• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

DC SHIMO ATAJA UMOJA NA MSHIKAMANO KUWA NGUZO KUU YA MAENDELEO TUNAPOSHEREHEKEA MIAKA 61 YA UHURU

Posted on: December 7th, 2022

Na. Michael Kashinde

Kuelekea kuadhimisha miaka 61 ya Uhuru wa Tanganyika Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Wilson Samwel Shimo ametoa rai kwa watanzania kuanzia ngazi za familia kuhakikisha wanailinda, kuitunza na kuihifadhi Amani ya nchi yetu ili kuendelea kuona mabadiliko katika sekta mbalimbali hapa nchini ikiwemo uchumi.

Ameyasema hayo Disemba 7, 2022 akiwa katika Kata ya Katoro katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita akiongoza zoezi la usafi na kupanda miti katika Kata hiyo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali za kijamii kuelekea kilele cha maadhimisho ya Miaka 61 ya Uhuru wa Tanganayika hapo Disemba 9, 2022.

Mhe. Shimo akizungumza na viongozi na wananchi mbalimbali katika Hospitali yenye hadhi ya Wilaya Katoro pamoja na Kituo cha Afya Katoro, amesema kuwa siri ya mafanikio makubwa yanayoonekana kwa sasa baada ya Uhuru, ni Umoja na Mshikamano uliopo baina ya watanzania na viongozi wao kuanzia awamu ya kwanza hadi sasa awamu ya sita, ambao umechangia kubadilisha hali ya nchi ya Tanzania kimaendeleo na kiuchumi.

DC Shimo amesema kuwa wakati nchi inapata Uhuru wake mwaka 1961 hakukuwa na huduma bora za kijamii kama vile hospitali, barabara na maji kama ilivyo sasa, huku akiwataka watanzania kuendelea kuwapongeza viongozi wa Taifa hili kwa mchango wao mkubwa katika maendeleo ambapo pia amewaasa watanzania kuendelea kuwaunga mkono viongozi wao ili  kupata maendeleo Zaidi.

Akiongoza zoezi la usafi wa mazingira na kupanda miti DC Shimo amewataka pia wananchi kuazia majumbani, sehemu binafsi na za wazi  kupanda miti ya aina mbalimbali ikiwa ni sehemu ya utunzaji wa mazingira na kudhibiti mabadiliko ya tabia ya nchi ambapo upandaji huo wa miti ya kutosha unaweza kuwa na faida mbalimbali kama vile lishe bora kwa miti ya matunda, kivuli na faida mbalimbali za kiuchumi huku akiwasisitiza kuitunza vizuri miti hiyo ambayo itakuwa kumbukumbu ya miaka 61 ya Uhuru.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Mji Mdogo wa Katoro Bw. Damian Aloyce amesema kuwa mpaka sasa Kuna jumla ya miti 4,000 ambapo katika eneo la Hopitali yenye hadhi ya Wilaya Katoro tayari imepandwa miti 130, huku miti mingine ikiendelea kugawiwa katika Taasisi mbalimbali zikiwemo shule kwa ajili ya zoezi hilo la kupanda miti ikiwa ni sehemu ya shughuli zinazofanyika katika maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru wa Tanganyika.

Taasisi nyingine zilizopatiwa miti kwa ajili ya kupanda ni pamoja  shule ya msingi Mji mwema  miti 200, eneo la shule ya sekondari Ludete miti 300, shule ya sekondari Mgunga miti 400, shule ya sekondari Bulengahasi  miti 400, na shule ya Sekondari ya Mama Samia ikitarajiwa kupatiwa pia miti 400.

Kaimu Mhifadhi misitu Wilaya ya Geita Sandusy Ngunyale amesema kuwa zoezi la kupanda miti limeanza Disemba 6, 2022 katika vijiji vya Buziba na Bufunda kabla ya kufika Katoro ambapo licha ya kuwashukuru wananchi kwa namna walivyoshiriki katika zoezi hilo ameendelea kuwahamasisha wananchi kuchukua na kupanda miti isiyopungua mitano majumbani.

Aidha Ngunyale ametoa mwongozo kwa watu wanaoishi vijijini kufika katika ofisi za watendaji wa vijiji ili kupatiwa miti ya kwenda kupanda, ambapo pia kwa wakazi wa Geita wanaweza kufika katika kitalu cha Wakala wa Misitu kilichopo Magogo na kupatiwa miti hiyo huku wakihamasishwa kuitunza ili ikue kama inavyotarajiwa.

Picha zaidi.


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa