• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LIMEWASILISHA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA SERIKALI KWA KIPINDI CHA JANUARI HADI MACHI 2024

Posted on: May 8th, 2024

BARAZA la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Geita leo May 8,2024 katika Kikao chake cha kawaida, limewasilisha taarifa za utekelezaji wa Shughuli za Serikali ngazi ya kata kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2024.


Jumla ya Kata 37 zimewasilisha taarifa katika baraza hilo ambapo Waheshimiwa Madiwani wameeleza changamoto mbalimbali zinazozikabili kata hizo zikiwepo za kuharibika kwa miundombinu ya barabara zinazounganisha maeneo mbalimbali kunapopelekea magari kushindwa kupita ikiwa ni pamoja na uharibifu wa miundombinu ya madarasa kutokana na mvua kubwa zenye upepo mkali zinazoendelea kunyesha.

Aidha Madiwani hao katika uwasilishaji wa taarifa za utekelezaji wa Shughuli za Serikali ngazi ya kata wameeleza changamoto ya uhaba wa walimu wa kike katika Shule nyingi na kuitaka ofisi ya Mkurugenzi kuendelea kufanya msawazo wa walimu wa kike ili kumaliza changamoto hiyo.


Pamoja na hayo, Waheshimiwa Madiwani wamesema kuchelewa kwa ukamilishwaji wa Miradi ya Maendeleo ambayo kampuni ya GGML inaietekeleza kunatokana na vifaa vya ujenzi kutokufika site kwa wakati na kupelekea mafundi kukaa site bila kazi.

Akizungumza katika Baraza hilo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe Charles Mabeyo Kazungu ameilekeza ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kuwaita wasimamizi wa Miradi kutoka kampuni ya GGML kushiriki vikao vya Baraza la Madiwani ili waweze kuzisikiliza changamoto zinazowasilishwa na Waheshimiwa Madiwani.


Aidha Mhe Kazungu ameiomba Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kuingilia kati Miradi inayotekelezwa na mfuko wa CSR kutoka GGML ili kuharakisha ukamilishwaji wa Miradi viporo ikiwepo maboma yaliyo jengwa kwa nguvu za Wananchi.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Nyamilolelwa Mhe Mashauri Gambula amesema mapato mengi ya Halmashauri yanapotea kufuatia ubovu wa barabara hasa barabara ya Saragulwa - Mgusu kukatika na kupelekea kikwazo katika Shughuli za uchumi kwa wananchi wa kata zote mbili na nje ya Halmashauri.


Akifunga kikao cha Baraza hilo kwa siku ya kwanza, Mhe Kazungu amewashukuru Waheshimiwa Madiwani kwa uwasilishaji mzuri wa Shughuli za Serikali ambazo zinatekelezwa kwenye kata zao, na kuwataka kuendelea kutatua changamoto ambazo zipo kwenye kata zao huku wakiwashirikisha Wananchi na wadau mbalimbali ili kuendelea kukabiliana na changamoto. 


Pamoja na hayo amewataka Waheshimiwa Madiwani kuendelea kuwaelimisha wananchi katika maeneo yao ikiwa ni pamoja na kuwataka kuwa wavumilivu kwani Serikali ipo kazini, kurekebisha miundombinu iliyo haribiwa na mvua kubwa zilizokuwa zikiambatana na upepo mkali.

"Muwaambie Wananchi kuwa na tahadhari kutokana na mabadiliko ya Hali ya hewa yanayotokea kutokana na mvua na upepo mkali ili wawe salama." Amesema Mhe Kazungu.


Kikao hicho kimehudhuriwa na wakuu wa Idara na vitengo kutoka Halmashauri ya wilaya ya Geita, Viongozi wa Chama na Serikali . Baraza hilo litaendelea siku ya tarehe 9, May 2024.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa