• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

Mahafali ya Saba ya Shule ya Sekondari Lutozo Geita DC Yang'ara

Posted on: October 5th, 2023

Jumla ya wanafunzi 394 wa kidato cha nne shule ya Sekondari Lutozo iliyopo kata ya Katoro Wilayani Geita wamehitimu kidato cha nne wasichana wakiwa 184 na wavulana 210.

Akisoma risala Katika mahafali ya Saba ya Shule hiyo, Mwalimu Revocatus John Malaha ambaye ni mkuu wa Shule hiyo amesema wanafunzi wanaoagwa walianza kidato cha kwanza mwaka 2020 wakiwa 479 kati yao wasichana wakiwa 234 na wavulana 245.

Mahala, alisema, shule hiyo imekuwa ya kwanza Katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita huku akipongeza jitihada za walimu, wazazi, wafanyabiasha pamoja na Mh Benedicto Kigongo ambaye ni diwani wa kata ya Katoro .

Aidha alisema shule hiyo imepata Kibali cha kuanzisha kidato cha tano na sita kwa michepuo ya Sayansi na sanaa.

Akizitaja changamoto, Mkuu huyo wa shule alisema, wanakabiliwa na upungufu wa walimu wa masomo ya Sayansi,  tatizo la maji safi na Salama pamoja na ukosefu wa mabweni  kwa wanafunzi wanaoshi mbali na mahitaj ya kidato cha tano na sita.

Naye Diwani wa kata hiyo Mhe Benedicto Kigongo amefarijika kwa jinsi wazazi wanavyojitoa kuchangia maendeleo ya shule ya Lutozo.

" Najua changamoto ni nyingi Lakini Serikalini yetu sikivu inayoongozwa na Mh Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania itaendelea kutatua changamoto zilizopo kadri fedha za miradi zinavyotoka kufika kwenye Halmashauri Yetu" alisema Kigongo.


Mgeni rasmi katika mahafali hayo ya saba Kaimu Afisa elimu Sekondari Mwalimu Richard Makoye akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Geita Mh Martini Shigela amewataka wahitimu hao kuwa na utii na nidhamu kwa jamii ili wastawi Kwenye maadili mema. " Mkawe mfano mzuri kwa jamii huku mkiyashika yote mliyoelekezwa na walimu wenu kuendelea kusimamia malezi bora yenye maadili ya Kitanzania" alisema Makoye.


Aidha Katika hotuba yake, Makoye aliwataka wahitimu hao kumtanguliza Mwenyezi Mungu katika maandalizi ya mitihani ijayo na kusimama katika misingi mizuri.

" Serikali itajivunia kuwa na vijana mahiri kuijenga nchi yao na  niwatake kuzipambania fursa za masomo ya ufadhili ( Mfuko wa mama Samia ) zinazotolewa na Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais  Dkt Samia Suluhu Hassan na kuifanya shule hii kuendelea kuwa The Giant school,"  ili kuendelea kuuletea Mkoa wetu wa Geita sifa,"Alisema Makoye.


Pamoja na kuwatunuku vyeti na zawadi wahitimu hao, Kaimu Afisa elimu huyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa aliweza kuongoza zoezi la Harambee ili kufanikisha ujenzi wa mabweni mawili na bwalo ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Geita ilitoa jumla ya mifuko 20 huku wageni waalikwa wakitoa jumla ya mifuko ya saruji 204 na kiasi cha shilingi 5,350,000


Mahafali hayo yalihudhuriwa na watu mbalimbali wakiwepo waheshimiwa madiwani, watendaji kata,  wenyeviti wa vijiji na wakuu wa shule za Halmashauri ya Wilaya ya Geita

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa