• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

BARAZA LA MADIWANI LAMPONGEZA MKURUGENZI KWA UKUSANYAJI WA MAPATO

Posted on: November 14th, 2024

Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Geita katika Mkutano wake wa kawaida robo ya kwanza Kwa mwaka wa fedha 2024/25 uliofanyika Novemba 14,2024 limempongeza Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg Karia Rajabu Magaro kwa usimamizi mzuri wa Miradi sambamba na ukusanyaji wa mapato.

Akizungumza katika Baraza hilo Mhe Diwani wa kata ya Nyamalimbe Mhe Jeremiah Ikangala amesema Mkurugenzi anapaswa kuendelea kutiwa moyo kwa kuwa usimamizi wa Miradi ya Maendeleo unaonekana pamoja na ukusanyaji na matumizi ya Mapato ndani ya Halmashauri. "Tuendelee kumtia moyo Mkurugenzi ili kasi aliyo nayo katika usimamizi wa Miradi na ukusanyaji wa mapato iendelee ili Halmashauri isonge mbele" amesema Mhe Ikangala.

Katika taarifa yake Kwenye Baraza hilo Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita ndg Karia Rajabu Magaro ametoa rai kwa Waheshimiwa Madiwani kuendelea kutoa ushirikiaono katika usimamizi wa Miradi ya Maendeleo katika kata zao ili Miradi hiyo iendelee kukamilika kwa wakati na kuwanufaisha Wananchi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg. Karia Magaro akiwasilisha taarifa ya utendaji mbele ya baraza la madiwani  


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe Charles Kazungu amewataka Madiwani kuendelea kusimamia vema miradi inayo tekelezwa kupitia Fedha za Serikali kuu na Mapato ya ndani ili Miradi hiyo ikamilike kwa wakati. " Tusimamie Fedha za Miradi na niwatake Saruji ambazo ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji inazitoa  tupange Mikakati mapema ili zisiharibike zilete tija kwenye kazi tulizokusudia" amesema Mhe Kazungu.

Vile vile Mhe Kazungu ameilekeza ofisi ya Mhandisi wa Halmashauri kukamilisha ramani na BOQ kwa wakati ili kasi ya Miradi isisimame”Nitoe rai kwenu tuongeze kasi ili tuweze kutekeleza miradi yetu ya maendeleo.”amesema Mhe Kazungu.

Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kupitia mapato ya ndani imetoa mifuko 100 ya saruji kwa kata zote 37 za Halmashauri ya Wilaya ya Geita ili kuendelea kuchochea shughuli za maendeleo ndani ya Halmashauri. “Niwaombe waheshimiwa Madiwani kuendelea kutoa vipaumbele kwenye maeneo yanayokumbwa na maafa ili kuyanusuru kwa haraka huduma za kijamii zisisimame” ameongeza Mkurugenzi.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji amesihi Madiwani kuendelea kuwahamasisha wananchi kuwa na vikundi na kujiandikisha ili kupata mikopo ya asilimia 10 ambapo halmashauri ina jumla ya shilingi Bilioni 1.7 kwa ajili ya kukopesha vikundi.

Jumla ya kiasi cha Shilingi Bilioni 2.4 kimekusanywa katika robo ya kwanza ambacho ni sawa na asilimia 28 ya mapato yaliyotarajiwa kukusanywa kwa mwaka.

Akihitimisha mkutano huo Mhe Kazungu amewataka waheshimiwa madiwani na wataalam wa Halmashauri kila mmoja kusimama kwenye nafasi yake ili kuendelea kudhibiti mapato ya Halmashauri huku akiwasisitiza madiwani hao kuendelea kutoa ushirikiano kwa watumishi.

“Tuendelee kukusanya kwenye vyanzo ambavyo vipo chini ili kufikia malengo mapema na haraka na yeyote atakayekwamisha swala la ukusanyaji wa mapato sitamvumilia”amesema Mhe Kazungu.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa