• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA YAHAMASISHA WADAU KUSAIDIA UJENZI WA NYUMBA ZA WALIMU.

Posted on: August 19th, 2021

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Geita Mwl.Edith Mpinzile, ametoa wito kwa Makampuni,Mashirika,Taasisi,na wadau mbalimbali wa maendeleo mkoani Geita, kujitokeza kusaidia miradi ya elimu hasa ujenzi wa nyumba za walimu, katika maeneo ambayo hakuna hata nyumba za kupanga.

Ametoa kauli hiyo leo Agosti 18 alipokuwa akizungumza na Afisa mawasiliano Mwandamizi wa kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML), Bw.Laurian Theophil Pima, ambapo amesema kuwa kuna changamoto kubwa ya uhaba wa  nyumba za walimu, hasa kwenye maeneo ambayo hakuna nyumba za kupanga.

Amesema kuwa  Mwalimu anahitaji kuheshimiwa na kuthaminiwa, ili awe na afya nzuri ya mwili na akili aweze kuzalisha watoto bora.hivyo, ni vyema akajengewa mazingira mazuri, ili afanye kazi zake kwa ufanisi, na hatimaye tupate matokeo mazuri tunayoyategemea.

Kaimu Mkurugenzi Wa Halmashauri ya wilaya ya Geita Mwl.Edith Mpinzile akizungumza ofisini kwake na Afisa Mawasiliano mwandamizi Wa GGML Bw.Laurian Theophil Pima 

Akinukuu kauli mbiu inayopendwa kutumiwa na mkuu wa mkoa wa Geita Bi.Rosemary Senyamule ya “GEITA YA DHAHABU, UTAJIRI NA HESHIMA” Mwl.Mpinzile amesisitiza kuwa, utajiri na heshima vitaonekana, pale wadau watakapojitolea kusaidia miradi ya maendeleo, na kuzalisha wataalamu wa baadae tuliowaandaa wenyewe.

Aidha ameipongeza kampuni ya Geita Gold Mining Limited, kwa mchango wake mkubwa katika maendeleo ya elimu na miradi mingine,ambapo kampuni hiyo imesaidia kujenga vyumba vitatu vya madarasa kwa ajili ya kidato cha tano na sita, mabweni matatu,bwalo la chakula,na kisima cha maji katika shule ya sekondari Bugando kupitia mradi wa fedha zinazotolewa na kampuni kama wajibu wake Kwa jamii yaani CSR.

Madarasa matatu ya A level yaliyojengwa na GGML kupitia mradi CSR katika Shule ya sekondari Bugando iliyopo ndani ya Halmashauri ya wilaya ya Geita

Mabweni matatu yaliyojengwa na GGML kupitia mradi wa CSR Kwa ajili ya wanafunzi Wa A level katika Shule ya sekondari Bugando.

Kwa upande wake makamu mkuu wa shule ya sekondari  bugando mwl.Gibson Petro ameishukuru GGML kupitia mradi wa CSR, kwa kuwasaidia katika ujenzi wa miradi hiyo huku akieleza kuwa kuanzishwa kwa masomo ya kidato cha tano na sita shuleni hapo kumeongeza hamasa na bidii kwa wanafunzi  wa madarasa ya chini ambao wanaonekana kuwa na shauku pia ya kuendelea na masomo ya kidato cha tano na sita,ambapo hata matokeo ya mitihani ya Mock mwaka huu yameboreka

Bwalo la chakula lililojengwa Kwa ufadhili Wa GGML katika Shule ya sekondari Bugando wilayani Geita kupitia mradi wa CSR.

Aidha mwl.Gibson ameendelea kusema kuwa, hata wao kama walimu wanajisikia fahari kufanya kazi kwenye mazingira vutivu,huku akieleza kuwa hata wazazi na jamii kwa ujumla imehamasika kwa kuwa hakukuwa na shule ya kidato cha tano na sita kabla, ambapo kwa sasa hawatahangaika tena kutafuta shule mikoa mingine kwa masomo ya A level  hasa katika michepuo ya sayansi.

Naye Ibrahimu Maulid Mchana Mwanafunzi wa kidato cha tano shuleni hapo katika mchepuo wa PCB ambaye malengo yake ni kuwa Daktari, amesema kuwa uwepo wa maabara shuleni kwao unawasaidia kufanya tafiti mbalimbali za kisayansi na kupata uzoefu, huku Rebeca Laurent mwanafunzi wa kidato cha nne akisema kuwa uwepo wa wanafunzi wenzao wa kidato cha tano na sita ni faida kubwa kwao, kwa kuwa wanapata wanafunzi wenzao wanaowasaidia katika masomo yao kwa ukaribu zaidi.

Wanafunzi Wa kidato cha nne na tano katika shule ya Sekondari Bugando wakifanya majaribio ya kisayansi katika maabara shuleni kwao iliyofadhiliwa na GGML.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa