• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

ELIMU YA MATUMIZI SAHIHI YA TEHAMA YAFIKA GESECO

Posted on: September 28th, 2021

Wanafunzi wametakiwa kutumia Tehama kwa lengo la kuongeza maarifa ya kitaaluma kuliko kutumia kwa mambo yasiyo ya msingi kwa kuwa Tehama ikitumika vibaya inaweza kuwa chanzo cha matatizo mbalimbali ikiwemo mmomonyoko wa maadili katika jamii.

Hayo yamebainishwa na Timu ya Uhamasishaji na matumizi sahihi ya Teknolojia ya Habari Mawasiliano (TEHAMA) Wilaya ya Geita wakati ikitoa mafunzo ya matumizi sahihi yaTEHAMA hii leo Septemba 28 kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Geita (GESECO)shuleni hapo.

Akiwawezesha wanafunzi hao Bw.Msajigwa Alfred Mkurugenzi wa Taasisi ya Infodigtech For Empowerment amesema kuwa Matumizi ya TEHAMA  ni muhimu sana kwa wanafunzi na inaweza kuwasaidia katika tafiti,elimu kwa njia ya mtandao,kutafuta machapisho ya kujifunzia na hata majadiliano ya mtandaoni.

 Ameendelea kusema kuwa endapo TEHAMA itatumiwa tofauti na wanafunzi hao kwa matumizi yasiyo ya msingi kama kuangalia picha zisizofaa, inaweza kuchangia kuporomosha maadili yetu suala lisilo na faida katika maisha ya mwanafunzi.

Aidha Mwezeshaji Frank Makonda ambaye pia ni Afisa TEHAMA wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita amesema kuwa ukuaji wa Sekta hiyo ya TEHAMA ni faida kwa wanafunzi hao katika kujisomea kwa kuwa kwa sasa kuna Maktaba mtandaoni inayowawezesha kupata maarifa mbalimbali yanayowahusu.

Amesema kuwa Maktaba mtandaoni inapunguza changamoto za uhaba wa Maktaba kwa kuwa si lazima ufike maktaba kujisomea, kwa kuwa unaweza kupata machapisho mbalimbali kwa njia ya mtandao huku akiwahamasisha wanafunzi hao kutumia fursa hiyo kujifunza kwa urahisi.

Kwa upande wake mwezeshaji Michael Mpamwa kutoka Infodigtech For empowerment amewataka wanafunzi hao kujizuia wenyewe kutumia vibaya TEHAMA kabla ya kuzuiwa na sheria huku akiwatahadharisha kuwa sheria kali zinaendelea kuchukuliwa kwa wanaoitumia vibaya mitandao.

Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo akiwemo Zachari Ezekiel Jembe Mwanafunzi wa kidato cha tano HKL amesema kuwa elimu hiyo imemsaidia kuyafahamu madhara mbalimbali ya kutumia vibaya mitandao lakini kufahamu adhabu anazoweza kuzipata mtu anayetumia vibaya TEHAMA.

Semina hiyo ni mwendelezo wa kuwafikia wadau mbalimbali na kuwaelimisha matumizi sahihi ya TEHAMA katika kuadhimisha wiki ya TEHAMA Wilayani Geita, ikiwa ni Utekelezaji wa kauli mbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu inayosema ‘’TEHAMA ni msingi wa Taifa endelevu itumie kwa usahihi na uwajibikaji’’suala linalowataka wadau wote wa TEHAMA zikiwemo taasisi zilizopewa dhamana hiyo kutoa elimu kwa jamii juu ya matumizi sahihi kwa maendeleo ya nchi yetu.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa