• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

KAZUNGU AWATAKA WATAALAMU KUWASHIRIKISHA MADIWANI KATIKA KUANDAA TAARIFA ZA MAENDELEO YA KATA

Posted on: February 2nd, 2022

Katika kuendeleza ushirikiano kwenye majukumu mbalimbali ya ujenzi wa Taifa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe.Charles Kazungu amewataka wataalamu kuwashirikisha moja kwa moja Madiwani katika kuandaa taarifa za kata zao.

Ametoa wito huo Februari 2, 2022 wakati akiahirisha mkutano wa kawaida wa baraza la Madiwani wa robo ya pili kwa mwaka wa fedha 2021/2022 kwa siku ya kwanza uliokuwa unapokea taarifa za utekelezaji wa shughuli za maendeleo ngazi ya kata kwa kipindi cha Oktoba hadi Disemba 2021.

Mhe.Kazungu amewataka madiwani kushirikishwa katika uandaaji wa taarifa hizo za kata ili wawe na uelewa wa kutosha kwa kuwa wao ndio wanaoziwasilisha taarifa hizo katika mikutano ya mabaraza huku akiwashauri wataalamu hao kuandaa mchanganuo wa matumizi ya fedha za uviko 19 hali itakayoisaidia Halmashauri kuwa na makisio sahihi ya ujenzi wa miundombinu mingine ya aina hiyo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita John Paul Wanga ametoa wito kwa Uongozi wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya kufuatilia changamoto za mgawanyiko wa viongozi hasa wanasiasa katika kata Nyawilimilwa zinazosababisha ushawishi kwa wananchi wasichangie miradi ya maendeleo.

Wito huo umekuja kufuatia taarifa ya kata ya Nyawilimilwa kuonesha changamoto hiyo ya mgawanyiko wa viongozi wa siasa ambao wametofautiana na kushawishi wananchi wasichangie shughuli ya maendeleo ambapo Mkurugenzi Wanga amekemea hilo na kutoa wito wa kuwashirikisha wananchi katika kuchangia shughuli za maendeleo ili wawe na uchungu na kile walichokianzisha kwa faida yao.

Baada ya jukumu la siku ya kwanza la kupokea taarifa za utekelezaji wa shughuli za maendeleo ngazi ya kata kwa kipindi cha mwezi Oktoba hadi Disemba, 2021 mkutano huo wa baraza la Madiwani unatarajiwa kuendelea tena hapo kesho Februari 3, 2022 katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Nzera kwa kujadili taarifa hizo.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI. June 05, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA URATIBU WA MWENGE WA UHURU MKOA YATEMBELEA YATEMBELEA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA, GEITA.

    June 24, 2025
  • ZAIDI YA BILIONI 50 ZATUMIKA KUKAMILISHA MIRADI GEITA 2020-2025.

    June 21, 2025
  • RAISI DKT. SAMIA AZINDUA DARAJA LA KIGOGO-BUSISI.

    June 19, 2025
  • WATUMISHI WILAYANI GEITA WAKUMBUSHWA SUALA LA KUJIFANYIA TATHMINI.

    June 18, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa