• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

KUJITOA KWENYE MRADI KWA MKANDARASI ALIYEKUWA NA JUKUMU LA KUUNGANISHA UMEME WA REA GEITA KUMETAJWA KUWA SABABU YA MRADI HUO KUSIMAMA KWA SASA

Posted on: November 18th, 2021

Imeelezwa kuwa kutokuunganishwa kwa umeme wa REA  hadi sasa katika maeneo mengi ya Wilaya ya Geita, hususani kata za Isulwabutundwe na Vijiji vyake vya Igaka,Ibisabageni na Nyakaduha  kumesababishwa na Mkandarasi aliyepewa kazi ya kuunganisha umeme katika Mkoa wa Geita amejitoa.

Bw.Joseph Essau kutoka ofisi za TANESCO Wilaya ya Geita amenukuliwa alipokuwa akijibu maswali ya Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Novemba 12, 2021 katika mkutano wa kawaida wa Baraza la Madiwani wa robo ya kwanza kwa mwaka wa fedha 2021/2022, uliokuwa ukijadili taarifa ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo ngazi  ya kata kwa  kipindi cha  kuanzia  Julai hadi Septemba 2021.

Maswali ya msingi ya  Mh.Sabina Mathias Lupuga diwani wa viti maalumu na Mh.Renatus Marco Ntelembi diwani wa kata ya Nyawilimilwa walitaka kujua ni lini huduma hiyo itawafikia wananchi wa  kata za Isulwabutundwe, Kakubilo na Vitongoji vyote vya Nyawilimilwa na Ntinachi.

Akijibu Maswali hayo Bw.joseph Essau alisema kuwa Mkandarasi aliyepewa kazi ya kuunganisha Mradi wa umeme wa REA katika Mkoa wa Geita alijitoa, ambapo kwa sasa Wizara kwa  kushirikiana na TANESCO wanaendelea kumtafuta mkandarasi mwingine wa kuendelea na kazi hiyo huku akiahidi ndani ya kipindi cha miezi mitatu atakuwa amepatikana.

Aidha bw.Essau amewataka waheshimiwa madiwani kuwaondoa hofu wananchi na kuwataka kuwa subira kwa kipindi hiki cha kusubiri mkandarasi apatikane huku akisisitiza kuwa kazi hiyo itakapoanza itafanyika kwa haraka na kwa umakini mkubwa ili kuwasaiidia wananchi wa maeneo hayo.

Kwa mujibu wa Mh.Renatus Ntelembi  diwani wa kata ya Nyawilimilwa umeme haujafika katika kijiji cha Kibwela na umeme Jazirishi unahitajika katika Vitongoji vyote vya Nyawilimilwa na Ntinachi.

Huduma hiyo ya nishati ya umeme inahitajika katika kata ya Isulwabutundwe na vijiji vyake vya Igaka, Ibisabageni, na Nyakaduha na baadhi ya maeneo ya kata ya Kakubilo na vijiji vyake vya Barasana,kabayole,Luhala na Kikwete kama alivyoeleza diwani wa viti maalumu Mh.Sabina Lupuga.  

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa