani haukubaliki na kusema mapambano dhidi ya ukimwi ni kwa jamii yote kwa kuhakikisha wale ambao wameambukizwa wanapewa kila aina ya nasaha, kuwasaidia kifikra, kimawazo ili waeze kuishi miaka mingi zaidi na wasikate tamaa.

Kwa takwimu za mwaka 2022 kiwango cha mambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI kwa mkoa wa Geita kilikuwa ni asilimia 5.1 na kwa mwaka 2023 takwimu zinaonyesha  kiwango cha maambukizi ni asilimia 4.7  hii ikiwa na maana maambukizi bado yapo hivyo ni vema kujipanga kwa kuweka mikakati ya kuweza kuondokana na janga hilo la upungufu wa kinga mwilini. 

Serikali imejiwekea malengo ifikapo mwaka 2030, asilimia 95 ya wenye maambukizi wafahamike kwa nchi nzima na kwa mkoa wa Geita asilimia 89 ya wananchi wawe wamezifahamu afya zao huku akiwashukuru wote ambao wamejitokeza kwa ajili ya kupima afya zao, kwani serikali imejiwekea malengo ya kupunga maambukizia mapya.  Alisema Mhe Shigela.

Pamoja na hayo Mhe Mkuu wa Mkoa aliwasihii watoa huduma za afya kuendelea kuwapenda wagonjwa na kuwajali kwani ndio kimbilio lao, Viongozi wa dini kuendelea kuwakumbusha waumini kila mara wanapokwenda kwenye misikiti na makanisani  mapambano dhidi ya ukimwi ili kuepuka maambukizi mapya, wanasiasa kupitia mikutano yao ya hadhara na ya ndani kuendelea kuwakumbusha wananchi ikiwa ni pamoja na kuifanya kuwa ajenda ya kudumu , walimu mashuleni wanapofundisha waendelee kuwakumbusha wanafunzi dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi.

Mkuu huyo wa Mkoa alitoa shukrani zake kwa Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kujiwekea malengo ya kuhakikisha wale wote waliopata maambukizi wanapata madawa, kuendelea kuboresha sekta ya afya  hususani kwenye madawa, vifaa tiba, kuongeza waganga na wauguzi ikiwa  ni sehemu ya kuondokana na changamoto za tiba na afya  katika Taifa letu. 

Mwisho aliwasihi wananchi wa Mkoa huo kuendeleaa kumuombea Rais kuwa na afya njema na maisha marefu kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya kwa ajili ya maisha ya Watanzania.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI. June 05, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MHE. WASIRA: AJENDA YA SERIKALI NI KUSIMAMIA MAENDELEO YA WANANCHI.

    June 18, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA YAPATA HATI SAFI, MHE. FATMA APONGEZA USIMAMIZI WA FEDHA ZA UMMA.

    June 13, 2025
  • UFUATILIAJI WAHIMIZWA KWENYE USIMAMIZI WA MIRADI WILAYA YA GEITA

    June 12, 2025
  • MKURUGENZI ASISITIZA HATUA KUCHUKULIWA KUDHIBITI UTORO SHULENI.

    June 05, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa