• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

KATIBU TAWALA MKOA WA GEITA MOHAMED AWATAKA WALIMU KUZINGATIA MAADILI NA MIIKO YA KADA YA ELIMU

Posted on: September 25th, 2024

Katibu Tawala Mkoa wa Geita Ndg Mohamed Gombati, Septemba 25, 2024 amewataka walimu kuendelea kuzingatia maadili na miiko ya kada ya ualimu ili kuendelea kuuletea Mkoa wa Geita sifa njema.

Gombati ameyasema hayo katika hafla ya Kuwapongeza walimu wa shule za Sekondari Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa shule zilizofanya vizuri katika mitihani ya kitaifa kidato cha pili, cha nne na cha sita.


Katibu Tawala wa Wilaya ya Geita Ndg. Mohamed Gombati (katikati) akizungumza na wakuu wa Shule za sekondari, wadau wa elimu na wanafunzi waliohudhuria hafla ya utoaji tuzo iliyofanyika Geita Mjini. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg. Karia Magaro na kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Charles Kazungu.

Walimu hao wametakiwa kuendelea kutoa ushirikiaono baina yao wenyewe, wazazi na Viongozi ili kuendelea vizuri zaidi. " Mafanikio haya yemetokana kwa namna ambavyo Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anavyoboresha maslahi ya walimu ikiwa ni pamoja na miundombinu, hivyo nitoe rai kwenu kuendelea kushirikiana pamoja na kusimamia maadili ya Wanafunzi wetu kuwajenga katika nidhamu ili waheshimu maadili wanayojifunza" amesema Gombati.

Walimu wa shule za Sekondari, wadau wa elimu na wanafunzi wakiwa katika Hafla ya utoaji tuzo kwa shule zilizofanya vizuri katika mtihani wa kidato cha pili, kidato cha nne na kidato cha sita.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe Charles Kazungu amewataka Wakuu wa shule, Maafisa Elimu kuendelea kuongeza bidii na kutokubweteka na ufaulu wa sasa.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg. Charles Kazungu akizungumza na wakuu wa shule za Sekondari wadau wa elimu na wanafunzi katika Hafla ya ugawahi tuzo kwa shule zilizofanya vizuri.

"Sisi Halmashauri ya Wilaya ya Geita tuna asilimia 40 ya shule kimkoa, hivyo tukifanya vizuri tunauinua Mkoa wetu wa Geita" amesema Mhe Kazungu.

Vile vile Mhe Kazungu amewahakikishia walimu hao kuendelea kutoa motisha kwa kuendelea Kuwapongeza ili kutoa chachu ya kuendelea kufanya vizuri.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu, Afya na Maji Halmashauri ya Wilaya ya Geita ambaye pia ni Diwani wa kata ya Nyaruyeye Mhe Malimi Samson amesema taarifa za ufaulu zinaleta faraja na kusema Halmashauri itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kutoa motisha kwa walimu na Wanafunzi wanaofanya vizuri.

Diwani wa kata ya Nyaruyeye Mhe. Malimi Samson Akizungumza katika hafla ya utoaji tuzo

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita ndg Karia Rajabu Magaro amewapongeza walimu kwa kuongeza asilimia ya ufaulu na kusema Halmashauri itaendelea kuboresha bajeti zake ili kuendelea kuwapa motisha walimu na Wanafunzi.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Geita Ndg. Karia Magaro akizungumza katika hafla ya utoaji tuzo.

Pamoja na hayo Afisa Elimu Sekondari Mwalimu Hosanna Nshulo amesema Halmashauri kwa kushirikiana na Serikali Kuu na Sekta binafsi imeweza kuongeza na kusajili shule mpya 29 za Sekondari za Serikali na Shule 2 mpya za Sekondari zisizo za Serikali kwa kipindi cha mwaka 2022 hadi 2024.

Afisa Elimu Sekondary Mwl Hosiana Nshulo akitoa taarifa ya hali ya elimu katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita 


Nshulo ameongeza kwa kusema Serikali inayo ongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan imeleta fedha kwa ajili upanuzi wa shule 2 za Sekondari ili kuwa na kidato cha 5 na 6 na kufanya Halmashauri kuwa na shule za Sekondari 77 kwa kidato cha kwanza hadi cha nne na shule 4 zinazotoa Elimu ya Sekondari ya juu hali ambayo imechangia kuinua kiwango cha taaluma shuleni na ufaulu kwa ujumla.

Baadhi ya watumishi mbalimbali wakitunukiwa

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa