• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MAHAKAMA KUU KANDA YA GEITA YATOA ELIMU YA SHERIA KWA WATENDAJI WA KATA NA VIJIJI GEITA DC

Posted on: January 28th, 2025

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Geita leo Januari 28, 2025 imetoa Elimu ya masuala ya sheria kwa watumishi wa umma Halmashauri ya Wilaya ya Geita ili kuwajengea uwezo Watendaji wa kata na vijiji katika maeneo yao ya kazi.

Awali akifungua mafunzo hayo katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita –Nzera, Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Geita Mhe Kevin Mhina amesema  Mahakama Kuu kanda ya Geita imeona umuhimu wa kuwapatia elimu ya maswala ya sheria watendaji kwani ni watu muhimu katika utumishi wa umma kuisaidia jamii.

“Tunatambua umuhimu  wa watendaji kwenye mnyororo wa haki na muunganiko wa kazi zenu  na kazi za haki na maswala yote yanayohusu mambo ya mahakama katika majukumu yenu kama watendaji katika jamii kwa mustakabali wa nchi na mkoa wetu wa Geita”Amesema Mhe Jaji Mhina.

Mhe Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Geita Kevin Mhina akizungumza na watendaji wa kata na vijiji katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita-Nzera

Aidha Mhe Jaji Mhina amesema kuwa mahakama hiyo inatumia mifumo na hakuna matumizi ya karatasi lengo likiwa ni kuendana na teknolojia ya dunia na kuongeza kuwa mahakama hiyo katika wiki ya sheria imejipanga kutoa elimu kwa wananchi kuhusu maswala ya kisheria.

Kwa Upande wake Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita na Mpatanishi wa Migogoro Nchini, Ndg Majaliwa Yohana amewakumbusha watendaji hao majukumu yao katika jamii hususani katika maswala ya kisheria iliwaweze kuisaidia Halmashauri na kuepusha migogoro katika jamii.

Aidha Majaliwa amewataka watendaji hao kusimamia maswala ya usalama na kudumisha amani na utulivu katika maeneo yao ya utawala ikiwa ni pamoja na kupitia mipango na bajeti pamoja na kusimamia utekelezaji wake sambamba na kuwahamasisha wananchi kushiriki katika shughuli za maendeleo.

Naye Hakimu Mkazi Mahakama ya Geita Mhe Frank Waane amewataka watendaji hao kwenda kusimamia na kutekeleza amri za mahakama, na usuluhishi wa maswala ya ndoa kwani wao wana nafasi katika muhimili wa mahakama.

“Watendaji wa Vijiji na Kata wanatambulika kisheria chini kifungu cha 51 na 56 cha sheria ya mahakimu ya mahakama sura ya 11 ya mwaka 2019 kuwa ni walinzi wa amani katika maeneo wanayo yahudumia. Amesema Mhe Waane.

Katika mafunzo hayo, Mhe Mary Kazungu, msaidizi wa sheria wa Jaji Mahakama kuu kanda ya Geita amewakumbusha watendaji hao majukumu yao mahakamani katika utoaji wa ushahidi kwa kuwa  wanapata taarifa mbalimbali juu ya migogoro inayowakabili wananchi katika maeneo yao.

Mhe Mary Kazungu, msaidizi wa sheria wa Jaji Mahakama kuu kanda ya Geita akizungumza na watendaji wa kata na vijiji katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita-Nzera 

Mhe Kazungu amewataka watendaji  hao kuwaelekeza wananchi mabaraza yanayotoa huduma za usuhishi wa ndoa kwa kuwa yanatambulika kisheria chini ya kifungu cha 102 cha sheria ya ndoa ya mwaka 1971 na yamewekwa katika ofisi za kata na sio kijiji.

Vilevile watendaji hao wametakiwa kuwafichua wahamiaji haramu katika maeneo yao ya utawala. Hayo yamesemwa na Afisa Uhamiaji Koplo Isihaka Abasi  ambapo amewataka watendaji kushirikiana na maafisa uhamiaji kata kwa ajili ya kidhibiti wahamiaji haramu wanaoingia katika maeneo yao.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita ambaye pia ni Mganga Mkuu wa Wilaya Dkt Modest Burchad ameishukuru Mahakama ya Kanda Mkoa wa Geita kwa kutoa mafunzo kwa Watendeji hao ili kuwajengea uwezo katika maeneo yao ya kiutendaji katika Halmashauri.

Hakimu Mkazi Mahakama ya Geita Mhe Bruno Fredrick akiwaasa Watendaji wa Kata na Vijiji kuzingatia uandishi wa maungamo kunapolekea kufutwa kwa kesi nyingi kwa  kuwa yanakosewa.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa