• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA YAHAMASISHA KASI YA MIRADI

Posted on: October 25th, 2024

Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango, Halmashauri ya Wilaya ya Geita, ikiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe Hadija S. Joseph, ikishirikiana na wataalamu wa Halmashauri, imefanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo katika majimbo ya Busanda na Geita Oktoba 24, 2024.

Jimbo la Busanda

Katika Jimbo la Busanda, Kamati ilitembelea miradi kadhaa ikiwa ni pamoja na ujenzi wa shule mpya ya Amali Chibingo inayolenga kufundisha ufundi, ujasiriamali, na kukuza vipaji. Mradi huo, unaotarajiwa kujengwa miundombinu kumi na moja, ikiwemo maabara, ofisi za utawala, madarasa manne, na vyoo, utahudumia zaidi ya wanafunzi 320 baada ya kukamilika kwa madarasa nane. Mwalimu Leonatus Martin, Mkuu wa Sekondari ya Nyamigota, alitoa taarifa ya maendeleo ya mradi huo, ambapo ujenzi uko katika hatua ya kuchimba msingi na kusambaza vifaa vya awali.

Mkuu wa Shule ya Sekondari Nyamigota Mwl Leonatus Martin akisoma taarifa ya mradi, mbele ya kamati ya fedha ilipotembelea mradi huo

Shughuli mbalimbali za ujenzi zikiendedelea katika eneo la ujenzi wa Shule ya Amali.

Kamati pia ilitembelea mradi wa upanuzi wa Shule ya Sekondari Kagega kwa ajili ya kidato cha tano na sita. Upanuzi huu unahusisha ujenzi wa mabweni mawili, madarasa, na matundu ya choo, ambapo kazi inaendelea kwa kuchimba msingi.

Hatua za awali za uchimbaji wa msingi na kusombelea mahitaji ya ujenzi katika shule ya skkondari Kagega


Aidha, Kamati ilipongeza maendeleo ya mradi wa shule mpya ya msingi inayosimamiwa na Shule ya Bwawani. Ujenzi umefika hatua ya msingi na tayari imetandaza jamvi. Wajumbe walisisitiza umuhimu wa kumaliza miradi kwa wakati ili kukidhi mahitaji ya elimu katika eneo hilo.

Kamati katika jimbo la Busanda ilimaliza kwa kutembelea upanuzi wa kidato cha tano na cha sita katika shule ya Sekondari Lutozo, ambapo hatua ya msingi na kuweka jamvi imekamilika.

Jimbo la Geita

Katika Jimbo la Geita, Kamati ya Fedha imetembelea Kata ya Usulwabutundwe, ambapo imekagua mradi wa ujenzi wa nyumba ya mtumishi (pacha) katika Shule ya Sekondari Nyakaduha, mradi wenye thamani ya Shilingi milioni 100,000,000 chanzo cha fedha kikiwa ni mfuko SEQUP. Kamati hiyo imetoa maagizo kwa fundi anayetekeleza mradi huo  kuongeza nguvu kazi ili ujenzi huo ukamilike ifikapo Novemba 30, 2024, sambamba na kuleta vifaa vya ujenzi kwa wakati ili kasi ya ujenzi isisimame.

Ujenzi wa Nyumba ya Mtumishi 2/1 shule ya sekondari Nyakaduha wenye thamani ya shilingi Milioni100,000,000 fedha kutoka mfuko wa SEQUIP. Mradi huu ni sehemu ya mikakati ya Serikali ya awamu ya sita kuendelea kuboresha mazingira mazuri katika sekta ya elimu.

Aidha, Kamati imekagua mradi wa ujenzi wa Shule Mpya ya Sekondari Kakubilo wenye thamani ya Shilingi 584,280,029, fedha za SEQUP. Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mhe. Maeda, ametoa maelekezo kwa mzabuni anayesambaza vifaa vya ujenzi katika mradi huo  kuhakikisha vifaa vya ujenzi vinawasilishwa kwa wakati ili kuondoa ucheleweshaji katika mradi huo.

Kamati ya Fedha uongozi na Mipango pamoja na wataalam kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Geita wakikagua ujenzi wa Mradi wa Shule mpya ya Sekondari Kakubilo wenye thamani ya Shilingi Milioni 584,280,029 fedha kutoka mfuko wa SEQUIP ambapo kamati imeshauri kila fundi apewe mkataba wa kisheria katika kutekeleza mradi huo ili uweze kukamilika ifikapo Novemba 30, 2024 kama ambavyo mkataba wa ujenzi unavyo elekeza.

Katika ziara hiyo, Kamati ilitembelea pia mradi wa shule mpya ya msingi katika Kata ya Kakubilo, ambao una thamani ya Shilingi milioni 351.500,000, fedha za BOOST. Kwa upande wake  Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ikigijo, Mwalimu Leonsio Mpandachombo Lukas, ambaye anasimamia ujenzi wa mradi huo, amesema kasi ya mradi huo si nzuri kutokana na mzabuni kushindwa kufikisha vifaa kwa wakati na kufanya mafundi ujenzi kushindwa kuendelea na kazi.

Ujenzi wa shule mpya ya Msingi Ikigijo  wenye thamani ya shilingi Milioni 351,500,000 fedha kutoka mfuko wa BOOST. Ujenzi wa shule hiyo utasaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi  ambapo unatarajiwa kuwa na madarasa 7 ya elimu ya msingi na madarasa 2 ya elimu ya awali na jengo la utawala.

Kufuatia changamoto mbalimbali katika ukamilishaji wa miradi hiyo, Kamati ya Fedha uongozi na Mipango imeitaka Halmashauri kusimamia  mikataba ya mafundi ili wakamilishe miradi kwa wakati sambamba na kuendelea kuwashauri wazabuni wengine wenye uwezo kujiunga na mfumo wa manunuzi NEST.

Ukamilishaji wa miradi ya shule hizo unaenda kupunguza msongamano wa Wanafunzi. Hizi ni jitihada za Serikali ya awamu ya sita inayo ongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuendelea kutoa Fedha nyingi kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa