• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WATOTO 66,000 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WAMEPATIWA CHANJO YA POLIO KATIKA SIKU YA KWANZA YA UZINDUZI WA KAMPENI HIYO

Posted on: May 20th, 2022

Katika siku ya kwanza ya Utekelezaji wa zoezi la Chanjo ya Polio Halmashauri ya Wilaya ya Geita imefanikiwa kutoa Chanjo kwa watoto elfu 66 tofauti na elfu 44 idadi iliyokuwa imetegemewa awali kwa siku ya kwanza ikiwa ni mafaniko ya zaidi ya asilimia 100 katika utekelezaji wa zoezi hilo.

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Dr.Modest Buchard Lwakahemula (MD,MPH) ameeleza mafanikio hayo katika siku ya kwanza ya utekelezaji wa zoezi hilo lililoanza Mei 18 na kutarajiwa kukamilika Mei 21 mwaka huu.

Dr. Lwakahemula ametumia nafasi hiyo kutoa elimu kwa kusema kuwa ugonjwa wa Polio ni hatari na usio na tiba na endapo mtoto akiupata anaweza kudumu nao milele jambo ambalo ni hatari kwa familia, jamii, na hata taifa kwa ujumla kutokana na kulazimika kutumia rasilimali nyingi kumhudumia mgonjwa.

Aidha ametumia fursa hiyo kuishukuru Serikali kwa ujumla na wadau mbalimbali ambao wameihamasisha jamii kujitokeza katika kufanikisha zoezi hilo hadi kuvuka malengo huku akiendelea kuwahamasisha ambao hawajijitokeza kutumia siku zilizobaki kupata huduma hiyo.

Kwa upande wake Msilanga Manyasi Mganga Mfawidhi zahanati ya Nyasembe na Timotheo Aloka Mganga Mfawidhi  zahanati ya Inyala wamebainisha  kuwa zoezi hilo linafanyika vizuri katika maeneo yao bila kukutana na changamoto kubwa na wameendelea kutoa elimu kwa wananchi wanaoonekana kuwa na mashaka juu chanjo hiyo.

Baadhi ya wananchi waliokuwa katika kituo cha kutolea chanjo katika zahanati ya Inyala akiwemo Bi.Mwaidi Athumani amesema kuwa amehamasika kuleta watoto wake kupata chanjo hiyo  kwa hofu ya watoto hao kupoozaikiwa ni matokeo ya ugonjwa wa Polio.

Kampeni ya Kitaifa ya Ugonjwa wa Polio ambayo katika Mkoa wa Geita ilizinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mh. Rosemary Senyamule Mei 18 mwaka huu kwa kuwahamasisha wananchi kushiriki kikamalifu katika chanjo hiyo inayotolewa katika vituo mbalimbali vya huduma za Afya huku wataalamu wengine wakipita nyumba hadi nyumba kutoa chanjo hiyo.

 

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa