• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA KINARA MATOKEO MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2024

Posted on: November 4th, 2024

Halmashauri ya Wilaya ya Geita imeongoza kati ya Halmashauri Sita za Mkoa wa Geita katika Matokeo ya Mbio za Mwenge wa Uhuru zilizofanyika Oktoba 5, 2024.

Mbio za Mwenge wa Uhuru 2024 zilianza Mkoani Kilimanjaro Aprili 2, 2024 ambapo Mhe Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa Majaliwa (MB)  alizindua mbio hizo na kuhitimishwa Oktoba 14, 2024 jijini Mwanza na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb), alipozindua mbio za Mwenge wa Uhuru  Aprili 2,2024 katika uwanja wa chuo kikuu cha Ushirikia Moshi. (picha kutoka maktaba)

Akizungumza na Kitengo cha Mawasiliano ya Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Mratibu wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg Alex Herman ameelezea furaha aliyo nayo kwa matokeo hayo na kusema kazi haikuwa ndogo.

Mratibu wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg Alex Herman akiwa kwenye mbio za Mwenge wa Uhuru uliokimbizwa Wilayani Geita Oktoba 5, 2024 na kupelekea Halmashauri ya Wilaya ya Geita kushika nafasi ya 17 Kitaifa.

“Sikutegemea kwa kweli kutokana na misukosuko na changamoto nyingi sana wakati wa maandalizi hayo ila Mwenyezi Mungu amewezesha na hatimaye tumekuwa washindi,” amesema Alex.

Aidha Mratibu huyo ametoa  shukrani kwa kamati zote zilizowezesha mapokezi ya mbio za mwenge wa uhuru 2024.”Kipekee sana nipende kuishukuru kamati ya ulinzi na usalama ikiongozwa na Mkuu  wa Wilaya Mh. Hashim Komba, Mkurugenzi Mtendaji Ndg.Karia Rajabu Magaro,viongozi wa chama na dini, wakuu wa idara na vitengo, Taasisi mbalimbali ikiwepo Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini TARURA na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mjini Geita (GEUWASA), wadau mbalimbali kwa namna walivyotoa michango yao pamoja na wananchi wote kwa jitihada na kuonesha ushirikiano kipindi chote cha maandalizi hadi tulipokabidhi Mwenge wa Uhuru Halmashauri ya Buchosa Wilayani Sengerema Oktoba 6,2024.” ameongeza Alex.

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya Geita Ndg Karia Rajab Magaro (kulia) akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji Geita Mji Ndg Yefred Miyenzi Oktoba 5, 2024 katika viwanja vya shule msingi Bugulula

Pamoja na kuwa ya kwanza Kimkoa, Halmashauri ya Wilaya ya Geita imeshika nafasi ya 6 kwa kanda yenye halmashauri 45 na kushika nafasi ya 17 kitaifa kati ya Halmashauri 195 zilizokimbiza Mwenge wa Uhuru 2024.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe Martine Shigela(Kulia) akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Said Mtanda Oktoba 6,2024 Halmashauri ya Buchosa Wilayani Sengerema baada ya kumaliza kukimbizwa Halmashauri ya Wilaya ya Geita

Mwenge wa Uhuru ni chombo kilichoasisiwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mwaka 1961 ikiwa ni tunu na ishara ya kuwepo kwa Taifa huru la Tanganyika.

Mbio za Mwenge wa Uhuru zilianza rasmi mwaka 1964 baada ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliozaa nchi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mwenge wa uhuru umekuwa kichocheo kikubwa katika kuimarisha uhuru wa Taifa la Tanzania,umoja wa kitaifa, kudumisha amani, kulinda Muungano na kuhamasisha maendeleo ndani na nje ya taifa la Tanzania.

Kauli mbiu ya Mwenge wa Uhuru 2024 imesema “Tunza Mazingira na Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Ujenzi wa Taifa Endelevu”

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan akipokea Mwenge wa Uhuru Oktoba 14, 2024 kutoka kwa Mkimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndg Godfrey Eliakimu Mzava Kwenye hafla ya kilele Cha mbio hizo Uwanja wa CCM Kirumba Mkoani Mwanza . (picha kutoka Maktaba)


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa