• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

GEITA DC YAWEKA KAMBI KATIKA KATA YA NYARUGUSU KUTOA MSAADA WA KISHERIA

Posted on: December 14th, 2022

Na. Michael Kashinde

Wananchi wameshauriwa kutoa taarifa kuanzia ngazi za msingi wanapokutana na changamoto mbalimbali ikiwemo za migogoro katika familia na masuala ya ukatili, kwa kuwa Serikali imeweka miundombinu rafiki inayoweza kuwaongoza kujua wapi wanaweza kupata huduma ya msaada kulingana na uhitaji wanaokuwa nao.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya jamii katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita Bi. Enedy Mwanakatwe akizungumza katika mkutano wa hadhara na wananchi wa Kata ya Nyarugusu Desemba 14, 2022 wakati wa kuhitimisha kambi ya siku moja ya msaada wa kisheria katika kata ya Nyarugusu.

Bi. Mwanakatwe amesema kuwa kuna haja ya kuendelea kutoa Elimu kwa jamii na kuwaunganisha na sehemu sahihi ambapo wanaweza kupata huduma kulingana na mahitaji yao huku akiwahamasisha wananchi hao kutumia ngazi za chini kupata suluhu ya migogoro ya kifamilia ikiwemo mabaraza ya wazee katika ngazi za Kata.

Kwa upande wake Majaliwa Yohana kutoka kitengo cha Sheria Halmashauri ya Wilaya ya Geita akizungumza na wananchi hao amesisitiza kutumia mabaraza ya usuluhishi kutatua migogoro hiyo badala ya kukimbilia kuripoti vituo vya Polisi ambapo wakati mwingine panakuwa sio sehemu sahihi ya wao kupata suluhu ya migogoro yao ya  kifamilia kama ambavyo wangeweza kupata suluhu katika mabaraza hayo.

Jackson Chami Afisa Ustawi wa Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Geita ametumia nafasi hiyo kuongea na wananchi hao huku akiwakumbusha kutofumbia macho vitendo vya ukatili hasa kwa watoto, ambapo pia amesisitiza kuwa manyanyaso na ukatili havivumiliki hivyo ni wajibu wa jamii kukemea na kutoa taarifa haraka pale wanapoona watu wananyanyasika au kufanyiwa vitendo vya ukatili katika maeneo yao.

Kwa upande wake diwani wa kata ya Nyarugusu Mhe. Swalehe Juma Msene akizungumza na wananchi hao amewataka kuendelea kujitokeza kwa wingi yanapotokea masuala kama hayo ya elimu ya msaada wa kisheria ili kuendelea kuwaongezea wananchi hao uelewa wa masuala ya haki mbalimbali za msingi, ambapo pia ameishukuru Halmashauri ya Wilaya ya Geita kuwatumia wataalamu hao kuwafikia wananchi kwenye maeneo yao na kuwapatia huduma hiyo.

Wananchi mbalimbali katika Kata ya Nyarugusu wamejitokeza kupata elimu na msaada wa kisheria kutoka kwa wataalamu wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita walioweka kambi ya siku moja katika kata hiyo kwa ajili ya shughuli hiyo.

Aidha wamepatiwa ushauri na maelekezo kuhusu changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwemo migogoro ya ndoa na kutelekeza watoto, migogoro ya ardhi, masuala ya mirathi, masuala ya talaka na haki mbalimbali za binadamu.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa