• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

DC SHIMO AWATAKA WAVUVI NA WASAFIRI KUCHUKUA TAHADHARI KABLA YA KUINGIA MAJINI KWA USALAMA WA MAISHA YAO

Posted on: June 12th, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Wilson Shimo ametoa wito kwa wananchi wanaofanya shughuli za uvuvi na usafirishaji kufuata taratibu na sheria zilizowekwa na Serikali kwa lengo la kulinda usalama wa raia na kufanya uvuvi endelevu.

Mhe. Shimo ameyasema hayo Juni 11, 2022 alipoambatana na kamati ya ulinzi na usalama Wilaya ya  Geita kuzungumza na viongozi, wafanyabiashara,  na wananchi wa kijiji cha Ihumilo  eneo la Mwalo wa makatani katika kata ya Nkome.

Amewataka viongozi wa mialo yote kusimamia sheria na tahadhari zote kabla ya kuingia majini ikiwemo uvaaji wa maboya ili kudhibiti ajali za majini ambazo hupoteza maisha ya watu ambapo kwa kipindi cha wiki moja kuna watu  watatu wamepoteza maisha kwa ajali za majini.

Amewataka pia wavuvi wa mialo yote ukiwemo mwalo wa Makatani kufanya uvuvi endelevu ambao unazingatia kiwango halali cha nyavu zinazotambulika na kuidhinishwa kutumika katika shughuli hizo za uvuvi wa samaki, kuliko kutumia dhana haramu ambazo zinatoa hadi samaki wachanga jambo ambalo ni hatari kwa kuwa linatishia kupotea kwa samaki wakubwa miaka ijayo.

Baada ya kusikiliza kero za wananchi na kuzijibu Mhe. Shimo, amewataka wanachi wote kwa pamoja kuzingatia katazo la kutoonekana watoto  wenye umri wa kuwa shule wakifanya kazi katika maeneo hayo, huku akitoa wito wa jamii kuwawezesha kwa chakula mashuleni ili kuongeza ufaulu kwa watoto wao, sambamba na kuhifadhi Misitu na kupanda miti ili kuendeleza uhifadhi wa mazingira.

Kwa upande wake Insp. Edward Lukuba Afisa Zimamoto Wilaya ya Geita akiongea na wananchi hao amekumbusha pia kuchukua tahadhari zote kabla ya kuingia kwenye maji kwa kuhakikisha wanakuwa na maboya, Majaketi ya kuzuia kuzama (Life Jackets), na filimbi ambavyo vifaa hivyo vinaweza kuzuia madhara makubwa endapo chombo kitapata ajali.

Insp. Lukuba amewasisitiza pia  kubeba mizigo au watu kulingana na mahitaji ya vyombo  vya usafiri wanavyotumia kwa kuacha kuzidisha, ili kuepuka ajali za vyombo vya majini zinazosababishwa na uzidishwaji wa mizigo.

Wakati huo huo amesema kuwa kila chombo cha majini kinapaswa kuwa na kifaa cha kuzimia moto (fire extinguisher), na kinasa radi ili kuepuka ajali za moto ndani ya maji ambazo zinaweza kusababishwa na radi kama chombo husika hakijafungwa kifaa maalumu cha kunasa radi.

Sambamba na hayo amewakumbusha wananchi pia kuchukua tahadhari za mioto majumbani kwa kuwa na vifaa vya kuzimia moto (Fire extinguisher), na kuwa na matumizi sahihi ya umeme na majiko ya gesi ambayo yamekuwa yakisababisha ajali za mioto mara kwa mara majumbani huku akisisitiza matumizi sahihi ya majiko ya gesi ikiwa ni pamoja na kubadilisha vifaa ya majiko hayo kwa wakati kama wanavyoshauriwa na wataalamu.  



Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa