• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

Geita DC yajipanga kukamilisha mapema zoezi la anwani za makazi na postikodi kabla ya muda uliopangwa

Posted on: February 23rd, 2022

Waheshimiwa Madiwani pamoja na watendaji wa kata zote za Halmashauri ya Wilaya ya Geita, wamepatiwa mafunzo maalumu leo tarehe 23 februari, 2022 ya kuwaongezea uelewa kuhusu utekelezaji  wa zoezi la anwani za makazi na postikodi.

Mafunzo hayo yametolewa na kamati ya zoezi la anwani za makazi na postikodi kwenye baraza la madiwani maalumu lililofanyika makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita Nzera.

Mwenyekiti wa kamati hiyo Hongera Edward amesema Serikali kupitia sera ya Taifa ya posta ya mwaka 2003, imedhamiria kuanzisha mfumo wa anwani zinazoendana na majina ya mitaa ambapo watu binafsi na maeneo ya biashara yatatambulishwa kwa kutumia majina ya maeneo yaliyopo pamoja na postikodi yao, ikiwa ni utekelezaji wa dira ya Taifa ya maendeleo ya mwaka 2025, yenye lengo la kuwaondoa watanzania kwenye umaskini na kuinua ubora wa maisha yao.

Zoezi la anwani za makazi na postikodi linatekelezwa kupitia Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ikishirikiana na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ambapo linatakiwa kukamilika kabla ya mwezi mei 2022, huku halmashauri ya wilaya ya Geita ikipanga kukamilisha zoezi hilo aprili 8 mwaka 2022.

Aidha kukamilika kwa zoezi hilo kutawezesha kufanyika kwa sensa ya watu na makazi zoezi linalotarajiwa kufanyika kuanzia mwezi Agosti, 2022.

Miongoni mwa mambo waliyofundishwa madiwani pamoja na watendaji hao wa kata ni pamoja na maana ya mfumo wa anwani za makazi na postikodi, manufaa ya mfumo wa anwani za makazi, vigezo vya uundaji wa majina ya barabara na mitaa, utaratibu wa utoaji wa jina la barabara au mtaa.

Mambo mengine ni taratibu za kufuatwa, vibao vya majina ya barabara au mtaa, utoaji na ubadilishaji wa majina ya barabara au mtaa, majina yasiyopendeza kimaadili, majina yenye viashiria vya kuharibu amani, utulivu na umoja wa kitaifa pamoja na uwekaji wa miundombinu ya anwani za makazi.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Charles Kazungu amewataka wajumbe wa kamati ya zoezi la anwani za makazi na postikodi kuzingatia mawazo yaliyotolewa na madiwani hao ili kazi iwe rahisi na nzuri zaidi.

Mheshimiwa Kazungu amesema wao kama madiwani wanalo jukumu kubwa la kwenda kuhamasisha wananchi ili zoezi litakapoanza wawe na uelewa mzuri.

Ameomba kila diwani katika kata yake na wale wa viti maalumu kutambua kwamba wanalo jukumu  la kwenda kuhamasisha wananchi kuelewa zoezi hilo na kuwataka watendaji wa kata kusimamia kwa weledi zoezi hilo.

Hata hivyo Mkuu wa Wilaya ya Geita Wilson Shimo amewataka watendaji wote kuendelea na zoezi hilo kwa kasi bila kubagua kundi lolote ikiwemo watu wenye ulemavu na Taasisi yoyote kuanzia ngazi za mwanzo.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI. June 05, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA URATIBU WA MWENGE WA UHURU MKOA YATEMBELEA YATEMBELEA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA, GEITA.

    June 24, 2025
  • ZAIDI YA BILIONI 50 ZATUMIKA KUKAMILISHA MIRADI GEITA 2020-2025.

    June 21, 2025
  • RAISI DKT. SAMIA AZINDUA DARAJA LA KIGOGO-BUSISI.

    June 19, 2025
  • WATUMISHI WILAYANI GEITA WAKUMBUSHWA SUALA LA KUJIFANYIA TATHMINI.

    June 18, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa