• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MIRADI YA SHULE YAENDELEA KUTEKELEZWA GEITA DC.

Posted on: November 15th, 2023

Na Hendrick Msangi.

Halmashauri ya Wilaya ya Geita inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali katika Kata za Halmashauri hiyo kwa fedha zinazotolewa kutoka Serikali Kuu kupitia SEQUIP.

Shule ya sekondari ya Samia iliyopo kata ya Katoro ni moja ya shule ambayo inajengwa kwa fedha za SEQUIP na kwa sasa shule hiyo imekamilisha mradi wa jengo la mtumishi (2 in 1) kwa gharama ya shilingi milioni mia moja.

Nyumba ya Watumishi iloyojengwa kwa fedha za SEQUIP kiasi cha shilingi milioni mia moja. Nyumba hiyo ipo kwenye hatua za ukamilishwaji.


Nyumba hiyo yenye ubora imefikia hatua za mwisho ambapo walimu wataweza kuingia na kupunguza gharama na umbali wa sehemu wanazoishi.

Shule hiyo yenye jumla ya madarasa nane ambayo yamekamilika ina jumla ya wanafunzi 321 wa kidato cha kwanza na walimu 15, na kwa sasa serikali imeelekeza fedha kwa ajili ya ukamilishwaji wa majengo ya maabara 3, maktaba 1 na jengo moja la Tehama.

Ujenzi wa Majengo ya Maabara na Maktaba shule ya Sekondari Samia unaendelea. Kwa sasa Shule ya Sekondari Samia ina wanafunzi wa kidato cha kwanza 321

Mradi mwingine wa shule ambao upo kwenye hatua za ukamilishwaji ni shule ya sekondari iliyopo kata ya Ludete ambayo ina jumla ya madarasa 8, jengo la utawala 1, Tehama 1 maktaba 1 na maabara tatu za masomo ya sayansi na matundu 8 ya vyoo wenye gharama ya kiasi cha shilingi 584,280,029 ambapo mwezi januari unatarajia kupokea wanafunzi wasiopungua 300 wa kidato cha kwanza.

Majengo ya Madarasa ya Sekondari kata ya Ludete Wilayani Geita yakiwa katika hatua za ukamilishwaji ambapo Mwezi Januari 2024, shule hiyo itapokea wanafunzi wa kidato cha kwanza wasiopungua 300.

Pamoja na hayo wataalam mbalimbali kutoka Halmashauri hiyo wakiongozwa na Mkurugenzi wake ndugu Karia Rajabu Magaro  wamekuwa wakitembelea  mara kwa mara miradi hiyo na  kutoa maelekezo kwa wakandarasi wanaotekeleza miradi hiyo pamoja na wasimamizi wa shule hizo kuendelea kufanya kazi kwa uadilifu na kwa ubora ili miradi hiyo ikamilike kwa wakati na kuweza kuhudumia jamii kwa kuhakikisha mafundi wa kutosha wanakuwa kwenye miradi, ulipwaji wa fedha kwa wazabuni na wakandarasi kwa wakati ili kusiwepo na sababu za kuchelewesha miradi hiyo kwani tayari fedha zimeshaelekezwa kwenye miradi hiyo.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndugu Karia Rajabu Magaro akikagua Ujenzi wa shule ya Sekondari iliyopo kata ya Ludete inayojengwa na fedha za SEQUIP kiasi cha shilingi 584,280,029

Halmashauri ya wilaya ya Geita inaendelea kuishukuru Serikali inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Saluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kutenga fedha nyingi kwa ajili ya miradi inayotekelezwa katika Halmashauri hiyo.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa