• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MAKARANI WA SENSA WATAKIWA KUFANYA ZOEZI HILO KWA UZALENDO MKUBWA ILI KUISAIDIA SERIKALI YAO KUFIKIA MALENGO YALIYOKUSUDIWA

Posted on: August 5th, 2022

Na Michael Kashinde

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Wilson Shimo akiwa na kamati ya ulinzi na usalama Wilaya ya Geita  na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Adv. John Wanga wakizungumza na makarani wa Sensa wanaoendelea kupatiwa mafunzo wamewataka kutanguliza uzalendo katika zoezi wanalokwenda kulisimamia Agosti 23 mwaka huu.

Mhe. Shimo akizungumza na Makarani hao Agosti 3 na 4 katika  Shule ya Sekondari Bugando na Shule ya Msingi Nyarugusu ambapo kuna vituo vya kutolea mafunzo kwa Makarani wa Sensa amesema kuwa zoezi hili ni zaidi ya Ukarani  kwa kuwa Serikali inawategemea wao kuiwakilisha Nchi na Taifa ili kupata takwimu sahihi.

Amesema kuwa zoezi hilo ni kubwa na litaisaidia Serikali kupanga mipango yake kwa usahihi baada ya kupata takwimu halisi za wananchi wake hivyo amewataka kutumia mbinu mbalimbali wanazofundishwa zitakazowasaidia kupata ushirikiano wa moja kwa moja kutoka kwa wananchi ili na wao  wawe huru kutoa taarifa sahihi zinazohitajika.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Adv. John Wanga ambaye amekuwa na desturi ya kupitia vituo hivyo kila siku tangu mafunzo hayo yameanza amekuwa akitoa wito kwa Makarani hao kutunza vifaa mbalimbali wanavyopewa kwa ajili ya zoezi hilo na kuvitumia kwa kazi iliyopangwa pekee.

Adv. Wanga amesema kuwa Serikali imetumia gharama kubwa kununua vifa hivyo ili kufanikisha zoezi la Sensa akitolea mfano wa kifaa kinachoitwa Kishikwambi kuwa kinahitaji umakini wa hali ya juu kwa kuwa kuharibika au kupotea kwa kifaa hicho kunaweza kupoteza pia taarifa muhimu suala linaloweza kuharibu zoezi huku akisisitiza kuwa sheria itachukua mkondo wake kwa wale watakaojaribu kuharibu zoezi kwa uzembe.

Michael Francis Bundala ambaye pia ni karani wa Sensa mwaka 2022 aliyekuwa akipatiwa mafunzo katika Shule ya Sekondari Bugando baada ya kufanya Mtihani wake Agosti 5 amesema kuwa wanashukuru kwa mafunzo hayo ambayo yamewapa pia majibu ya mitihani hiyo akieleza kuwa mafunzo hayo yana tija hata wakienda kazini watakuwa na uelewa wa kutosha kufanya zoezi hilo.

Makarani wa Sensa katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita wanaendelea kupatiwa mafunzo katika vituo ya Bugando, Nyarugusu na Katoro ikiwa ni sehemu ya maadalizi ya msingi kabisa kuelekea zoezi hilo la kitaifa la kuhesabu watu ambao watalala nchini usiku wa Agosti 23, Kwa kauli mbiu ya "SENSA KWA MAENDELEO, JIANDAE KUHESABIWA'' ni dhahiri kuwa kila mtanzania anawajibika katika kufanikisha zoezi hili hivyo kila mtu kwa nafasi yake akiamua pia kumhamasisha na jirani yake bila shaka litafanikiwa.


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • UBORESHAJIWA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025 WAFIKIA KIKOMO GEITA.

    May 08, 2025
  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa