• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

KATORO NA MKONO VISION SEKONDARI WAFIKIWA NA ELIMU YA MATUMIZI SAHIHI YA TEHAMA

Posted on: September 30th, 2021

Jamii imeshauriwa kutopenda kuweka taarifa binafsi katika mitandao ya kijamii ili kuepuka kutapeliwa au kuwa watumwa wa baadhi ya watu wenye nia mbaya ambao wanaweza kutumia taarifa hizo kufanya mambo yasiyokubalika katika jamii ikiwemo utapeli.

Rai hiyo imetolewa Septemba 28,2021 na Mhandisi Kadaya Baluhye kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), wakati wa mafunzo ya matumizi sahihi ya Teknolojia ya Habari Mawasiliano (TEHAMA) katika Shule za Sekondari Katoro na Mkono Vision, katika mwendelezo wa mafunzo ya matumizi sahihi ya TEHAMA yanayotolewa na Timu ya uhamasishaji wa matumizi sahihi ya TEHAMA Wilaya ya Geita katika maadhimisho ya wiki ya TEHEMA ki Wilaya.

Mhandisi Baluhye amesema kuwa si vyema kuweka taarifa binafsi katika mitandao ya kijamii kwa kuwa uzoefu unaonyesha baadhi ya matapeli wanaweza kutumia taarifa hizo kuwalaghai watu wengine ambao wasipokuwa makini wanaweza kufikiri ni mhusika mwenyewe hali inayopelekea watu kutapeliwa.

Aidha akiongea na wanafunzi wa shule hizo amewaasa kuacha tabia ya kupenda kupiga picha za faragha hasa wasichana pindi watakapokuwa na umri wa kuanzisha mahusiano, kwa kuwa wakati mwingine baadhi ya watu hasa wanaume wanatumia picha hizo kutaka fedha kwa kutishia kuzisambaza suala linalowageuza kuwa mateka wa watu kwa kuhofia fedheha.

Akiwasilisha mada ya Maktaba Mtandao Bw.Frank Makonda Mkuu wa Idara ya TEHAMA katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita amesema kuwa, matumizi ya TEHAMA kwa Mwanafunzi ni kwa ajili ya kujisomea pekee huku akiwahamasisha kutumia huduma rahisi ya maktaba mtandao Kwa lengo la kuongeza maarifa na sio kwa mambo yasiyowasaidia kitaaluma.

Kwa upande wake Bw.Thomas Novatus Festus Mkuu wa Idara ya TEHAMA katika Halmashauri ya Geita mji akiwasilisha mada ya faida za matumizi ya TEHAMA, amesema kuwa TEHAMA ina faida nyingi kwa mwanafunzi kama vile kufanya tafiti,kujisomea kwa mtandao na hata kuomba mikopo ya elimu za juu huku akisema kuwa Serikali ina mpango wa kuleta vifa vya TEHAMA mashuleni ili kukuza taaluma hiyo.

Aidha Bi.Mwanne Abdallah Afisa usajili wa vizazi na vifo kutoka RITA akizungumza pia na wanafunzi hao amesema kuwa TEHAMA inasaidia sana katika kutunza taarifa za mteja huku akisisitiza kuwa kuna huduma ya usajili kwa njia ya mfumo suala linaloweza kufanywa bila ya kufika sehemu husika kufuatilia cheti cha kuzaliwa huku akiwahamasisha wanafunzi hao kuingia kwenye mfumo kufuatilia vyeti vyao vya kuzaliwa.

Semina hiyo ni mwendelezo wa kuwafikia wadau mbalimbali na kuwaelimisha matumizi sahihi ya TEHAMA katika kuadhimisha wiki ya TEHAMA Wilayani Geita, ikiwa ni Utekelezaji wa kauli mbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu inayosema ‘’TEHAMA ni msingi wa Taifa endelevu itumie kwa usahihi na uwajibikaji’’suala linalowataka wadau wote wa TEHAMA zikiwemo taasisi zilizopewa dhamana hiyo kutoa elimu kwa jamii juu ya matumizi sahihi kwa maendeleo ya nchi yetu.


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa