• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MAADHIMISHO YA SIKU YA UKIMWI GEITA YAACHA UJUMBE MZITO KWA JAMII

Posted on: November 25th, 2024

Halmashauri ya Wilaya ya Geita imeadhimisha Siku ya UKIMWI Duniani mnamo Novemba 25, 2024, katika Kata ya Nyaruyeye, kwa lengo la kuhamasisha jamii kujikinga dhidi ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU) na kuhimiza umuhimu wa kujua hali za afya. Tukio hilo lililofanyika chini ya kauli mbiu "Chagua Njia Sahihi, Tokomeza UKIMWI" lilihudhuriwa na viongozi wa serikali, wawakilishi wa mashirika yasiyo ya kiserikali, na wananchi kutoka maeneo mbalimbali.

 

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Geita Mhe khadija Said, akizungumza na wananchi waliohudhuria katika maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani yaliyofanyika katika Kata ya Nyaruyeye.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Mheshimiwa Khadija Said, ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Nyamigota, aliongoza maadhimisho hayo na kusisitiza umuhimu wa kila mmoja kujitokeza kwa upimaji wa hiari.

"Afya zetu ndizo msingi wa kila kitu. Kupima afya ni hatua ya kwanza ya kujilinda na kuendelea kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo. Niwaombe ndugu zangu, tujitokeze kwa wingi kufuatia maadhimisho haya," alisema Mheshimiwa Khadija.

 

Wananchi wa Kata ya Nyaruyeye wakiwa katika zoezi la upimaji wa afya, katika maadhimisho ya siku ya Ukimwi 

Maadhimisho hayo yalihusisha huduma za bure za upimaji wa VVU, uchunguzi wa saratani ya mlango wa kizazi, na upimaji wa magonjwa yasiyoambukiza, yakifanikishwa kwa ushirikiano na mashirika kama ICAP, SHDEPHA, HACOCA, na H-PON. Wananchi waliojitokeza walitoa shukrani kwa huduma hizo, wakisisitiza umuhimu wa kuwa na taarifa sahihi kuhusu hali zao za kiafya.

 

Wananchi wa kata ya Nyaruyeye wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya ukimwi 

Ernest Daudi Gawile, mkazi wa Nyaruyeye, alisema:

"Nimepima afya yangu kwa sababu nimeona umuhimu wake, hasa kwa kuwa huduma hizi ni bure. Nawashauri wananchi wenzangu, tusikose nafasi kama hii."

Kwa upande wake, Musa Stephano, mchimbaji wa madini, alisema mazingira ya migodini yamekuwa na changamoto kubwa za maambukizi, hivyo hatua ya kujua hali ya afya ni muhimu sana.

 

Kwa mujibu wa Mratibu wa UKIMWI wa Halmashauri ya wilaya ya Geita, Bi Mathalene Mgina, amesema takwimu za hivi karibuni zinaonesha idadi kubwa Zaidi ya maambukizi kwa wanawake wa umri kati ya miaka 15-24 ukilinganisha na idadi ya wanaume wanaoambukizwa katika umri huo. Aliongeza kuwa idadi kubwa ya maambukizi ipo katika maeneo ya machimbo ya dhahabu na mialo ya uvuvi, ambako hali za kijamii na kiuchumi zinachochea maambukizi.

Katika hafla hiyo, mgeni rasmi alikabidhi  msaada wa sare za shule na madaftari kwa watoto 40 wanaoishi na virusi vya ukimwi Pamoja na wanaotoka kwenye mazingira hatarishi ya kuambukizwa virusi vya UKIMWI., huku akitoa shukrani kwa mashirika yasiyo ya kiserikali kwa mchango wao mkubwa katika mapambano dhidi ya UKIMWI.

Mhe Khadija Said, Mgeni rasmi akikabidhi msaada wa mahitaji ya shule, kama Sare za shule na daftari kwa wanafunzi wenye wanaoishi na Maambukizi ya virusi, misaada hiyo ilipokelewa na waalimu wakuu

"Ni muhimu tushirikiane sote kama jamii na wadau mbalimbali ili kufanikisha jitihada za Serikali katika kukabiliana na ugonjwa huu," alisisitiza Mheshimiwa Khadija.

 

Burudani kutoka Kwaya ya Mwanzo Mgumu ya Nyaruyeye iliwapa hamasa washiriki wa tukio hilo, lililoweka alama ya kudumu kwa jamii ya Nyaruyeye kuhusu umuhimu wa kuchukua hatua za kinga, kujua hali za afya, na kuishi kwa tahadhari zaidi.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa