• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

JUMLA YA WASICHANA 96,481 KUPATA CHANJO YA HPV-GEITA DC

Posted on: April 24th, 2024

Na: Hendrick Msangi

JUMLA ya Wasichana 96,481 wenye umri wa Miaka 9 hadi 14 wanatarajiwa kupata chanjo ya Human Papillomavirus (HPV) ili kuwakinga kupata saratani ya Mlango wa Kizazi.

Hayo yameelezwa wakati wa uzinduzi wa chanjo ya HPV na shughuli jumuishi za lishe Halmashauri ya Wilaya ya Geita uliofanyika katika shule ya msingi Ihumilo kata ya Nkome Aprili 24, 2024 huku Kauli Mbiu ya wiki ya chanjo kwa mwaka 2024 ikisema, Jamii iliyochanjwa, Jamii yenye Afya.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi ambaye ni Mhe Masumbuko Nsembe Diwani wa Kata ya Nkome, Dkt Maro Willium kutoka Ofisi ya Mganga Mkuu wa Wilaya ya Geita amesema zoezi la utoaji wa chanjo limeanza kutekelezwa Aprili 22, 2024 ambapo linatarajiwa kumalizika ifikapo  Aprili 28, 2024 likienda sambamba na huduma za afua za lishe, huku lengo likiwa ni kuwafikia wasichana 96,481.

  • Mwanafunzi Elizabeth John darasa la sita akipata chanjo ya Human Papillomavirus (HPV) ili kumkinga dhidi ya saratani ya Mlango wa Kizazi.

    • Wanafunzi wa Shule ya Msingi Ihumilo kata ya Nkome wakipewa chanjo ya Human Papillomavirus (HPV) ili kuwakinga dhidi ya saratani ya Mlango wa Kizazi katika uzinduzi wa wiki ya chanjo uliofanyika kata ya Nkome.

Akiendelea kuzungumza katika Uzinduzi wa Chanjo ya HPV na shughuli jumuishi za Lishe , Dkt Maro amesema Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali  wa maendeleo itaendelea kuelimisha jamii ili kutambua umuhimu wa kuwapeleka watoto kliniki kwa lengo la kupata chanjo na elimu. “Serikali itaendelea kutoa elimu ya lishe kupitia klabu za afya na lishe mashuleni na kuendelea kufuata sheria mbalimbali zilizotungwa ili kuhakikisha haki za watoto zinalindwa” Amesema Dkt Maro.

Mhe Masumbuko Nsembe Diwani wa Kata ya Nkome,amewataka wanafunzi wa shule ya msingi Ihumilo kuwa mabalozi kwa wenzao ambao hawajapewa chanjo  huku akiwapongeza walimu kwa kuendelea kutoa ushirikiano kwa wataalam wa afya katika kuwaelemisha wanafunzi mabinti juu ya umuhimu wa chanjo ya HPV

Mhe Nsembe akipokea maelezo kutoka kwa Wataalam wa Afya baada ya uzinduzi wa wiki ya chanjo HPV katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita kata ya Nkome

Akizungumza katika Uzinduzi huo, mgeni rasmi Mhe Masumbuko Nsembe Diwani wa Kata ya Nkome amewataka wasichana wa shule ya msingi Ihumilo ambapo Uzinduzi huo umefanyika kuendelea kuwa mabalozi wazuri kwa wasichana wenzao wenye umri wa miaka 9 hadi 14 ambao hawajapata chanjo hiyo kuona umuhimu wa kupata chanjo ya HPV kwa lengo la kuwalinda na Saratani ya Mlango wa Kizazi.

Aidha Mhe Nsembe amewapongeza walimu kwa kuendelea kutoa ushirikiano kwa wataalam wa afya katika kuwaelemisha wanafunzi mabinti juu ya umuhimu wa chanjo hiyo ambayo serikali inahakikisha inawafikia mabinti wote wanaotakiwa kuchanjwa.

  • Dkt Maro Willium kutoka Ofisi ya Mganga Mkuu wa Wilaya ya Geita amesema amesema Serikali itaendelea  kushirikiana na wadau mbalimbali  wa maendeleo kuelimisha jamii ili kutambua umuhimu wa kuwapeleka watoto kliniki kwa lengo la kupata chanjo na elimu katika kukabilina na magonjwa ikiwemo saratani ya Mlango wa Kizazi.  

Naye Mratibu wa Chanjo Wilaya ya Geita ndugu Jalion Manyi amesema zoezi la Chanjo linaendelea katika kata zote 37 za Halmashauri ya wilaya ya Geita huku jumla ya vituo 60 vya kutolea huduma vikiendelea na zoezi la utoaji wa Chanjo ya HPV. “Tunategemea kufikia jumla ya shule za msingi 234 na sekondari 74 tukishirikiana na walimu pamoja na wataalam wa afya  kwenye vituo vyote vya afya  na kwa wale wasichana ambao wapo mtaani watapata huduma  kupitia vituo maalum vilivyotengwa katika kila kata.” Amesema Jalion Manyi.

Mratibu wa Chanjo Wilaya ya Geita , Jalion Manyi amesema Serikali itaendelea kushirikiana na walimu pamoja na wataalam wa afya  kwenye vituo vyote vya afya  ili kufikia lengo la kuwachaja wanafunzi mabinti katika shule za msingi 234 na sekondari 74 na wale ambao wapo mtaani kwani jumla ya vituo 60  vinatoa huduma ya chanjo ya HPV ili kuwakinga mabinti wenye umri wa miaka 9 hadi 14 dhidi ya maambukizi ya saratani ya Mlango wa Kizazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita

Wakati huo huo Mwanafunzi wa darasa la sita, Elizabeth John mwenye umri wa miaka 13 ameshukuru kwa kupata chanjo hiyo na kusema atawahamasisha na wasichana wengine ili kupata chanjo hiyo muhimu ya kinga dhidi ya maambukizi ya saratani ya mlango wa kizazi.

Serikali Kupitia Wizara ya Afya imepanga hadi kufikia mwezi Disemba 2024 iwe imefikia jumla ya wasichana Milioni 4,841,298 wenye Umri wa Miaka 9 hadi 14 kwa kuwapa dozi moja ya chanjo ya Human Papillomavirus (HPV) baada ya kujiridhirisha kuwa chanjo hiyo haina madhara na kwamba dozi moja inatosha kutoa kinga kamili dhidi ya maambukizi ya saratani ya mlango wa kizazi.

Halmashauri ya Wilaya ya Geita inaendelea kuishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuwezesha vifaa vya kupima na kutibu mabadiliko ya awali ya Saratani ya Mlango wa Kizazi mpaka ngazi ya Zahanati ili kuwa na watanzania wenye afya bora kwa maendeleo ya Taifa lao.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI. June 05, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA URATIBU WA MWENGE WA UHURU MKOA YATEMBELEA YATEMBELEA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA, GEITA.

    June 24, 2025
  • ZAIDI YA BILIONI 50 ZATUMIKA KUKAMILISHA MIRADI GEITA 2020-2025.

    June 21, 2025
  • RAISI DKT. SAMIA AZINDUA DARAJA LA KIGOGO-BUSISI.

    June 19, 2025
  • WATUMISHI WILAYANI GEITA WAKUMBUSHWA SUALA LA KUJIFANYIA TATHMINI.

    June 18, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa