Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mhe. Hashim Komba, amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita, itaendelea na juhudi za kuhakikisha inatoa huduma bora, hususani katika sekta za Afya, Elimu, na Maji ili kusudi wananchi waweze kuondokana na changamoto zinazowakabili kwenye maeneo yao.
Akizungumza wakati wa ziara maalumu tarehe 16, Mei katika Kata ya Lwenzera, Wilayani Geita, ambapo alipata nafasi ya kutembelea miradi na kusikiliza kero za wananchi katika vijiji vya Nyalubanga, Idosero na Bweya, Mhe. Komba amesema serikali, kupitia kwa viongozi ambao wamepewa dhamana kwenye ngazi za Vijiji na Vitongoji, ina wajibu wa kusimamia na kuhakikisha miradi ambayo inatekelezwa, inawafikia wananchi na kuwanufaisha.
Katika Zahanati ya Nyalubanga ambayo ipo kwenye hatua za mwishoni za ukamilishaji, ikiwa ni michango ya wananchi pamoja na fungu la CSR, Mhe. Komba amewapongeza wananchi waliojitoa kwenye ukamilishaji wa jengo hilo pamoja na ujenzi wa Nyumba ya Mtumishi, huku akiwasisitiza Wahandisi kuhakikisha mradi huo unakamilika mapema ili wananchi waweze kuanza kupata huduma.
Kwa upande wake, Dkt. Alphonse Bagambabyaki akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi, amesema kuwa kwa mwaka wa fedha 2024/2025, Halmashauri imeweza kuvuka malengo iliyojiwekea kwenye ukusanyaji wa mapato, na kwamba kabla ya mwaka mpya wa fedha, Halmashauri itahakikisha inatoa fedha ili ujenzi wa Zahanati hiyo uweze kukamilika.
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita
Simu: +225 282520061
Mobile:
Barua pepe: info@geitadc.go.tz
Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa