• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI CSR

Posted on: October 5th, 2021

Baraza la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Geita limepitisha mapendekezo ya mpango na bajeti ya wajibu wa kampuni kwa jamii (CSR) kwa mwaka 2021 wenye jumla ya shilingi bilioni 4 na milioni 300.

Baraza hilo lililokutana hii leo Oktoba 5, katika mkutano maalumu wa baraza la Madiwani katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Nzera, limejadili mapendekezo ya Mpango huo na bajeti unaoonesha miradi yote iliyoanzishwa lakini bado haijakamilika.

Awali akiwasilisha mapendekezo ya mpango huo Mkuu wa Idara ya maendeleo ya jamii Bi.Furaha Chiwile alisema kuwa menejimenti imefanya tathmini kama ilivyoazimiwa na kikao cha kamati ya fedha, uongozi na mipango cha Agosti 9, 2021 na kubaini kuwa jumla ya miradi 1,251 iko katika hatua mbalimbali ikihitaji kiasi cha shilingi bilioni 15 na milioni 800 ili kuanza kutumika.

Ameendelea kusema kuwa kutokana na wingi wa miradi na gharama zinazohitajika ni dhahiri kuwa inahitajika zaidi ya miaka mitatu kuikamilisha miradi hiyo kwa kutawanya rasilimali kidogo kidogo kwa kila mradi, hali inayolazimu kuchagua miradi michache ambayo ikipewa fedha itaweza kukamilika na kuanza kutumika ili kudhihirisha dhana ya thamani ya fedha.


Ameendelea kusema kuwa kutokana na wingi wa miradi na gharama zinazohitajika ni dhahiri kuwa inahitajika zaidi ya miaka mitatu kuikamilisha miradi hiyo kwa kutawanya rasilimali kidogo kidogo kwa kila mradi, hali inayolazimu kuchagua miradi michache ambayo ikipewa fedha itaweza kukamilika na kuanza kutumika ili kudhihirisha dhana ya thamani ya fedha.

Aidha mpango uliopendekezwa na kupitishwa kwa mwaka huu 2021 unatarajiwa kugharimu kiasi cha shilingi bilioni 4 na milioni 300 ukiwa umezingatia maoni ya wadau na mapendekezo kutoka kwenye kata kwa kuhakikisha kwamba miradi itakayotengewa fedha inakamilika na kuanza kutumika.

Vigezo vingine ni pamoja na  kuwa na uwiano kati ya miradi ya ujenzi wa miundombinu na  huduma za jamii, miradi ya kiuchumi kwa ajili ya kuongeza kipato ili kupunguza umasikini wa kaya na kuimarisha masuala ya ulinzi na usalama.

Aidha Miradi mingine ni pamoja na Afya bilioni 2 na milioni 114, Elimu msingi milioni 464, Elimu Sekondari milioni 256, Usimamizi na ufuatiliaji milioni 74, Utafiti na Maendeleo milioni 77 ambapo kwa ujumla inagharimu kiasi cha shilingi bilioni 4 na milioni 300.




Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI. June 05, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA URATIBU WA MWENGE WA UHURU MKOA YATEMBELEA YATEMBELEA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA, GEITA.

    June 24, 2025
  • ZAIDI YA BILIONI 50 ZATUMIKA KUKAMILISHA MIRADI GEITA 2020-2025.

    June 21, 2025
  • RAISI DKT. SAMIA AZINDUA DARAJA LA KIGOGO-BUSISI.

    June 19, 2025
  • WATUMISHI WILAYANI GEITA WAKUMBUSHWA SUALA LA KUJIFANYIA TATHMINI.

    June 18, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa