• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MHE. KOMBA ATOA WITO WA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUPAMBANA NA UZUSHI, AWASIKILIZA WANANCHI NYAMBOGE

Posted on: September 25th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mhe. Hashim Komba, amewataka wananchi wa kata ya Nyamboge kushirikiana na serikali kupambana na maneno ya uzushi yanayosambaa katika maeneo mbalimbali. Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Nyamboge, Mhe. Komba alitoa tahadhari juu ya taarifa zisizo na ukweli zinazodai kuwa kuna watu wanang'olewa figo.

“Kuna maneno ya uzushi yanayosema watu wanang'olewa figo, lakini baada ya uchunguzi niliofanya kwa polisi na wananchi, hakuna tukio lolote kama hilo lililoripotiwa. Ni muhimu tuelewe kuwa uzushi huu unaweza kusababisha taharuki na kuleta madhara kwa jamii,” alisema Mhe. Komba.

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Abdallah Komba akizungumza na wananchi wa kata ya Nyamboge katika mkutano wa hadhara ulifanyika katika kata hio


Tahadhari Dhidi ya Wizi wa Watoto

Mhe. Komba pia alitumia fursa hiyo kuzungumzia suala la wizi wa watoto, akieleza kuwa uzushi kama huo unaweza kuwapa fursa watu wenye nia mbaya. Alisema, "Panapokuwa na maneno ya uzushi, watu wenye nia mbaya wanaweza kutumia fursa hiyo kufanikisha matendo yao maovu. Tunapaswa kuongeza nguvu na kushirikiana kama jamii ili kuhakikisha usalama wa watoto wetu."

Alisisitiza umuhimu wa ulinzi shirikishi katika ngazi ya jamii, akiwataka wananchi kutoa taarifa za vitendo vya uhalifu kama vile wizi, ubakaji, na uporaji, ili kusaidia serikali kudhibiti vitendo hivyo.

Wananchi wa kata ya Nyamboge wakifuatilia kwa makini mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata hio Oktoba 24, 2024

Mwenge wa Uhuru 2024

Mkuu huyo wa wilaya alieleza kuwa mwaka 2024, Mwenge wa Uhuru utapita katika kata ya Nyamboge, ambapo miradi mbalimbali itazinduliwa na wananchi watapata nafasi ya kushiriki. Alitoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kuupokea Mwenge na kushiriki kikamilifu kwenye mbio hizo.

“Wajibu wetu ni kujitokeza kwa wingi hapa Nyamboge na baadaye kushirikiana kukesha viwanja vya stand ya Nkome,” alihimiza Mhe. Komba.

Ushiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Aidha, Mhe. Komba alisisitiza umuhimu wa wananchi kujiandikisha katika daftari la wapiga kura ili kushiriki kikamilifu kwenye uchaguzi wa viongozi wa serikali za mitaa. Alisema, “Jitokezeni kwa wingi kupiga kura ili tupate viongozi bora watakaosaidia kusukuma mbele maendeleo ya kata yetu.”

Utatuzi wa Kero za Maji na Umeme

Katika mkutano huo, wananchi wa kata ya Nyamboge walimweleza Mhe. Komba changamoto za upatikanaji wa maji katika kijiji cha Lukaya, ambapo mradi wa maji unaotumia nishati ya sola umeshindwa kusukuma maji ya kutosha kutokana na nguvu ndogo ya sola hiyo. Aidha, kijiji cha Chilameno kililalamikia kutokuwa na kisima cha maji.



Mwananchi kutoka kata ya Nyamboge akitoa kero ya maji, katika kijiji cha Lukaya mbele ya mkuu wa Wilaya ya Geita. 

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Hashim Komba (katikati) akizikiliza kero ya mwananchi wa kata ya Nyamboge

Mhe. Komba alieleza kuwa kuna mradi mkubwa wa maji unaoendelea kutekelezwa, ambao utahusisha pia kata ya Nyamboge. Pia aliagiza mamlaka ya maji RUWASA kuhakikisha wanatekeleza mradi wa ujenzi wa kisima katika kijiji cha Chilameno.


Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe.Hashim Komba (wa kwanza kulia) akitoa maelekezo kwa Meneja wa RUWASA Charles Sunday (wa pili kulia) juu ya utatuzi wa kero ya maji kwa wananchi wa Nyamboge

Katika suala la umeme, wananchi walilalamikia baadhi ya vijiji kutokufikiwa na nishati hiyo. Mhe. Komba alibainisha kuwa nia ya serikali ni kuhakikisha umeme unafika kwenye kila kijiji, na kuwa wananchi wanapaswa kuwa na imani kwamba serikali iko kwenye mchakato wa kutatua changamoto hiyo.

Changamoto za Kilimo na Elimu

Mhe. Komba pia alizungumzia changamoto za kilimo, ambapo wananchi walieleza kuwa bei ya pembejeo ni ya juu, hali inayokwamisha maendeleo ya kilimo katika kata hiyo. Mhe. Komba alifafanua kuwa serikali inachukua hatua za kuhakikisha pembejeo zinapatikana kwa bei nafuu ili wakulima waweze kuzimudu.

Aidha, alisisitiza kuwa changamoto za elimu pia zimetatuliwa na serikali kwa kiasi kikubwa, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuboresha sekta hiyo kwa manufaa ya wananchi wote.

Mkutano huo ulihudhuriwa pia na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Dr. Modest, pamoja na wataalamu kutoka halmashauri hiyo.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI. June 05, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA URATIBU WA MWENGE WA UHURU MKOA YATEMBELEA YATEMBELEA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA, GEITA.

    June 24, 2025
  • ZAIDI YA BILIONI 50 ZATUMIKA KUKAMILISHA MIRADI GEITA 2020-2025.

    June 21, 2025
  • RAISI DKT. SAMIA AZINDUA DARAJA LA KIGOGO-BUSISI.

    June 19, 2025
  • WATUMISHI WILAYANI GEITA WAKUMBUSHWA SUALA LA KUJIFANYIA TATHMINI.

    June 18, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa