• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

DC KOMBA ATEMBELEA KIWANDA CHA KUCHAKATA MPUNGA NYABUSAKAMA AMCOS LTD-GEITA DC

Posted on: May 28th, 2024

NYAMWILOLELWA

Na: Hendrick Msangi

NYABUSAKAMA ni Chama cha Ushirika kinachoundwa na muunganiko wa Vijiji Saba ambavyo ni Nyakabale, Nyansalwa, Nungwe, Bugulula, Saragulwa, Kasota na Manga chenye jumla ya wanachama 426.

Chama hicho kilianzishwa mwaka 2016 na kupata ufadhili kutoka Mgodi wa dhahabu wa Geita (GGML) kwa kuwajengea maghala ya kuhifadhia mpunga na alizeti kutoka kwa wakulima Saragulwa na Kasota.

Akisoma taarifa ya Chama hicho mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Abdallah Komba alipotembelea kiwanda hicho May 26, 2024, Mwenyekiti wa bodi ya chama hicho ndugu Sakumi Makungu amesema chama hicho kimewawezesha wakulima kutumia fursa zilizopo katika masoko ya mpunga na alizeti kwa kuzalisha mpunga na alizeti kwa kuzingatia kilimo cha kisasa.


Ghala lililojengwa na kampuni ya mgodi wa dhahabu ya Geita (GGML) kwa kiasi cha shilingi 658,000,000 lenye uwezo wa kuhifadhi gunia 30,000 za mpunga sawa na tani 2,700 kata ya Nyamwilolelwa Halmashauri ya Wilaya ya Geita. Mradi huo unawanufaisha wakulima wa mpunga 1,653 kupitia chama cha Ushirika (AMCOS) ya Nyabusakama, wakulima wengine wa kijiji cha Saragulwa na vijiji jirani kwa kuhifadhi na kuongeza thamani.

Aidha ndg Sakumi amesema chama hicho kimeendelea kuongeza thamani ya mpunga na alizeti kwa kutumia kiwanda cha kisasa cha kukoboa, kugredi na kupaki mchele, pamoja na mashine ya kukamua mbegu za alizeti kupata mafuta safi ya alizeti na kuuza mazao yao kwa kuzingatia mbinu za ujasiliamali ili kuwa wakulima wafanyabiashara.

Wanachama hao wameiomba ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita kuwajengea uwezo wa kupata mkopo kwani mkopo walio nao kutoka benki una waumiza na kusema Bora waurudishe mkopo huo kwani kwao umekuwa changamoto.

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Abdallah Komba akiwa na baadhi ya wajumbe wa timu ya menejimenti Halmashauri ya Wilaya ya Geita wakisikiliza namna kiwanda hicho kinavyofanya kazi. Kiwanda  hicho kina uwezo wa kukoboa tani 1.2 za mpunga kwa saa

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita ndg Karia Rajabu Magaro amewataka wanachama hao kujiandikisha ili wanufaike na Mikopo inayotolewa na Halmashauri kwani haina riba.

Pamoja na hayo, wajumbe wa bodi ya chama hicho wameiomba ofisi ya Mkuu wa Wilaya iwasaidie ili wawe sehemu ya wasambazaji wa mchele kulisha mgodi  wa dhahabu wa Geita (GGML ) ili chama hicho kiendelee kukua.

Akiwa katika ghala hilo lililojengwa na kampuni ya mgodi wa dhahabu ya Geita (GGML) kwa kiasi cha shilingi 658,000,000 lenye uwezo wa kuhifadhi gunia 30,000 za mpunga sawa na tani 2,700 na kukoboa tani 1.2 za mpunga kwa saa, Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Abdallah Komba ameipongeza bodi ya chama hicho cha Ushirika cha NYABUSAKAMA na kampuni ya mgodi wa dhahabu wa Geita (GGML) kwa uwekezaji huo na kukitaka chama hicho kuendelea kuwa wabunifu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita ndg Karia Rajabu Magaro akiwa na wajumbe wa bodi ya Chama cha Ushirika cha Nyabusakama (AMCOS) ya Nyabusakama, AMCOS Ltd wakati alipotembelea Kiwanda hicho cha Kuchakata Mpunga na kuwashauri wakope mikopo isiyo na riba inayotelewa na serikali kupitia Halmashauri

“Mkawe na ushirika wa kisasa ili kuendelea kupata vyanzo vingine vya mapato katika kuendesha mradi kwa kuwa na miradi ya kujiongezea kipato kwa kuzalisha, kununua na kuuza badala ya kutegemea wanachama pekee” amesema Mhe Komba

Magunia ya Mpunga wa wanachama yakiwa yamehifadhiwa kwenye ghala hilo lenye uwezo wa kuhifadhi gunia 30,000 za mpunga sawa na tani 2,700. Mpaka sasa Idadi ya wanachama ni 426, wanaume wakiwa 313 na wanawake 113

Wajumbe wa bodi hiyo wamemshukuru Mhe Mkuu wa wilaya na timu ya menejemeneti ya Halmashauri ya wilaya ya Geita kwa kuwatembelea huku kauli mbiu yao ikisema Nyabusakama-Pamoja tujenge uchumi.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa