• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU KITAIFA AFURAHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI GEITA DC

Posted on: October 9th, 2024

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndg Godfrey Eliakimu Mnzava amepongeza namna miradi ya maendeleo inavyotekelezwa Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Mnzava ameyasema hayo wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru Oktoba 5, 2024 wakati ulipokimbizwa ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita umbali wa 45.6 km kutoka eneo la mapokezi kata ya Bugulula hadi eneo la mkesha kata ya Nkome na Kuzindua, kuona,pamoja na kuweka mawe ya Msingi katika Miradi mbalimbali ya maendeleo.

KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

“Tunza Mazingira na Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa ujenzi wa Taifa Endelevu” ni kauli mbiu ambayo imetawala kila kona ya Nchi ya Tanzania kufuatia tukio kubwa  la Kikatiba  na kidemokrasia  litakalofanyika Novemba 27, 2024 kote nchini la uchaguzi wa serikali za mitaa.

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru ndg Mnzava amewasihi wananchi kuendea kutunza amani ya nchi kwa wivu mkubwa na kuwataka kujitokeza kwa wingi siku ya uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27, 2024 ikiwa ni pamoja na kuwataka wananchi kuchuja na kuwapima wagombea huku wakiepuka rushwa. “Tujitokeze kwa wingi kwenye mikutano ya hadhara ya wagombea ili kusikiliza sera zao, uwezo wao na kisha kuchagua viongozi watakaotuunganisha na kutuletea maendeleo” amesema Mnzava.

UWEZESHAJI WA VIJANA KUPITIA MIKOPO YA HALMASHAURI

Mwenge wa Uhuru 2024 umetembelea kikundi cha vijana Masakuro chenye mradi wa kukodisha baiskeli ambacho kilikopeshwa kiasi cha shilingi milioni 15 na Halmashauri kwa ajili ya kuendesha mradi wa kukodisha baiskeli ambapo Ndg Mnzava amekipongeza kikundi hicho cha vijana kwa namna kinavyoendesha  shughuli zake ikiwa ni pamoja na kurejesha mkopo huo kwa wakati. 

Pamoja na pongezi hizo ndg Mnzava ameitaka Halmashauri kuendelea kuviratibu na kuvisimamia vikundi vingine vinavyopewa mikopo na serikali ili kurejesha kwa uaminifu ili kuendelea kujenga uchumi.

UTEKELEZAJI WA MIRADI KUPITIA MAPATO YA NDANI

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa ndg Godfrey Eliakimu Mnzava akiwa kata ya Nzera amezindua ofisi ya Kata iliyojengwa kwa mapato ya ndani jumla ya shilingi 117,257,879. 

Mnzava ameipongeza Halmashauri kwa kutenga mapato ya ndani kujenga ofisi kisasa ambayo watumishi watafurahia kufanya kazi katika ofisi hiyo.”Tumefurahishwa kwa namna ambavyo Halmashauri imetenga fedha za mapato ya ndani kujenga ofisi ya kisasa kwa ajili ya watumishi watakaofanya kazi katika mazingira mazuri na ya kupendeza” amesema Mnzava

UIMARISHAJI WA MIUNDOMBINU YA BARABARA

Mwenge wa Uhuru ukiwa katika kata ya Nzera umeweza kuweka jiwe la msingi kwenye barabara ya lami nyepesi inayosimamiwa na TARURA yenye urefu wa kilometa 1.1 yenye thamani ya shilingi milioni 737, 494,984.00 ambazo ni fedha zitokanazo na tozo ya mafuta.

Ndg Mnzava ameipongeza TARURA kwa namna wanavyotumia mfumo wa manunuzi NEST katika kutekeleza mradi huo. “Lengo la Serikali ni kuendelea kuboresha maisha ya wananchi, vitendo ni utekelezaji na tumeona hivyo ni wasihi wananchi kuendelea kutunza miradi hii.” Amesema Mnzava.

UTEKELEZAJI WA FALSAFA YA MWENGE WA UHURU

Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alitamka maneno ya Kifalsafa kwa kusema “Sisi tumekwisha uwasha Mwenge wa uhuru na kuuweka juu ya Mlima Kilimanjaro, umulike ndani na nje ya mipaka yetu, ulete matumani pale ambapo hakuna matumani , ulete upendo mahali penye chuki na heshima mahali palipo jaa dharau.

Hii imedhihirika pale ambapo Mkimbiza Mwenge wa Uhuru kitaifa ndg Mnzava alipogawa Bima ya Afya ya jamii iliyoboreshwa (ICHF), Sukari, Penseli na madaftari kama sehemu ya zawadi kwa watoto wenye mahitaji maalumu pamoja na familia zao.

Akigawa vifaa hivyo ndg Godfrey Mnzava kwa watoto hao ambao wamewakilisha watoto wengine wenye mahitaji maalumu ambao wako katika  maeneo mbali mbali ya  Halmashauri ametoa wito kwa jamii kuonyesha upendo kwa watoto hao.“Tusiwanyanyase tuendelee kuonyesha upendo kwa watoto wenye mahitaji maalum”. Amesema Mnzava.

MIRADI YA AFYA

Mwenge wa Uhuru umetembelea na kuweka jiwe la msingi ujenzi wa Kituo cha afya Kata ya Nkome chenye majengo matatu Jengo la Wagonjwa wa Nje (OPD), Jengo la Maabara, na Wodi ya Wazazi (Maternity) unatekelezwa kupitia Mpango wa CSR huku ukitarajiwa kukamilika tarehe 31 Oktoba 2024 ambapo wananchi wa Nkome wapatao 60,000 hawatalazimika kusafiri umbali mrefu kwenda kupata huduma za afya. 

Kituo hicho kitapunguza msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya Wilaya iliyopo Nzera.

MAPAMBANO DHIDI YA MALARIA

Mwenge wa uhuru 2024 umeendelea kuhamasisha kampeni ya kupambana na malaria kupitia kauli mbiu isemayo “Ziro Malaria inaanza na Mimi- Nachukua hatua kuitokomeza” ambapo kiongozi wa mbio za Mwenge ndg Mnzava amegawa  vyandarua kwa wawakilishi wa makundi maalumu  (wazee, wajawazito na Watoto) ili kujikinga na mbu waenezao Malaria.

Halmashauri ya Wilaya ya Geita imefanya kampeni ya kitaifa ya ugawaji wa vyandarua kwenye jamii (kaya) kwa kata zote 37 kwa kipindi cha mwezi August hadi Oktoba 2024, ambapo kaya 175,337 (asilimia 95), watu 1,234,473 (asilimia 112) waliandikishwa na jumla ya vyandarua vilitolewa kwa kaya zote ni 660,734. Vyandarua vya kampeni vimetolewa nchini kwa ufadhili wa JHUCCP na USAID kupitia Mfuko wa Rais wa Kudhibiti Malaria (PMI).

MAZINGIRA

Sheria ya Usimamizi wa Mazingira Sura 191 imeweka masharti yanayozuia uharibifu na uchafuzi wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumi na kijamii. Katika kusimamia sheria,kanuni na miongozo inayotolewa na serikali juu ya uhifadhi wa Mazingira, misitu na rasilimali  zake, Halmashauri ya wilaya ya Geita imeendelea kutambua juhudi na mchango wa wananchi na vikundi vinavyojishughulisha na hifadhi ya mazingira na kuenzi juhudi za wananchi wanaojitolea kutunza, kusimamia na kuhifadhi mazingira ambapo kiongozi wa Mbio za Mwenge amekabidhi vifaa vya usafi kwa kikundi cha usafi cha Red cross kata ya Nkome venye thamani ya shilingi milioni 2. Aidha katika kuyatunza mazingira Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndg Godfrey Eliakimu Mnzava ameweka jiwe la Msingi pamoja na kupanda mti wa kumbukumbu katika shamba la miti lililopo kijiji cha Igate linalomilikiwa na mwananchi.

Halmashauri ya Wilaya ya Geita inaendelea kuishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kutoa fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo zikiwepo shule, miradi ya afya, maji na miundombinu mizuri katika kuendelea kukuza uchumi wa Taifa.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa