• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 2.1 JIMBO LA GEITA YAKAGULIWA NA KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO

Posted on: January 20th, 2026

Geita

Kamati ya Fedha uongozi na Mipango Halmashauri ya Wilaya ya Geita Januari 19, 2026 imefanya ziara ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika jimbo la Geita.

Akizungumza katika ziara hiyo Diwani wa Kata ya Butobela Mhe Pascal Mapung’o amewataka Wahandisi wa Halmashauri kuhakikisha wanashughulikia kasoro zote ambazo zimeonekana kwenye miradi hiyo ili iweze kukamilika kwa wakati na kuanza kutumika.

“Kasoro zote ambazo tumeziona kwenye miradi zifanyiwe kazi kwa wakati ili miradi ikamilike kwa wakati na kuanza kutumika” Amesema Mhe Mapung’o

Shule mpya ya Mchepuo wa Kiingereza Nzera Modern Pre & Primary School wenye thamani ya shilingi Milioni 573,791,319.36 kutoka CSR ya Mgodi wa Dhahabu wa Geita. Shule hiyo imekamilika tayari kupokea wanafunzi

Aidha Mhe Mapung’o amewataka wasimamizi wa miradi kuzingatia maelekezo yanayotolewa na Halmashauri ili miradi hiyo ikamilike kulingana na gharama zilizowekwa kwa kila mradi.

Naye diwani wa kata ya Chigunga Mhe Anthony Anacreti ametoa wito kwa viongozi wa kata na vijiji kuendelea kuwahamasisha wananchi kushiriki shughuli za maendeleo katika maeneo yao miradi inapotekelezwa.

Kwa upande wake mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji Bi Sarah Yohana ambaye pia ni Afisa Mipango Halmashauri ya Wilaya ya Geita amewataka mafundi ujenzi wanaotekeleza miradi hiyo kuongeza kasi ili miradi hiyo ikamilike kwa wakati.

Ujenzi wa mradi wa shule ya msingi Kakubilo  Madarsa 4 na matundu 6 ya vyoo Pamoja na ukarabati wa vyumba 8 vya madarasa na ofisi 2.Kukamilika kwake kutapunguza msongamano wa wanafunzi kwenye madarasa na kuweka mazingira safi ya kujisomea.

“Niwatake mafundi kuongeza kasi ya ujenzi ikiwa ni pamoja na wasimamizi wa miradi hii kuwalipa mafundi ujenzi kwa wakati” Amesema Bi Sarah

Vilevile Bi Sarah ametoa wito kwa Wasimamizi wa miradi kuwashirikisha wananchi katika maeneo yao utekelezaji wa miradi na kuwajulisha wananchi fedha za miradi zinapoingia ili wananchi waweze kushiriki kikamilifu miradi ya maendeleo.

Kamati hiyo ikiwa na wataalam kutoka Halmashauri, imetembelea miradi ya ujenzi wa shule, ukarabati wa miundombinu ya madarasa,ujenzi wa nyumba za watumishi Pamoja na uzio katika nyumba hizo miradi ambayo thamani yake ni kiasi cha Shilingi Bilioni 2.1.

Miradi hiyo ambayo imetembelewa na kamati ya fedha uongozi na mipango chanzo cha fedha ni Mapato ya ndani, BOOST na wajibu wa Kampuni ya mgodi wa dhahabu wa Geita kwa jamii (CSR-GGML)

Halmashauri ya Wilaya ya Geita inaendelea kuishukuru serikali inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kutoa fedha nyingi za miradi, Pamoja na waheshimiwa wabunge kwa jitihada zao za kuleta maendeleo kwa wananchi wa Geita.

Tangazo

  • HIZI HAPA AJIRA ZA KUMWAGA GEITA DC July 15, 2025
  • TANGAZO LA KUKODI MAGARI August 31, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 02, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 2.1 JIMBO LA GEITA YAKAGULIWA NA KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO

    January 20, 2026
  • MRADI WA ELIMU WA BRIDGE-TZ WAZINDULIWA RASMI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA.

    January 07, 2026
  • CRDB YAKABIDHI VIFAA NETIBOLI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA.

    January 05, 2026
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA YATOA MIKOPO ISIYO NA RIBA YA SHILINGI MILIONI 500 KWA VIKUNDI 58

    January 05, 2026
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa