• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MKURUGENZI GEITA DC AWATAKA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI KUZINGATIA KANUNI ZA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

Posted on: November 24th, 2024

Wasimamizi wa vituo na Makarani waongozaji kutoka Jimbo la Geita na Busanda wamepewa mafunzo katika kuwajengea uwezo kuelekea  Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 27, 2024.

Mafunzo hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Bomani Geita kwa wasimamizi wa Jimbo la Geita huku Jimbo la Busanda wakipewa mafunzo  katika ukumbi wa shule ya Sekondari Butundwe ambapo wasimamizi na makarani hao wamepewa mafunzo namna ya kusimamia zoezi zima la uchaguzi ili wawapo katika vituo waweze kusimamia na kuzingatia kanuni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg Karia Magaro akizungumza na Wasimamizi wasaidizi na Makarani katika Ukumbi wa Mikutano Bomani-Geita ambapo amewataka kuwa waadilifu katika zoezi la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Novemba 27.

Akizungumza katika mafunzo hayo Msimamizi  Msaidizi Ndg Juma Chota amewasihi Makarani na wasimamizi wasaidizi hao kuzingatia taratibu na kanuni zote kwa mujibu wa muongozo wa uchaguzi wa viongozi wa ngazi za vijiji na vitongoji.

Pamoja na mafunzo hayo, wasimamizi wasaidizi na makarani hao wameelekezwa taratibu zote za upigaji kura, sifa za wapiga kura na vifaa vitakavyotumika katika zoezi zima la upigaji kura.

Akifunga mafunzo hayo Msimamizi wa Uchaguzi ngazi ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg Karia Rajabu Magaro amewataka wasimamizi wasaidizi na makarani hao kupitia mafunzo waliyopewa kufuata kanuni na taratibu za muongozo wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ili zoezi la Uchaguzi liweze kwenda vizuri.

Wasimamizi wasaidizi na Makarani waandikishaji wakiwa kwenye mafunzo katika Ukumbi wa shule ya Sekondari Butundwe ambapo wameaswa  kusimamia kwa uadilifu zoezi zima la uchaguzi ili wananchi waweze kushiriki vema zoezi hilo na wasiwe sehemu ya changamoto katika uchaguzi huo

“Tusiwe wabinafsi kama jambo hulielewi uliza kwa viongozi wako ili mzingatie kanuni zilizowekwa na kuwa makini kuepuka kushurutishwa na mtu yeyote wakati wa zoezi zima la Uchaguzi” amesema Magaro.

Aidha Magaro amewataka wasimamizi wasaidizi na makarani hao kulinda dhamana walizopewa kwa kuaminiwa katika zoezi zima la Uchaguzi.”Tuzingatie kuwahi mapema kwenye vituo ili kuhakikisha maandalizi yote yapo vizuri ili saa mbili Wananchi waanze kupiga kura hadi saa kumi jioni ili kama Halmashauri zoezi liweze kwenda vizuri” ameongeza Magaro.

Wasimamizi wasaidizi na Makarani waandikishaji wakiwa kwenye mafunzo katika Ukumbi wa shule ya Sekondari Butundwe ambapo wamekula kiapo cha utii, uadilifu na uaminifu mbele ya Mkurugenzi Mtendaji Ndg Karia Magaro Novemba 23, 2024

Pamoja na mafunzo hayo wasimamizi wasaidizi na makarani hao wamekula kiapo cha utii, uadilifu na uaminifu mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Mahakama ya Wilaya Geita Mhe Devotha Kasebele.

Halmashauri ya Wilaya ya Geita ina majimbo mawili ya Uchaguzi yenye Kata 37, Vijiji 145 na Vitongoji 593 ambapo jumla ya  vyama 7 vya Siasa ambavyo ni Chama cha Mapinduzi (CCM), Chama Cha Demokrasia na Maendelo(CHADEMA), ACT WAZALENDO, CCK, TLP na ADC vitashiriki Uchaguzi huo Novemba 27, 2024.

Wasimamizi wasaidizi na Makarani waandikishaji wakiwa kwenye mafunzo katika Ukumbi wa Halmashauri Bomani-Geita ambapo wamekula kiapo cha utii, uadilifu na uaminifu mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Mahakama ya Wilaya Geita Mhe Devotha Kasebele. Novemba 22, 2024


Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI. June 05, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA URATIBU WA MWENGE WA UHURU MKOA YATEMBELEA YATEMBELEA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA, GEITA.

    June 24, 2025
  • ZAIDI YA BILIONI 50 ZATUMIKA KUKAMILISHA MIRADI GEITA 2020-2025.

    June 21, 2025
  • RAISI DKT. SAMIA AZINDUA DARAJA LA KIGOGO-BUSISI.

    June 19, 2025
  • WATUMISHI WILAYANI GEITA WAKUMBUSHWA SUALA LA KUJIFANYIA TATHMINI.

    June 18, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa